JKCI na Watalaamu wa Ujerumani waokoa Maisha ya watoto 15
Wataalamu wa upasuaji wa moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao kutoka taasisi isiyo ya kiserikali ya Moyo Mission ya nchini Ujerumani wakimfanyia mtoto upasuaji wa kuziba tundu la moyo katika kambi maalumu ya siku tano ya upasuaji wa moyo kwa watoto iliyofanyika JKCI ambapo watoto 15 walifanyiwa upasuaji. Daktari bingwa wa usingizi na wagonjwa walioko katika uangalizi maalumu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Alex Loth na daktari bingwa wa moyo kwa watoto kutoka taasisi isiyo ya kiserikali ya Moyo Mission ya nchini Ujerumani Harms Sebastian wakimfanyia kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi mtoto ambaye moyo wake una tundu wakati wa kambi maalumu ya siku tano ya upasuaji wa moyo kwa watoto iliyofanyika JKCI. Wataalamu wa kuendesha mashine ya kuusaidia moyo na mapafu kufanya kazi (Heart Lung Machine) wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na mwenzao kutoka taasisi isiyo ya kiserikali ya Moyo Mission ya nchini Ujerumani wakiendesha mas...