JKCI yawagusa wananchi Njombe kupitia kampeni ya “Jua Namba Zako”
Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Samweli Mbilinyi akimpa vipeperushi vya elimu ya magonjwa ya moyo Dorah Kachele ambaye ni Mkurugenzi wa vipindi na maudhui wa Kings FM ya mjini Njombe alipofika katika Hoteli ya Agreement kwaajili ya kupata huduma za uchunguzi na matibabu ya magonjwa mbalimbali zinayotolewa kwenye Kikao Kazi cha 21 cha Maafisa Habari, Mawasiliano, Itifaki na Uhusiano Serikalini kilichoandaliwa na Idara ya Habari- Maelezo. Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Modesta Nyagawa akimpima shinikizo la damu mkazi wa Njombe aliyefika katika Hoteli ya Agreement iliyopo mjini Njombe kwaajili ya kupata huduma ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa mbalimbali zinazotolewa kwenye Kikao Kazi cha 21 cha Maafisa Habari, Mawasiliano, Itifaki na Uhusiano Serikalini kilichoandaliwa na Idara ya Habari- Maelezo. Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Modesta Nyagawa akimpima kiwango cha sukari kwenye damu mkazi wa Njombe aliyefika katika Hotel...