Jamii yahimizwa kutambua vihatarishi vya magonjwa ya moyo mapema
Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Rafael Kwileka akimsomea majibu mwananchi aliyefika katika kambi maalumu ya uchunguzi wa afya ya siku tatu inayofanywa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Jumuiya ya Wafanyabiashara Kariakoo katika kliniki ya JKCI iliyopo Kariakoo jijini Dar es Salaam. Mhudumu wa Afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Halima Shaban akimpima uwiano wa urefu na uzito mwananchi aliyejitokeza kufanya uchunguzi wa afya wakati wa kambi maalumu ya siku tatu ya uchunguzi wa afya inayofanywa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Jumuiya ya Wafanyabiashara Kariakoo katika kliniki ya JKCI iliyopo Kariakoo jijini Dar es Salaam. Mtunza kumbukumbu za afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Emiliana Roshy akimsajiri mwananchi aliyejitokeza kufanya uchunguzi wa afya wakati wa kambi maalumu ya siku tatu ya uchunguzi wa afya inayofanywa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Jumu...