Siku ya Msikilizaji Habari Maalum Media yaleta uchunguzi wa Moyo bure Ngaramtoni
Matroni wa Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Center (ALMC) inayosimamiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Sr. Flora Kasembe akitoa elimu ya magonjwa ya moyo kwa wananchi waliohudhuria maadhimisho ya Siku ya Msikilizaji yaliyoandaliwa na Habari Maalum Media na kufanyika Ngaramtoni jijini Arusha. Wakazi wa Arusha wakisubiri kupata huduma ya upimaji wa magonjwa ya moyo iliyokuwa inatolewa na wataalamu wa Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Center (ALMC) inayosimamiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa maadhimisho ya Siku ya Msikilizaji yaliyoandaliwa na Habari Maalum Media na kufanyika Ngaramtoni jijini Arusha. Matroni wa Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Center (ALMC) inayosimamiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Sr. Flora Kasembe akimpima shinikizo la damu mkazi wa Arusha wakati wa maadhimisho ya Siku ya Msikilizaji iliyoandaliwa na Habari Maalum Media na kufanyika Ngaramtoni jijini Arusha. Na JKCI ***********************...