Wagonjwa nane wenye mishipa ya damu iliyoziba kufanyiwa upasuaji wa moyo
Wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakishirikiana na mwenzao kutoka Hospitali ya Jaslok iliyopo Mumbai nchini India Upendra Bhalerao kumfanyia upasuaji wa kupandikiza mshipa wa damu wa moyo bila kusimamisha moyo mgonjwa mwenye matatizo ya mishipa ya damu kuziba wakati wa kambi maalumu ya siku nane inayofanyika katika Taasisi hiyo jijini Dar es Salaam. Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo, mishipa ya damu na kifua kutoka Hospitali ya Jaslok iliyopo Mumbai nchini India Upendra Bhalerao akitoa mafunzo kwa wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) namna ya kutoa huduma kwa wagonjwa ambao mshipa yao ya damu imeziba wakati wa kambi maalumu ya siku nane inayofanyika katika Taasisi hiyo jijini Dar es Salaam. Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo, mishipa ya damu na kifua kutoka Hospitali ya Jaslok iliyopo Mumbai nchini India Upendra Bhalerao akiangalia taarifa za mgonjwa aliyelazwa katika wodi ya uangalizi maalumu (ICU) mara baada ya kufanyiwa upasuaji wa kupandikiza ms...