Posts

Wizara ya Afya, JKCI na Children’s HeartLink waweka mikakati ya kuimarisha huduma za moyo kwa watoto nchini

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akiwa katika picha ya pamoja na wadau wa sekta ya afya na viongozi kutoka Wizara ya Afya mara baada ya mkutano na wadau hao kuweka mikakati ya kitaifa kuimarisha huduma za matibabu ya moyo kwa watoto uliofanyika jana katika ukumbi wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akielezea namna Taasisi hiyo inavyotoa huduma kwa watoto wenye magonjwa ya moyo wakati wa mkutano na wadau wa afya kuweka mikakati ya kitaifa kuimarisha huduma za matibabu ya moyo kwa watoto uliofanyika jana katika ukumbi wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.   Mkurugenzi wa huduma za tiba Wizara ya Afya Dkt. Hamad Nyembea akizungumza wakati wa mkutano na wadau wa afya kuweka mikakati ya kitaifa kuimarisha huduma za matibabu ya moyo kwa watoto uliofanyika jana katika ukumbi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo jijini Dar es Salaam. M...

Benki ya KCB yachangia shilingi milioni 20 matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akipokea hundi ya shilingi milioni 20 kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Vihatarishi na Uzingatiaji benki ya Kenya Commercial (KCB) tawi la Tanzania Angelina Semioni jana wakati wa hafla fupi ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo iliyofanyika katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akielezea namna wodi ya watoto wenye magonjwa ya moyo inavyotoa huduma wakati wa hafla fupi ya kukabidhi hundi ya shilingi milioni 20 iliyotolewa na benki ya Kenya Commercial (KCB) kwaajili ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza wakati wa hafla fupi ya kupokea hundi ya shilingi milioni 20 kutoka benki ya Kenya Commercial (KCB) tawi la Tanzania kwajili ya kuchangia matibabu ...

JKCI yang'ara mkutano wa kimataifa wa PEN-PLUS (ICPPA 2026), yaonesha teknolojia inayotumia katika matibabu ya moyo.

Image
Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hania Bwahama akimuelezea mshiriki wa mkutano wa tatu wa Kimataifa wa Kikanda PEN-PLUS (ICPPA 2026) kutoka nchini Zambia James Titus huduma zinazotolewa na taasisi hiyo alipotembelea banda la JKCI wakati wa mkutano huo uliofanyika katika kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) na kumalizika jana jijini Dar es salaam Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Karen Ngobei akiwaeleza washiriki wa mkutano wa tatu wa Kimataifa wa Kikanda PEN-PLUS (ICPPA 2026) kuhusu huduma zinazotolewa na taasisi hiyo walipotembelea banda la JKCI wakati wa mkutano huo uliofanyika katika kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) na kumalizika jana jijini Dar es salaam.     Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hania Bwahama akimuelezea mshiriki wa mkutano wa tatu wa Kimataifa wa Kikanda PEN-PLUS (ICPPA 2026) kutoka Boston nchini Marekani Gehe Bakhman huduma zinazotolewa na taasis...

Wakuu wa Taasisi za afya zinazotoa huduma bingwa bobezi wakutana kuboresha ushirikiano na masuala ya tafiti

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akichangia mada wakati wa kikao cha wakuu wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI), Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH),   Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI) na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS)    kuimarisha ushirikiano na kuboresha utoaji wa huduma kilichofanyika jana katika Ukumbi wa MUHAS jijini Dar es Salaam. Wakurugenzi Watendaji kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge, Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) Dkt. Delilah Kimambo, Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) Balozi Ulisubisya Mpoki, Mwakilishi wa Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI)  Dkt. Nazima Dharsee, na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Prof. Appolinary Kamuhabwa wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa kikao cha ujirani mwema kuimarisha ushirikiano na kuboresha utoaji wa huduma ki...

JKCI yashiriki mkutano wa kimataifa kujadili mikakati ya kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza Afrika PEN-PLUS (ICPPA 2026)

Image
  Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hania Bwahama akimuelezea Mshiriki wa mkutano mkuu wa tatu wa Kimataifa wa kikanda PEN-PLUS (ICPPA 2026) kutoka nchini Nigeria Mya Nyon vifaa vinavyotumika wakati wa upasuaji wa moyo alipotembelea banda la JKCI lililopo katika mkutano huo unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) kilichopo jijini Dar es Salaam. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hania Bwahama akimuelezea mtaalamu wa afya kutoka nchini Afrika Kusini Roylah Rykiel kuhusu huduma za upasuaji wa moyo zinazotolewa na Taasisi hiyo wakati wa mkutano mkuu wa tatu wa Kimataifa wa kikanda PEN-PLUS (ICPPA 2026) unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) kilichopo jijini Dar es Salaam. Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Alex Msoka akimuelezea Mkurugenzi Msaidizi wa Elimu kwa Umma Dkt Rahma Hingora kuhusu kampeni ya Jua Namba Zako inayofanywa ...

JKCI kuanzisha kampuni tanzu kuimarisha tiba utalii nchini

Image
Mwenyekiti Msaidizi wa Kamati ya Maandalizi ya mpango mkakati wa watu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Iddi Lemah akizungumza na wafanyakazi wa Taasisi hiyo wakati wa kikao cha kuwasilisha mpango mkakati wa tatu wa JKCI kwa wafanyakazi kilichofanyika jana katika ukumbi wa JKCI iliopo jijini Dar es Salaam. Mshauri wa maandalizi ya mpango mkakati wa watu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Ivan Tarimo akielezea vitu vilivyoanishwa katika mpango mkakati huo wakati wa kikao cha kuwasilisha mpango mkakati wa tatu wa JKCI kwa wafanyakazi kilichofanyika jana katika ukumbi wa Taasisi hiyo uliopo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akielezea namna ambavyo mpango mkakati wa tatu wa JKCI utakavyoboresha huduma wakati wa kikao cha kuwasilisha mpango mkakati huo kwa wafanyakazi kilichofanyika jana katika ukumbi wa Taasisi hiyo iliopo jijini Dar es Salaam. Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwe...

Wataalamu kutoka nchini Namibia watembelea JKCI kuona huduma zinazotolewa

Image
Mkurugenzi wa Idara ya Upasuaji wa Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Angela Muhozya akimpatia zawadi Kaimu Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Uwekezaji na Maendeleo ya nchini Namibia (NIPDB) Jessica Hauuanga wakati wataalamu kutoka nchini Namibia walipofanya ziara katika Taasisi hiyo kwaajili ya kujifunza na kuona namna watashirikiana katika kutoa huduma za matibabu ya moyo kwa wananchi wa Namibia. Fundi Sanifu wa Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Kulindwa Kasubi akielezea huduma zinazotolewa katika chumba cha upasuaji mdogo wa moyo kwa kutumia mtambo wa Cathlab kwa wajumbe kutoka nchini Namibia walipotembelea Taasisi hiyo kwaajili ya kujifunza na kuona huduma zinazotolewa ili wagonjwa kutoka nchini Namibia waanze kupata huduma katika Taasisi hiyo.  Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Alex Joseph akizungumza na ujumbe kutoka nchini Namibia walipotembelea Taasisi hiyo kwaajili ya kujifunza na kuona huduma ...