Watumishi REA wahimizwa kufahamu “Namba Zao” kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza
Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group, Fatma Suedy akimpima shinikizo la damu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Mhandisi Hassan Saidy wakati wa kambi maalumu ya utoaji wa elimu na uchunguzi wa afya kwa wafanyakazi wa taasisi hiyo iliyofanyika hivi karibuni jijini Dodoma. Mtaalamu wa Maabara wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Kliniki ya Oysterbay Hamisi Msangi akimpima kiwango cha sukari kwenye damu Afisa Usafirishaji wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Samwel Sumwa wakati wa kambi maalumu ya utoaji wa elimu na uchunguzi wa afya kwa wafanyakazi wa REA iliyofanyika hivi karibuni jijini Dodoma. Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Monica Kaganga akitoa elimu ya “ Jua Namba Zako” kwa wafanyakazi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika ukumbi wa mikutano wa taasisi hiyo iliyofanyika hivi karibuni jijini Dodoma wakati wa kambi maalumu ya utoaji wa elimu na ...