JKCI mshindi wa kwanza watoa huduma bora za afya na tiba maonesho ya SABASABA
Waziri wa Kazi na Uwekezaji Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Shariff Ali Shariff akimkabidhi tuzo ya mshindi wa kwanza kwa utoaji wa huduma bora za afya na tiba Mkurugenzi wa Fedha na Mipango wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) CPA. Agnes Kuhenga wakati wa hafla ya kufunga maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA). Afisa uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Simon Sawe akimpima kiwango cha sukari kwenye damu mkazi wa Dar es Salaam aliyetembelea banda la JKCI wakati wa maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA) yaliyofungwa jana jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Fedha na Mipango wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) CPA. Agnes Kuhenga akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Taasisi hiyo mara baada ya kuibuka washindi wa kwanza wa mtoa huduma bora za afya na tiba katika maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA). Picha na JKCI ***************************************************...