Posts

JKCI na Poland: Fursa mpya za Utafiti, Ujuzi na "Grants"

Image
Balozi wa Poland nchini Tanzania Mhe. Sergiusz Wolski akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge na wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Jagiellonian kilichopo nchini Poland walipotembelea ubalozi huo leo kwaajili ya kuona namba watakavyofanya  ushirikiano na JKCI katika masuala ya utafiti, ujuzi na “ grants”. Balozi wa Poland nchini Tanzania Mhe. Sergiusz Wolski akizungumza na ujumbe kutoka chuo Kikuu cha Jagiellonian kilichopo nchini Poland walipotembelea ubalozi huo leo kwaajili ya kuona namna ya kufanya ushirikiano na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) katika masuala ya utafiti, ujuzi na “ grants”. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akielezea huduma zinazotolewa na Taasisi hiyo wakati wa kikao na Balozi wa Poland nchini Tanzania Mhe. Sergiusz Wolski kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam cha kujadili namna Taasisi hiyo itakavyoshirikiana na Chuo Kikuu cha Jagiellonia...

ALMC na MOI kuendesha kambi maalumu ya matibabu ya magonjwa ya mifupa Arusha

Image
 Mkurugenzi wa Magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tatizo Waane akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kambi maalumu ya siku 5 ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa mbalimbali ya mifupa na mishipa ya fahamu itakayofanywa na wataalamu wa  Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) ambayp inayosimamiwa na JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa Taasisi ya Tiba na Mifupa Muhimbili (MOI). Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) Antony Assey akielezea huduma ambazo Taasisi hiyo itazitoa wakati wa kambi maalumu ya siku 5 ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa mbalimbali ya mifupa na mishipa ya fahamu itakayofanyika tarehe 23-27/02/2026 katika Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) inayosimamiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI). Baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifuatilia mkutano na waandishi wa habari kuhusu kambi maalumu ya siku 5 ya uchunguzi na matibabu ya magonjw...

Watu zaidi ya 300 wafanyiwa uchunguzi wa afya na JKCI Tamasha la IST Festival

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila akizungumza na wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) alipotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa Tamasha la IST Festival lililofanyika jana katika viwanja vya Coco Beach vilivyopo jijini Dar es Salaam.  Daktari wa kinywa na meno wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Aitham Mohamed akimfanyia uchunguzi wa kinywa mwananchi aliyetembelea banda la Hospitali hiyo kwaajili ya kupata huduma wakati wa Tamasha la IST Festival lililofanyika jana katika viwanja vya Coco Beach vilivyopo jijini Dar es Salaam. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Fakihi Mguwalo akimpima shinikizo la damu (BP) Mkurugenzi wa Halmashauri jiji la Dar es Salaam Elihuruma Mabelya aliyetembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa Tamasha la IST Festival lililofanyika jana katika viwanja vya Coco Beach vilivyopo jijini Dar es Salaam. Afisa huduma kwa wateja wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Stephano Zavara ...

Wataalamu wa afya kutoka Madagascar wavutiwa na ubora wa huduma za moyo za JKCI

Image
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Robert Mallya akimkabidhi zawadi Mfamasia Mkuu wa Bohari ya Dawa kutoka nchini Madagascar (SALAMA) Soafara Andrianone wakati wa ziara ya ujumbe wa wataalamu wa afya kutoka nchini humo ulipotembelea JKCI hivi karibuni kuona huduma zinazotolewa na kuangalia namna ya kushirikiana. Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Robert Mallya akimkabidhi zawadi Mkurugenzi wa Idara ya Famasia kutoka Wizara ya Afya nchini Madagascar Dkt. Maximine Ravaoarimanana wakati wa ziara ya ujumbe wa wataalamu wa afya kutoka nchini humo ulipotembelea JKCI hivi karibuni kuona huduma zinazotolewa na kuangalia namna ya kushirikiana. Viongozi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na ujumbe wa wataalamu wa afya kutoka nchini Madagascar (SALAMA) wakijadiliana wakati ya ziara ya ujumbe huo ulipotembelea JKCI hivi karibuni kwa ajili ya kuona huduma zinazotolewa pamoja na kuangalia namna ya kushirikiana. Mkurugenzi wa Taasi...

Serikali yagharamia milioni 758 matibabu ya Wagonjwa wa Moyo

Image
Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Stella Mongela akimpima mtoto kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (Echocardiography - ECHO) ******************************************************************************************************************* Serikali imegharamia jumla ya shilingi milioni 758,178,091 kwa ajili ya matibabu ya wagonjwa wa moyo wasiokuwa na uwezo wa kulipia huduma hizo pamoja na kusamehe gharama za miili ya marehemu waliokuwa wakipatiwa matibabu katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI). Akizungumza na mwandishi wa habari hii jijini Dar es Salaam kuhusu siku 100 za utekelezaji wa ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kugharamia matibabu ya kibingwa kwa wagonjwa wa moyo wasiokuwa na uwezo, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Dkt. Peter Kisenge, alisema serikali ya awamu ya sita imeendelea kuweka mkazo katika kuwasaidia wananchi wenye uhitaji ...

Kamati ya upandikizaji moyo yakabidhi rasimu ya muongozo wa upandikizaji moyo

Image
 

Viatu vyenye kisigino kirefu hatari kwa afya ya magoti.

Image
Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Beatrice Nangawe akitoa elimu ya afya bora kwa wafanyakazi wa Bohari ya Dawa (MSD) wakati wa kambi maalumu ya siku mbili ya uchunguzi wa afya iliyofanyika hivi karibuni katika ofisi za MSD Kanda ya Mabibo jijini Dar es Salaam. Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mohamed Aloyce akimpa ushauri mmoja wa wafanyakazi wa Bohariy a Dawa (MSD) wakati  wa kambi maalumu ya uchunguzi wa afya iliyofanyika hivi karibuni katika ofisi za MSD Kanda ya Mabibo jijini Dar es Salaam. Daktari bingwa wa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Theophilly Mushi  akitoa elimu kuhusu magonjwa ya moyo kwa wafanyakazi wa Bohari ya Dawa (MSD) wakati wa kambi maalumu ya uchunguzi wa afya iliyokuwa ikifanywa na wataalamu wa JKCI hivi karibuni katika ofisi za MSD Kanda ya Mabibo jijini Dar es Salaam. Mtaalamu wa mazoezi tiba wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Da...