Posts

Watu 253 wafanyiwa uchunguzi wa afya mkutano wa e-GA

Image
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akimpatia tuzo Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi wa Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) ambayo kwa sasa inasimamiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Salehe Mwinchete kutambua na kuthamini mchango wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa kufunga kikao kazi cha sita cha Serikali Mtandao kilichofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Arusha (AICC) jijini Arusha.  Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Sahiya Yahya akimsikiliza mmoja wa wafanyakazi aliyepata huduma wakati wa kambi maalumu ya siku tatu ya uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha sita cha Serikali Mtandano kilichofanyika katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Arusha (AICC) jijini Arusha. Mtaalamu wa vipimo vya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Beatrice Mwakabende akimpima mmoja wa wafanyakazi aliyefika katika kambi maalumu ya siku tatu ya uch...

JKCI yahimiza kupima afya mapema: Fursa adimu kwa washiriki wa mkutano wa e-GA

Image
Mkurugezi wa Tiba Shirikishi wa Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) Salehe Mwinchete akipokea zawadi kutoka kwa Afisa mwendesha ofisi wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) Getrude Shirima wakati wa kambi maalumu ya siku tatu ya uchunguzi na matibabu ya moyo katika Kikao kazi cha 6 cha Serikali Mtandao kinachofanyika katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Arusha (AICC). Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Sahiya Yahya akitoa ushauri wa kiafya kwa mfanyakazi wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) wakati wa kambi maalumu ya siku tatu ya uchunguzi na matibabu ya moyo katika Kikao kazi cha 6 cha Serikali Mtandao kinachofanyika katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Arusha (AICC). Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Epifania Mlay akimpima shinikizo la damu (BP) Mfanyakazi wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) aliyehudhuria  kambi maalumu ya siku tatu ya uchunguzi na matibabu ya moyo katika Kikao Kazi cha 6 cha Serikali Mtandao kinachofa...

JKCI yaiweka Tanzania kwenye ramani ya Afrika kwa upasuaji wa Moyo wa kisasa

Image
  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimkabidhi zawadi  Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi hiyo Dkt. Hassan Mahmoud Mshinda alipotembelea JKCI kwa mara ya kwanza leo kwaajili ya kuona utendaji kazi pamoja na kukutana na viongozi.   Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimweleza utendaji kazi wa taasisi hiyo     Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Wadhamini ya JKCI     Dkt. Hassan Mahmoud Mshinda alipotembelea taasisi hiyo     kwa mara ya kwanza leo kwaajili ya kuona utendaji kazi pamoja na kukutana na viongozi.  Baadhi ya viongozi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakimsikiza Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Wadhamini ya JKCI Dkt. Hassan Mahmoud Mshinda alipotembelea taasisi hiyo     kwa mara ya kwanza leo kwaajili ya kuona utendaji kazi pamoja na kukutana na viongozi. *************************************************************...

Uchunguzi wa Afya kwenye Kazi: JKCI yawafikia Watumishi wa Serikali

Image
Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi wa  Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) ambayo kwa sasa inasimamiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Salehe Mwinchete akitoa elimu ya magonjwa ya moyo kwa watumishi wa umma wanaoshiriki Kikao kazi cha 6 cha Serikali Mtandao kinachofanyika katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Arusha (AICC) . Wataalamu wa JKCI wanatoa huduma ya Uchunguzi na matibabu ya moyo kwenye kikao kazi hicho. Mtaalamu wa vipimo vya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Beatrice Mwakabende akimpima Mtumishi wa Umma kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi wakati wa  Kikao kazi cha 6 cha Serikali Mtandao kinachofanyika katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Arusha (AICC). Afisa Uuguzi wa Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) ambayo kwasasa inasimamiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Nadia Zuberi akimpima kipimo cha kuangalia uwiano baina ya urefu na uzito (BMI) Mtumishi wa Umma aliyehudhuria Kikao Kazi cha...

Ushirikiano wa Kimataifa: JKCI na Poland kufungua milango ya Utafiti na Mafunzo ya Kitaalamu

Image
Balozi wa Poland nchini Tanzania Mhe. Sergiusz Wolski akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge na wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Jagiellonian kilichopo nchini Poland walipotembelea ubalozi huo leo kwaajili ya kuona namba watakavyofanya  ushirikiano na JKCI katika masuala ya utafiti, ujuzi na “ grants”. Balozi wa Poland nchini Tanzania Mhe. Sergiusz Wolski akizungumza na ujumbe kutoka chuo Kikuu cha Jagiellonian kilichopo nchini Poland walipotembelea ubalozi huo leo kwaajili ya kuona namna ya kufanya ushirikiano na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) katika masuala ya utafiti, ujuzi na “ grants”. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akielezea huduma zinazotolewa na Taasisi hiyo wakati wa kikao na Balozi wa Poland nchini Tanzania Mhe. Sergiusz Wolski kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam cha kujadili namna Taasisi hiyo itakavyoshirikiana na Chuo Kikuu cha Jagiellonia...

ALMC na MOI kuendesha kambi maalumu ya matibabu ya magonjwa ya mifupa Arusha

Image
 Mkurugenzi wa Magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tatizo Waane akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kambi maalumu ya siku 5 ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa mbalimbali ya mifupa na mishipa ya fahamu itakayofanywa na wataalamu wa  Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) ambayp inayosimamiwa na JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa Taasisi ya Tiba na Mifupa Muhimbili (MOI). Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) Antony Assey akielezea huduma ambazo Taasisi hiyo itazitoa wakati wa kambi maalumu ya siku 5 ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa mbalimbali ya mifupa na mishipa ya fahamu itakayofanyika tarehe 23-27/02/2026 katika Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) inayosimamiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI). Baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifuatilia mkutano na waandishi wa habari kuhusu kambi maalumu ya siku 5 ya uchunguzi na matibabu ya magonjw...

Watu zaidi ya 300 wafanyiwa uchunguzi wa afya na JKCI Tamasha la IST Festival

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila akizungumza na wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) alipotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa Tamasha la IST Festival lililofanyika jana katika viwanja vya Coco Beach vilivyopo jijini Dar es Salaam.  Daktari wa kinywa na meno wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Aitham Mohamed akimfanyia uchunguzi wa kinywa mwananchi aliyetembelea banda la Hospitali hiyo kwaajili ya kupata huduma wakati wa Tamasha la IST Festival lililofanyika jana katika viwanja vya Coco Beach vilivyopo jijini Dar es Salaam. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Fakihi Mguwalo akimpima shinikizo la damu (BP) Mkurugenzi wa Halmashauri jiji la Dar es Salaam Elihuruma Mabelya aliyetembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa Tamasha la IST Festival lililofanyika jana katika viwanja vya Coco Beach vilivyopo jijini Dar es Salaam. Afisa huduma kwa wateja wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Stephano Zavara ...