Matumizi ya shisha na sigara kusababisha magonjwa ya moyo, matatizo ya mapafu na saratani
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza wakati wa hafla fupi ya kuzindua taarifa ya mwaka 2025 kuhusu Kampuni za Tumbaku zinavyoingilia Sera ya Afya nchini iliyofanywa na Chama cha Kudhibiti Tumbaku Tanzania (TTCF) katika ukumbi wa JKCI iliyopo jijini Dar es Salaam. Na JKCI ************************************************************************************************* Vijana na wananchi kwa ujumla wametakiwa kutunza afya zao na kujiepusha na matumizi ya tumbaku hususani sigara na shisha yanayoweza kupelekea magonjwa ya moyo, matatizo ya mapafu na saratani hivyo kusababisha vifo vya ghafla. Rai hiyo imetolewa na Mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge hivi karibuni wakati wa hafla fupi ya kuzindua taarifa ya mwaka 2025 kuhusu Kampuni za Tumbaku zinavyoingilia Sera ya Afya nchini iliyofanywa na Chama cha Kudhibiti Tumbaku Tanzania (TTCF) katika ukumbi wa JKCI iliyopo jijini Dar es...