Watumishi wa Wizara ya Fedha wanufaika na kambi maalumu ya uchunguzi wa Moyo
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akitoa elimu ya magonjwa ya moyo kwa mfanyakazi wa Wizara ya Fedha wakati wa kambi maalumu ya upimaji wa afya kwa watumishi hao iliyomalizika jana jijini Dodoma. Baadhi ya watumishi wa Wizara ya Fedha wakisubiri kupata huduma za uchunguzi wa afya zinazotolewa na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa kambi maalumu ya upimaji wa afya iliyomalizika jana jijini Dodoma. Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mohamed Aloyce akitoa elimu ya “ Jua Namba Zako ” kwa mtumishi wa Wizara ya Fedha wakati wa kambi maalumu ya upimaji wa afya kwa watumishi hao iliyomalizika jana jijini Dodoma. Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Moris Budotela akitoa elimu ya “ Jua Namba Zako ” kwa Afisa Sheria wa Idara ya Huduma za Sheria wa Wizara ya Fedha Yohana Msengi wakati wa kambi maalumu ya upimaji wa afya iliyomalizika jana jiji...