Posts

UFAFANUZI KUHUSU TAARIFA ZA MGONJWA ZINAZOSAMBAA MTANDAONI

Image
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) inapenda kutoa ufafanuzi kuhusu taarifa za mgonjwa zinazosambaa mtandaoni kuhusu matibabu aliyokuwa akipatiwa katika Taasisi yetu.  Mgonjwa huyo alipokelewa JKCI tarehe 25 Mei 2026 akiwa na matatizo makubwa ya moyo yaliyosababisha moyo kushindwa kufanya kazi kama inavyotakiwa. Mara baada ya kulazwa, alipatiwa matibabu ya kina kwa lengo la kuimarisha hali yake ili aweze kuendelea na hatua nyingine za matibabu ikiwemo upasuaji wa moyo. Katika kipindi cha matibabu jopo la wataalamu wakiwemo madaktari bingwa wa upasuaji wa moyo walikutana na mgonjwa pamoja na ndugu zake kuwaeleza kwa kina hali ya mgonjwa na hatari zilizokuwepo.  Wataalamu walieleza kuwa kufanya upasuaji katika kipindi hicho kungeweza kuhatarisha zaidi maisha yake kutokana na hali yake kuwa dhaifu hivyo ilikubaliwa aendelee na matibabu ya kuimarisha afya yake. Licha ya juhudi kubwa zilizofanywa na wataalamu wetu na matibabu yote aliyokuwa akipatiwa hali ya mgonjwa...
Image
TAKUKURU yachangia milioni 20.89 matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo.   Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akipokea hundi ya shilingi milioni 20.89 kutoka kwa Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Ilala Faustine Maijo kwaajili ya kusaidia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.   Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza wakati wa hafla fupi ya kupokea hundi ya shilingi milioni 20.89 kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwajili ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Ilala Faustine Maijo akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi hundi ya shilingi milioni 20.89 kwaajili ya kuwasaidia watoto wenye magonjwa ya moyo wanao...

Mkazi wa Temeke apongeza huduma za upasuaji wa moyo alizofanyiwa JKCI

Image
Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Agness Samuel akiangalia mapigo ya moyo ya mgonjwa Jonathan Mwanayongo aliyefanyiwa upasuaji wa kuzibua mishipa ya damu ya moyo bila kusimamisha moyo na wataalamu wa JKCI wakishirikiana na wenzao kutoka Hospitali ya Jaslok ya nchini India.  Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Agnes Samuel akimuhudumia mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji wa kuzibua mishipa ya damu ya moyo bila kusimamisha moyo Jonathan Mwanayongo. Mgonjwa huyo amefanyiwa upasuaji huo na wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao kutoka Hospitali ya Jaslok ya nchini India. *************************************************************************************************** Mkazi wa Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam Jonathan Mwanayongo ameipongeza Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kufanikisha upasuaji mkubwa wa moyo uliokuwa ufanyike nchini India. Akizungumza na Mwandishi wa habari hii Jonathan alisema  amegundulika kuwa na matatizo la ...

JKCI yahamasisha wananchi Dodoma Kujua Namba Zao na kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza

Image
Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Ghati Chacha akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika Viwanja vya Chinangali Park vilivyopo jijini Dodoma. Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo CPA. Ashraph Abdulkarim akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika Viwanja vya Chinangali Park vilivyopo jijini Dodoma. Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo CPA. Ashraph Abdulkarim akizijua namba zake kwa kupima uwiano wa urefu kwa uzito alipotembelea banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika Viwanja vya Chinangali Park vilivyopo jijini Dodoma. Afisa Utafiti wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Makrina Komba akimpima mzunguko wa kiuno mwananchi aliyetembelea banda la ...

JKCI yasaini makubaliano na China ujenzi wa hospitali mpya ya moyo

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge na Kiongozi wa kamati ya ukaguzi wa mradi wa ujenzi kutoka Jamhuri ya Watu wa China Yang Ling wakionesha hati ya makubaliano ya ujenzi wa hospitali mpya moyo mara baada ya kusaini hati hiyo jana katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge na Kiongozi wa kamati ya ukaguzi wa mradi wa ujenzi kutoka Jamhuri ya Watu wa China Yang Ling wakisaini hati ya makubaliano ya ujenzi wa hospitali mpya moyo jana katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na wafanyakazi wa JKCI pamoja na wataalamu wa mradi wa ujenzi kutoka Jamhuri ya Watu wa China wakati wa hafla fupi ya kusaini hati ya makubaliano ya ujenzi wa hospitali mpya moyo jana katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es...

JKCI yaweka kambi ya matibabu Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Dodoma

Image
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejmenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Juma Mkomi akizungumza na Maafisa kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) alipotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyoanza leo jijini Dodoma. Afisa Utafiti wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Makrina Komba akimpima uwiano wa urefu kwa uzito Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejmenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Juma Mkomi alipotembelea banda la Taasisi hiyo lililopo katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma. Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Daud Gwilenza akimsikiliza mwananchi aliyetembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika Viwanja vya Chinangali jijini Dodoma. Na JKCI ******************************************************************************************************* Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) yafikisha Kampeni y...

Maabara inayotumia akili unde kupunguza muda wa kusubiri majibu ya vipimo.

Image
  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimweleze mwandishi wa habari wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Ibrahim Chawe kuhusu maabara ya kisasa inayotumia akili unde (AI) wakati wa kambi maalumu ya uchunguzi wa afya kupitia maabara hiyo inayofanyika JKCI bila malipo. Mtaalamu wa maabara wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mwajuma Chibwana akichukua sampuli ya damu kutoka kwa mkazi wa Dar es Salaam aliyefika katika kambi maalumu ya uchunguzi wa afya kupitia maabara inayotumia akili unde (AI) inayofanyika bila malipo katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Baadhi ya wananchi wakisubiri kupatiwa huduma ya kufanyiwa vipimo vya malaria na mafuta mwilini wakati wa kambi maalumu ya uchunguzi wa afya kupitia maabara inayotumia akili unde (AI) inayofanyika bila malipo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI). Na Agnes Sikaonga *********************************************************************************** Maabara ya kisa...