Maabara inayotumia akili unde kupunguza muda wa kusubiri majibu ya vipimo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimweleze mwandishi wa habari wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Ibrahim Chawe kuhusu maabara ya kisasa inayotumia akili unde (AI) wakati wa kambi maalumu ya uchunguzi wa afya kupitia maabara hiyo inayofanyika JKCI bila malipo. Mtaalamu wa maabara wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mwajuma Chibwana akichukua sampuli ya damu kutoka kwa mkazi wa Dar es Salaam aliyefika katika kambi maalumu ya uchunguzi wa afya kupitia maabara inayotumia akili unde (AI) inayofanyika bila malipo katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Baadhi ya wananchi wakisubiri kupatiwa huduma ya kufanyiwa vipimo vya malaria na mafuta mwilini wakati wa kambi maalumu ya uchunguzi wa afya kupitia maabara inayotumia akili unde (AI) inayofanyika bila malipo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI). Na Agnes Sikaonga *********************************************************************************** Maabara ya kisa...