Posts

Serikali yamuokoa Mama wa Kivule kwa matibabu ya moyo ya shilingi milioni 29 JKCI

Image
Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Zaina Mlingo akimpima shinikizo la damu Mama Anna Mwansasu mkazi wa Kisamvule jijini Dar es Salaam ambaye amefanyiwa upasuaji mdogo wa kupandikiziwa   kifaa cha CRT (Cardiac Resynchronization Therapy) ambacho kinausaidia moyo kupiga mapigo yake kwa mpangilio sahihi. Gharama ya matibabu hayo ni zaidi ya shilingi  milioni 29 ambapo serikali ya awamu ya sita ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imelipia. ***************************************************************************************************************************************************************************************************** Mkazi wa Kivule jijini Dar es Salaam Mama Anna Mwansasu , ameishukuru Serikali ya awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumsaidia kugharamia matibabu ya kubadilishiwa kifaa cha CRT (Cardiac Resynchronization Therapy) ambacho kinausaidia moyo kupiga mapigo yake kwa mpangilio sahihi...

Ushirikiano na Jamii waongeza nguvu ya matibabu ya Moyo JKCI

Image
Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi wa     Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Naizihijwa Majani akiwa katika picha ya pamoja na wadau kutoka Taasisi isiyokuwa ya kiserikali ya Moyo Mission ya nchini Ujerumani     pamoja na wafanyakazi wa JKCI wakati wa uzinduzi wa kampeni ya ushirikiano wa kutoa huduma za matibabu ya moyo kwa watoto uliofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Naizihijwa Majani akizungumza na wadau wa afya hivi  karibuni wakati wa uzinduzi wa kampeni ya ushirikiano wa utoaji huduma za matibabu ya moyo kwa watoto baina ya JKCI na Taasisi isiyokuwa ya kiserikali ya Moyo Mission ya nchini Ujerumani.  Msanii wa muziki wa kizazi kipya Bernard Paul maarufu  kama Ben Paul akizungumza kuhusu ushirikiano wa Taasisi isiyokuwa ya Kiserikali ya Moyo Mission ya nchini Ujerumani na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wa kutoa huduma za matibabu ya moyo kwa w...

Wanawake zaidi ya 200 wafanyiwa uchunguzi wa saratini ya shingo ya kizazi na matiti

Image
Meneja wa Rasilimali watu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Abdulrahman Muya akikabidhi zawadi kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group mgeni rasmi ambaye ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu kutoka Bakhresa Group of Company Mwanafumo Mohamed wakati wa hafla ya kuadhimisha siku ya wanawake duniani iliyofanywa na wanawake wa Hospitali hiyo jana jijini Dar es Salaam. Mgeni rasmi wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group ambaye ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu kutoka Bakhresa Group of Company Mwanafumo Mohamed akimpatia zawadi mmoja wa wagonjwa waliolazwa katika Hospitali hiyo wakati wa hafla fupi ya kuadhimisha siku ya wanawake duniani iliyofanywa na wanawake wa Hospitali hiyo jana jijini Dar es Salaam. Mgeni rasmi wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar...

Zaidi ya wananchi 100 washiriki uchunguzi wa Moyo na kuchangia damu JKCI

Image
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Naizihijwa Majani akiwa katika picha ya pamoja na wanawake wa taasisi hiyo wakati wa upimaji wa afya na uchangiaji wa damu uliofanywa na wanawake wa JKCI katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani leo katika viwanja vya JKCI iliyopo jijini Dar es Salaam.  Afisa Uhusiano na Mawasiliano wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Agnes Sikaonga akiwapatia vipeperushi wananchi waliojitokeza kufanyiwa uchunguzi wa afya pamoja na kuchangia damu wakati wanawake wa Taasisi hiyo wakiadhimisha siku ya wanawake duniani leo katika viwanja vya JKCI iliyopo jijini Dar es Salaam. Afisa Lishe wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Emmanuel Lingindo akitoa elimu ya lishe kuhusu umuhimu wa kuzingatia mlo uliokamilika kwa wananchi waliojitokeza kupima afya na kuchangia damu wakati wanawake wa Taasisi hiyo walipoadhimisha siku ya wanawake duniani leo katika viwanja vya JKCI iliyopo jijini Dar es Salaam. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya...

JKCI yahimiza familia kulinda watoto dhidi ya mazingira hatari

Image
  Sophia Yohana akiongoza maombi wakati Wanawake wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI Women) walipotembelea Makao ya Watoto Kurasini jijini Dar es Salaam na kutoa msaada wa mahitaji mbalimbali ikiwemo jiko la kuokea mikate, mchele na sukari vyenye thamani ya shilingi milioni 3.55 ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo kilele chake ni Machi 8, 2026.   Mwenyekiti wa Chama cha Wanawake wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI),  Theresia Marombe  akisaini kitabu cha wageni wakati yeye na wanachama wa chama hicho walipotembelea Makao ya Watoto Kurasini jijini Dar es Salaam jana na kutoa msaada wa mahitaji mbalimbali yenye thamani ya shilingi  milioni 3.55  ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya  Siku ya Wanawake Duniani . Afisa Ustawi wa Makao ya Watoto Kurasini, Andrew Haule   akiwakaribisha wanawake wa Chama cha Wanawake wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) walipotembelea makao hayo jana jijini Dar es Salaam na...

Rasimu ya kwanza ya mpango mkakati wa tatu wa JKCI yajadiliwa

Image
Baadhi ya wajumbe wa kamati ya maandalizi ya mpango mkakati wa tatu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifuatilia mada zilizokuwa zikiendelea wakati wa kikao cha kupitia rasimu ya kwanza ya mpango huo kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam. Baadhi ya wajumbe wa kamati ya maandalizi ya mpango mkakati wa tatu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifuatilia mada zilizokuwa zikiendelea wakati wa kikao cha kupitia rasimu ya kwanza ya mpango huo kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam. Mjumbe wa kamati ya maandalizi ya mpango mkakati wa tatu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Fiona Kavishe akichangia mada wakati wa kikao cha kupitia rasimu ya kwanza ya mpango huo kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam. Mshauri wa mpango mkakati kutoka kampuni ya Bankable Tanzania Limited Caroline Chema akiwasilisha rasimu ya kwanza ya mpango mkakati wa tatu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa wajumbe wa kamati ya mpango huo leo jijini Dar es Salaam. Picha na: JKCI *************...

Rushwa na Ukiukwaji wa maadili vyapigwa vita JKCI

Image
Afisa Maadili Mwandamizi kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Grace Matunda akitoa elimu ya maadili kwa viongozi na wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) hii leo katika ukumbi wa mikutano wa JKCI jijini Dar es Salaam. Elimu hiyo imelenga kuwajenga viongozi na wafanyakazi wa taasisi hiyo kuendelea kuwa na maadili mazuri katika maeneo yao ya kazi.   Afisa Maadili Mwandamizi kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda Maalum ya Dar es Salaam Hamadi Bakari  akitoa elimu ya maadili ya Utumishi wa Umma kwa viongozi na wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.   Baadhi ya Viongozi na Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifuatilia  mafunzo ya maadili kwa viongozi wa utumishi wa yaliyokuwa yanatolewa na  Afisa Maadili Mwandamizi ...