Posts

Wakuu wa Taasisi za afya zinazotoa huduma bingwa bobezi wakutana kuboresha ushirikiano na masuala ya tafiti

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akichangia mada wakati wa kikao cha wakuu wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI), Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH),   Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI) na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS)    kuimarisha ushirikiano na kuboresha utoaji wa huduma kilichofanyika jana katika Ukumbi wa MUHAS jijini Dar es Salaam. Wakurugenzi Watendaji kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge, Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) Dkt. Delilah Kimambo, Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) Balozi Ulisubisya Mpoki, Mwakilishi wa Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI)  Dkt. Nazima Dharsee, na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Prof. Appolinary Kamuhabwa wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa kikao cha ujirani mwema kuimarisha ushirikiano na kuboresha utoaji wa huduma ki...

JKCI yashiriki mkutano wa kimataifa kujadili mikakati ya kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza Afrika PEN-PLUS (ICPPA 2026)

Image
  Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hania Bwahama akimuelezea Mshiriki wa mkutano mkuu wa tatu wa Kimataifa wa kikanda PEN-PLUS (ICPPA 2026) kutoka nchini Nigeria Mya Nyon vifaa vinavyotumika wakati wa upasuaji wa moyo alipotembelea banda la JKCI lililopo katika mkutano huo unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) kilichopo jijini Dar es Salaam. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hania Bwahama akimuelezea mtaalamu wa afya kutoka nchini Afrika Kusini Roylah Rykiel kuhusu huduma za upasuaji wa moyo zinazotolewa na Taasisi hiyo wakati wa mkutano mkuu wa tatu wa Kimataifa wa kikanda PEN-PLUS (ICPPA 2026) unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) kilichopo jijini Dar es Salaam. Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Alex Msoka akimuelezea Mkurugenzi Msaidizi wa Elimu kwa Umma Dkt Rahma Hingora kuhusu kampeni ya Jua Namba Zako inayofanywa ...

JKCI kuanzisha kampuni tanzu kuimarisha tiba utalii nchini

Image
Mwenyekiti Msaidizi wa Kamati ya Maandalizi ya mpango mkakati wa watu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Iddi Lemah akizungumza na wafanyakazi wa Taasisi hiyo wakati wa kikao cha kuwasilisha mpango mkakati wa tatu wa JKCI kwa wafanyakazi kilichofanyika jana katika ukumbi wa JKCI iliopo jijini Dar es Salaam. Mshauri wa maandalizi ya mpango mkakati wa watu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Ivan Tarimo akielezea vitu vilivyoanishwa katika mpango mkakati huo wakati wa kikao cha kuwasilisha mpango mkakati wa tatu wa JKCI kwa wafanyakazi kilichofanyika jana katika ukumbi wa Taasisi hiyo uliopo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akielezea namna ambavyo mpango mkakati wa tatu wa JKCI utakavyoboresha huduma wakati wa kikao cha kuwasilisha mpango mkakati huo kwa wafanyakazi kilichofanyika jana katika ukumbi wa Taasisi hiyo iliopo jijini Dar es Salaam. Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwe...

Wataalamu kutoka nchini Namibia watembelea JKCI kuona huduma zinazotolewa

Image
Mkurugenzi wa Idara ya Upasuaji wa Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Angela Muhozya akimpatia zawadi Kaimu Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Uwekezaji na Maendeleo ya nchini Namibia (NIPDB) Jessica Hauuanga wakati wataalamu kutoka nchini Namibia walipofanya ziara katika Taasisi hiyo kwaajili ya kujifunza na kuona namna watashirikiana katika kutoa huduma za matibabu ya moyo kwa wananchi wa Namibia. Fundi Sanifu wa Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Kulindwa Kasubi akielezea huduma zinazotolewa katika chumba cha upasuaji mdogo wa moyo kwa kutumia mtambo wa Cathlab kwa wajumbe kutoka nchini Namibia walipotembelea Taasisi hiyo kwaajili ya kujifunza na kuona huduma zinazotolewa ili wagonjwa kutoka nchini Namibia waanze kupata huduma katika Taasisi hiyo.  Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Alex Joseph akizungumza na ujumbe kutoka nchini Namibia walipotembelea Taasisi hiyo kwaajili ya kujifunza na kuona huduma ...

Watu 546 wapimwa Namba Zao katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Dodoma

Image
Baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyokuwa yakifanyika katika Viwanja vya Chinangali Park na kumalizika leo jijini Dodoma. Jumla ya watu 546 wamepimwa Namba Zao.  Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Bakar Mohamed akimpima shinikizo la damu mwananchi aliyefika katika banda la Taasisi hiyo kwaajili ya kujua Namba Zake wakati wa maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyokuwa yakifanyika katika Viwanja vya Chinangali Park na kumalizika leo jijini Dodoma. Jumla ya watu 546 wamepimwa Namba Zao.  Wananchi wakiendelea kupata elimu kuhusu Namba Zao katika banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyokuwa yakifanyika katika Viwanja vya Chinangali Park na kumalizika leo jijini Dodoma. Jumla ya watu 546 wamepimwa Namba Zao. Na JKCI *******************************************************************************...

UFAFANUZI KUHUSU TAARIFA ZA MGONJWA ZINAZOSAMBAA MTANDAONI

Image
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) inapenda kutoa ufafanuzi kuhusu taarifa za mgonjwa zinazosambaa mtandaoni kuhusu matibabu aliyokuwa akipatiwa katika Taasisi yetu.  Mgonjwa huyo alipokelewa JKCI tarehe 25 Mei 2026 akiwa na matatizo makubwa ya moyo yaliyosababisha moyo kushindwa kufanya kazi kama inavyotakiwa. Mara baada ya kulazwa, alipatiwa matibabu ya kina kwa lengo la kuimarisha hali yake ili aweze kuendelea na hatua nyingine za matibabu ikiwemo upasuaji wa moyo. Katika kipindi cha matibabu jopo la wataalamu wakiwemo madaktari bingwa wa upasuaji wa moyo walikutana na mgonjwa pamoja na ndugu zake kuwaeleza kwa kina hali ya mgonjwa na hatari zilizokuwepo.  Wataalamu walieleza kuwa kufanya upasuaji katika kipindi hicho kungeweza kuhatarisha zaidi maisha yake kutokana na hali yake kuwa dhaifu hivyo ilikubaliwa aendelee na matibabu ya kuimarisha afya yake. Licha ya juhudi kubwa zilizofanywa na wataalamu wetu na matibabu yote aliyokuwa akipatiwa hali ya mgonjwa...
Image
TAKUKURU yachangia milioni 20.89 matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo.   Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akipokea hundi ya shilingi milioni 20.89 kutoka kwa Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Ilala Faustine Maijo kwaajili ya kusaidia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.   Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza wakati wa hafla fupi ya kupokea hundi ya shilingi milioni 20.89 kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwajili ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Ilala Faustine Maijo akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi hundi ya shilingi milioni 20.89 kwaajili ya kuwasaidia watoto wenye magonjwa ya moyo wanao...