Mkutano wa CardioTan 2026 wahitimishwa, wataalamu wapata ujuzi uchunguzi vipimo vya moyo
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Saad Mtambule akimpatia tuzo mshindi wa kesi bora iliyowasilishwa wakati wa mkutano wa nne wa Kimataifa wa magonjwa ya moyo – CardioTan Imaging 2026 Dkt. Abdi Dibaba kutoka Hospitali ya Saifee wakati wa hafla fupi ya kufunga mkutano huo iliyofanyika jana katika ukumbi wa Blue Sapphire jijini Dar es Salaam. Jumla ya washiriki zaidi ya 600 kutoka nchi zaidi ya 16 wameshiriki mkutano huo. Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Saad Mtambule akizungumza na wataalamu wa afya walioshiriki mkutano wa nne wa Kimataifa wa Magonjwa ya Moyo – CardioTan Imaging 2026 wakati wa hafla fupi ya kufanga mkutano huo iliyofanyika jana katika ukumbi wa Blue Sapphire jijini Dar es Salaam. Jumla ya washiriki zaidi ya 600 kutoka nchi zaidi ya 16 wameshiriki mkutano huo Mkurugenzi wa Idara ya Upasuaji wa Moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Angela Muhozya akizungumza na washiriki wa mkutano wa nne wa kimataifa wa magonjwa ya moyo – CardioTan Imaging 2026 kwa niaba y...