Mkutano wa CardioTan Imaging 2026, WHO yaeleza maendeleo ya JKCI
Meneja wa Program Shirika la Afya Duniani (WHO) nchini Tanzania Dkt. Sisay Tegegne akizungumza na wataalamu wa afya alipokuwa akimwakilisha Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika, Shirika la Afya Duniani (WHO) Prof. Mohame Janabi wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa nne wa Kimataifa wa Magonjwa ya Moyo – CardioTan Imaging 2026 unaofanyika katika ukumbi wa Blue Sapphire jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akielezea mafanikio ya taasisi hiyo wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa nne wa Kimataifa wa Magonjwa ya Moyo – CardioTan Imaging 2026 unaofanyika katika ukumbi wa Blue Sapphire jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na Katibu Mkuu Msaidizi wa Ligi ya Arab kutoka nchini Misri Balozi Mohanad Legouzi wakisaini mkataba wa mashirikiano katika kujali afya za wanamichezo, kubadilishana ujuzi na kushiriki katika huduma za jamii kupitia shirika la Heart to Heart Association for sustainable develop...