Posts

China kutumia shilingi bilioni 112 kujenga Jengo jipya la JKCI Mloganzila

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimpatia zawadi mhandisi kutoka Jamhuri ya Watu wa China Zhang Ziying wakati wa kikao na ujumbe wa wahandisi kutoka China kujadili mradi wa ujenzi wa jengo jipya la JKCI litakalojengwa katika eneo la mloganzila jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akielezea mafanikio ya Taasisi hiyo wakati wa kikao na ujumbe wa wahandisi kutoka Jamhuri ya Watu wa China kujadili mradi wa ujenzi wa jengo jipya la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) litakalojengwa katika eneo la mloganzila jijini Dar es Salaam. Mwakilishi kutoka Ubalozi wa China Nchini Tanzania Yang Zeyu akizungumza wakati wa kikao na Ujumbe wa wahandisi kutoka nchini China kujadili mradi wa ujenzi wa jengo jipya la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) litakalojengwa katika eneo la mloganzila jijini Dar es Salaam. Mkuu wa mradi wa ujenzi wa jengo jipya la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)...

Mhe. Dkt. Kikwete apokea taarifa ya utekelezaji wa fedha za Gala Dinner za matibabu ya moyo kwa watoto

Image
Rais Mstaafu wa awamu ya nne Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge pamoja na Mtendaji Mkuu wa Heart Team Africa Foundation (HTAF) Dkt. Naizihijwa Majani walipomtembelea ofisini kwake hivi karibuni kwa lengo la kumpa taarifa ya utekelezaji wa fedha zilizokusanywa kupitia Gala Dinner ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo. Rais Mstaafu wa awamu ya nne Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge mara baada ya kupokea taarifa ya fedha zilizokusanywa na Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Heart Team Africa Foundation (HTAF) kupitia Gala Dinner ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa JKCI. Mtendaji Mkuu wa Heart Team Africa Foundation (HTAF) Dkt. Naizihijwa Majani akitoa taarifa kwa Rais Mstaafu wa awamu ya nne Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete kuhusu utekelezaji wa fedha zilizoku...

Watumishi REA wahimizwa kufahamu “Namba Zao” kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Image
Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group, Fatma Suedy  akimpima shinikizo la damu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Mhandisi Hassan Saidy wakati wa kambi maalumu ya utoaji wa elimu na uchunguzi wa afya kwa wafanyakazi wa taasisi hiyo iliyofanyika hivi karibuni jijini Dodoma.   Mtaalamu wa Maabara wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Kliniki ya Oysterbay Hamisi Msangi  akimpima kiwango cha sukari kwenye damu Afisa Usafirishaji wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Samwel Sumwa  wakati wa kambi maalumu ya utoaji wa elimu na uchunguzi wa afya kwa wafanyakazi wa REA  iliyofanyika hivi karibuni jijini Dodoma.   Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Monica Kaganga akitoa elimu ya “ Jua Namba Zako” kwa wafanyakazi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika ukumbi wa mikutano wa taasisi hiyo iliyofanyika hivi karibuni jijini Dodoma wakati wa kambi maalumu ya utoaji wa elimu na ...

Watumishi wa Wizara ya Fedha wanufaika na kambi maalumu ya uchunguzi wa Moyo

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akitoa elimu ya magonjwa ya moyo kwa mfanyakazi wa Wizara ya Fedha wakati wa kambi maalumu ya upimaji wa afya kwa watumishi hao iliyomalizika jana jijini Dodoma. Baadhi ya watumishi wa Wizara ya Fedha wakisubiri kupata huduma za uchunguzi wa afya zinazotolewa na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa kambi maalumu ya upimaji wa afya iliyomalizika jana jijini Dodoma. Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mohamed Aloyce  akitoa elimu ya “ Jua Namba Zako ” kwa mtumishi wa Wizara ya Fedha wakati wa kambi maalumu ya upimaji wa afya kwa watumishi hao iliyomalizika jana jijini Dodoma. Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Moris Budotela  akitoa elimu ya “ Jua Namba Zako ” kwa Afisa Sheria wa Idara ya Huduma za Sheria wa Wizara ya Fedha Yohana Msengi  wakati wa kambi maalumu ya upimaji wa afya iliyomalizika jana jiji...

Shinikizo la Damu laua kimyakimya, JKCI yatoa wito wa hatua za haraka

Image
  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimpima shinikizo la damu mwandishi wa habari wakati wa zoezi la upimaji afya ikiwa ni kuelekea katika  Maadhimisho ya Siku ya Shinikizo la Juu la Damu Duniani yanayofanyika kila mwaka tarehe 17 Mei. Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Kliniki ya Oysterbay Noel Mushi akimpima shinikizo la damu mwandishi wa Azam TV Esterbella Malisa wakati wa zoezi la upimaji afya ikiwa ni kuelekea katika  Maadhimisho ya Siku ya Shinikizo la Juu la Damu Duniani yanayofanyika kila mwaka tarehe 17 Mei. *************************************************************************************************************************************************************************************************** Mtindo usiofaa wa maisha umetajwa kuwa miongoni mwa sababu kuu zinazochangia kuongezeka kwa tatizo la shinikizo la juu la damu ugonjwa unaoendelea kuwa tishio kubwa la afya duniani na kusaba...

JKCI yawahimiza Wafanyakazi kupima Afya mara kwa mara kuepuka magonjwa yasiyoambukiza

Image
  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Dkt. Peter Kisenge akimkabidhi zawadi ya mashine ya kupimia shinikizo la damu, joto la mwili na kiwango cha sukari Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Fedha, Lucius Mwenda mara baada ya kumaliza kutoa elimu ya kujikinga na magonjwa ya moyo wakati wa zoezi la upimaji wa afya kwa watumishi wa Wizara hiyo jijini Dodoma. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Dkt. Peter Kisenge akitoa elimu kuhusu magonjwa ya moyo kwa wafanyakazi wa Wizara ya Fedha wakati wa zoezi la upimaji wa afya kwa watumishi wa Wizara hiyo jijini Dodoma. Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Fedha Lucius Mwenda akizungumza na wafanyakazi wa wizara hiyo mara baada ya kupata elimu ya kujikinga na magonjwa ya moyo wakati wa zoezi la upimaji wa afya kwa watumishi wa Wizara ya Fedha jijini Dodoma. Mtaalamu wa Maabara wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)Glory Mtui akimchukua sampuli ya damu Afisa ...

Mbunge Kigoma mjini Cleyton Chipando ataka Kitengo cha elimuishe mtandaoni

Image
Mbunge wa Kigoma Mjini, Clayton Chipando, (Baba Levo) akichangia Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2026/27 leo jijini Dodoma ************************************************************************************************************************** Mbunge wa Kigoma Mjini, Clayton Chipando, (Baba Levo) ameshauri Wizara ya Afya kuwa na Kitengo maalum kwa ajili ya kutoa elimu Afya ya Lishe Mitandaoni dhidi ya baadhi ya watu wanaotoa Elimu hiyo bila kuwa na mwongozo sahihi wa Wizara yenye dhamana ya Afya. Mhe. Chipando ameyasema hayo Mei 12, 2026 jijini Dodoma wakati akichangia Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2026/27  "Mhe. Mwenyekiti mimi nimekula Ugali kwa miaka 35, lakini Leo kila ukiingia mtandaoni utakutana na matangazo mbalimbali yanayotumika kuelimisha watu juu ya utaratibu wa matumizi ya chakula" amesema Mhe. Chipando Mhe. Chipando amesema katìka siku za hivi karibuni kumekuwepo na wimbi la watoa huduma, ambao kwa namna moja au nyi...