Mbunge Kigoma mjini Cleyton Chipando ataka Kitengo cha elimuishe mtandaoni
Mbunge wa Kigoma Mjini, Clayton Chipando, (Baba Levo) akichangia Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2026/27 leo jijini Dodoma ************************************************************************************************************************** Mbunge wa Kigoma Mjini, Clayton Chipando, (Baba Levo) ameshauri Wizara ya Afya kuwa na Kitengo maalum kwa ajili ya kutoa elimu Afya ya Lishe Mitandaoni dhidi ya baadhi ya watu wanaotoa Elimu hiyo bila kuwa na mwongozo sahihi wa Wizara yenye dhamana ya Afya. Mhe. Chipando ameyasema hayo Mei 12, 2026 jijini Dodoma wakati akichangia Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2026/27 "Mhe. Mwenyekiti mimi nimekula Ugali kwa miaka 35, lakini Leo kila ukiingia mtandaoni utakutana na matangazo mbalimbali yanayotumika kuelimisha watu juu ya utaratibu wa matumizi ya chakula" amesema Mhe. Chipando Mhe. Chipando amesema katìka siku za hivi karibuni kumekuwepo na wimbi la watoa huduma, ambao kwa namna moja au nyi...