Posts

Kambi Maalum ya Upimaji na Matibabu ya Moyo Yawafikia watu 302 Arusha

Image
Mkurugenzi wa Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) ambayo kwa sasa inasimamiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tatizo Waane akipokea cheti cha shukrani kutoka kwa Daktari Bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watu wazima na Mshauri wa Upasuaji wa moyo kupitia tundu dogo kutoka  National Heart Institute (NHI) nchini Misri Prof. Ghada Kazamel baada ya kumalizika kwa kambi maalumu ya siku mbili ya uchunguzi na matibabu ya moyo kwa watoto na watu wazima iliyokuwa ikifanyika katika Hospitali ya ALMC  na wataalamu wa JKCI, ALMC, Heart to Heart Association for Sustainable Development na  Egyptian African Heart Association (EAHA). Daktari Bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Goup Eva Wakuganda akimpima kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (ECHO) mtoto wakati wa kambi maalumu ya siku mbili ya uchunguzi na matibabu ya moyo iliyofanywa na wataalamu wa JKCI, ALMC na   Heart to Heart Association f...

Shilingi milioni 30 zatoa tumaini kwa watoto wenye magonjwa ya Moyo

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akipokea hundi ya Shilingi milioni 30 kutoka kwa viongozi wanawake wanaoshiriki mafunzo ya Female Future Program msimu 11 yanayotolewa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) walipotembelea Taasisi hiyo jana na kukabidhi mchango huo. Mtendaji Mkuu wa Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Heart Team Africa Foundation (HTAF) Dkt. Naizihijwa Majani akizungumza na viongozi wanawake wanaoshiriki mafunzo ya Female Future Program msimu 11 yanayotolewa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) walipotembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) jana kwaajili ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa na JKCI. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akiwashukuru viongozi wanawake wanaoshiriki mafunzo ya Female Future Program msimu 11 yanayotolewa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE)  mara baada ya kuchangia kiasi cha shilingi milioni 30 kwaajili ya matibabu ya watot...

Ziara ya Kujifunza: Viongozi wa Congo wapata huduma za kibingwa za Moyo JKCI

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimpima Shinikizo la damu (BP) Balozi wa Tanzania katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Mhe. Said Juma Mshana alipofika katika Taasisi hiyo leo kwaajili ya kufanya uchunguzi wa afya. Mtaalamu wa Maabara wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Jesca Mlay akimtoa damu Gavana wa jimbo la Maniema Mhe. Mussa Kabwankubi Moise alipofika katika Taasisi hiyo tawi la Oysterbay leo pamoja na ujumbe wa viongozi kutoka jimbo hilo kwaajili ya kufanya uchunguzi wa afya.  Mtaalamu wa vipimo vya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Loyce Victor akimpima kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanyakazi (Echocardiograph – ECHO) mjumbe kutoka jimbo la Maniema wakati wajumbe hao walipotembelea JKCI tawi la Oysterbay leo kwaajili ya kufanya uchunguzi wa afya Gavana wa jimbo la Maniema Mhe. Mussa Kabwankubi Moise pamoja na wajumbe kutoka jimbo hilo wakisubiri kupata huduma alipofika katika Taasisi ya Moyo Ja...

JKCI na ABC Group kushirikiana kufikisha huduma za matibabu ya moyo kwa wananchi

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge pamoja na Mkurugenzi wa Kampuni ya ABC Group Mohammed Shareef wakisaini mkataba wa makubaliano ya ushirikiano wa kuwatibu wateja wa ABC Group Tanzania kwa punguzo la asilimia 20, uliofanyika katika ofisi za ABC jijini leo Dar es Salaam.   Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akiongea na waandishi wa habari wakati wa hafla fupi ya kusaini mkataba wa makubaliano ya ushirikiano kati ya JKCI na Kampuni ya ABC Group kuwatibu wateja wa ABC kwa punguzo la asilimia 20 iliyofanyika leo katika ofisi za ABC zilizopo jijini Dar es Salaam.   Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akipokea hundi kuashiria ushirikiano kati ya Taasisi hiyo na kampuni ya ABC Group mara baada ya hafla fupi ya kusaini mkataba wa ushirikiano kuwatibu wateja wa ABC kwa punguzo la asilimia 20 iliyofanyika leo ofisi za ABC zilizopo jijini Dar es...

JKCI kufungua tawi DRC Congo

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimpatia zawadi Gavana wa jimbo la Maniema la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Mhe. Mussa Kabwankubi Moise alipotembelea Taasisi hiyo leo kwaajili ya kuona huduma zinazotolewa pamoja na kuangalia namna ya kushirikiana na Taasisi hiyo kukuza huduma za moyo nchini Congo. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na balozi wa Tanzania katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Mhe. Said Juma Mshana na Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia Congo nchini Tanzania Mhe. Prof. Jean Pierre Massala walipotembela Taasisi hiyo leo kwaajili ya kuona huduma zinazotolewa pamoja na kuangalia namna ya kushirikiana na Taasisi hiyo kukuza huduma za moyo nchini Congo. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na Gavana wa jimbo la Maniema la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Mhe. Mussa Kabwankubi Moise alipotem...

Wafanyabiashara Kariakoo Kunufaika na Huduma za Afya Baada ya JKCI Kufungua Kliniki Mpya

Image
Mwenyekiti wa bodi ya wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Hassan Mahmoud Mshinda pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Dkt. Peter Kisenge wakikata utepe leo wakati wa ufunguzi wa kliniki mpya ya JKCI  iliyopo katika Soko Kuu la Kariakoo jijini Dar es Salaam.    Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Alex Msoka akiwaelezea viongozi huduma zitakazotolewa katika kliniki mpya ya JKCI iliyofunguliwa leo katika Soko Kuu la Kariakoo lililopo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na wadau waliofika katika ufunguzi wa kliniki mpya ya JKCI iliyopo katika Soko Kuu la Kariakoo jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti wa bodi ya wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Hassan Mahmoud Mshinda akizungumza na waandishi wa habari wakati wa ufunguzi wa Kliniki mpya ya JKCI leo katika Soko Kuu la Kariakoo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taa...

Siku ya Msikilizaji Habari Maalum Media yaleta uchunguzi wa Moyo bure Ngaramtoni

Image
Matroni wa Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Center (ALMC) inayosimamiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Sr.  Flora Kasembe akitoa elimu ya magonjwa ya moyo kwa wananchi waliohudhuria maadhimisho ya Siku ya Msikilizaji yaliyoandaliwa na Habari Maalum Media na kufanyika Ngaramtoni jijini Arusha.   Wakazi wa Arusha wakisubiri kupata huduma ya upimaji wa magonjwa ya moyo iliyokuwa inatolewa na wataalamu wa  Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Center (ALMC) inayosimamiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa  maadhimisho ya Siku ya Msikilizaji yaliyoandaliwa na Habari Maalum Media na kufanyika Ngaramtoni jijini Arusha. Matroni wa Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Center (ALMC) inayosimamiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Sr. Flora Kasembe akimpima shinikizo la damu mkazi wa Arusha wakati wa maadhimisho ya Siku ya Msikilizaji iliyoandaliwa na Habari Maalum Media na kufanyika Ngaramtoni jijini Arusha. Na JKCI ***********************...