Watu zaidi ya 300 wafanyiwa uchunguzi wa afya na JKCI Tamasha la IST Festival
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila akizungumza na wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) alipotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa Tamasha la IST Festival lililofanyika jana katika viwanja vya Coco Beach vilivyopo jijini Dar es Salaam. Daktari wa kinywa na meno wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Aitham Mohamed akimfanyia uchunguzi wa kinywa mwananchi aliyetembelea banda la Hospitali hiyo kwaajili ya kupata huduma wakati wa Tamasha la IST Festival lililofanyika jana katika viwanja vya Coco Beach vilivyopo jijini Dar es Salaam. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Fakihi Mguwalo akimpima shinikizo la damu (BP) Mkurugenzi wa Halmashauri jiji la Dar es Salaam Elihuruma Mabelya aliyetembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa Tamasha la IST Festival lililofanyika jana katika viwanja vya Coco Beach vilivyopo jijini Dar es Salaam. Afisa huduma kwa wateja wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Stephano Zavara ...