Kambi Maalum ya Upimaji na Matibabu ya Moyo Yawafikia watu 302 Arusha
Mkurugenzi wa Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) ambayo kwa sasa inasimamiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tatizo Waane akipokea cheti cha shukrani kutoka kwa Daktari Bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watu wazima na Mshauri wa Upasuaji wa moyo kupitia tundu dogo kutoka National Heart Institute (NHI) nchini Misri Prof. Ghada Kazamel baada ya kumalizika kwa kambi maalumu ya siku mbili ya uchunguzi na matibabu ya moyo kwa watoto na watu wazima iliyokuwa ikifanyika katika Hospitali ya ALMC na wataalamu wa JKCI, ALMC, Heart to Heart Association for Sustainable Development na Egyptian African Heart Association (EAHA). Daktari Bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Goup Eva Wakuganda akimpima kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (ECHO) mtoto wakati wa kambi maalumu ya siku mbili ya uchunguzi na matibabu ya moyo iliyofanywa na wataalamu wa JKCI, ALMC na Heart to Heart Association f...