Posts

Dkt. Kisenge awapongeza Wafanyakazi JKCI, Asisitiza ufanisi na weledi kazini

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimkabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni tano Mfanyakazi Hodari wa taasisi hiyo kwa mwaka wa fedha wa 2025/2026 Afisa Tawala Adila Musa wakati wa hafla ya kuwatambua na kuwapongeza wafanyakazi Hodari iliyofanyika jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimkabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni mbili Mfanyakazi Hodari wa taasisi hiyo nafasi ya pili kwa mwaka wa fedha wa 2025/2026 Mkaguzi wa Hesabu za Ndani Sitty Hamis wakati wa hafla ya kuwatambua     na kuwapongeza wafanyakazi Hodari iliyofanyika jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimkabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni moja na nusu Mfanyakazi Hodari wa taasisi hiyo nafasi ya tatu kwa mwaka wa fedha wa 2025/2026 Afisa Muuguzi Edna Kajuna wakati wa hafla ya kuwatambua na kuwapongeza wafanyakazi hodari ili...

JKCI na TBS waungana kuboresha Afya ya Wafanyakazi kupitia upimaji wa Moyo

Image
Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Agnes Kajangwa akimpima kiwango cha sukari kwenye damu Mkurugenzi wa Uandaaji Viwango wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) David Ndibalema Lugome wakati wa kambi maalumu ya upimaji wa magonjwa ya moyo iliyolenga kuongeza uelewa kuhusu magonjwa hayo na njia za kujikinga ili kuboresha afya na ufanisi kazini kwa wafanyazi wa shirika hilo. Jumla ya Wafanyakazi 68 walipata huduma ambapo nane kati yao walipewa rufaa ya kwenda kutibiwa katika Tawi la JKCI Oysterbay. Afisa Masoko wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Agness Mndasha akimkabidhi vipeperushi vya taasisi hiyo Afisa Utumishi Mwandamizi wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Mariam Mbarouk wakati wa kambi maalumu ya upimaji wa magonjwa ya moyo iliyolenga kuongeza uelewa kuhusu magonjwa hayo na njia za kujikinga ili kuboresha afya na ufanisi kazini kwa wafanyazi wa shirika hilo. Jumla ya Wafanyakazi 68 walipata huduma ambapo nane kati yao walipewa rufaa ya kwenda ku...

Wafanyakazi JKCI Dar Group wapewa onyo dhidi ya ubadhilifu wa mali za Umma

Image
Mkurugenzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Dkt. Tulizo Shemu akizungumza   na wafanyakazi wa Hospitali hiyo hiyo jana   jijini Dar es Salam wakati   wa hafla ya kuwatambua wafanyakazi bora kuelekea maadhimisho ya Sikukuu ya Wafanyakazi duniani. Mkurugenzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Dkt. Tulizo Shemu akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa taasisi hiyo wakati   wa hafla ya kuwatambua wafanyakazi bora kuelekea maadhimisho ya Sikukuu ya Wafanyakazi Duniani. Na JKCI **************************************************************************************************** Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group wametakiwa kuepuka ubadhilifu katika matumizi ya mali za umma ikiwemo matumizi yasiyo sahihi ya vifaa vya ofisi pamoja na vitendo vya uhujumu uchumi vinavyoweza kuathiri utendaji wa kazi za taasisi. Rai hiyo imetolewa  jana na Mkurugenzi wa JKCI Hospital...

Serikali yajipanga kusogeza huduma bingwa za Moyo karibu na Wananchi

Image
Meneja wa Rasilimali watu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Abdulrahman Muya akimkabidhi Waziri wa Kazi Mhe. Deus Clement Sanga zawadi ya mashine ya BP, RBG na Thermometer kama sehemu ya kampeni ya kuhamasisha jamii kujua namba zao za afya alipotembelea banda la taasisi hiyo lililopo kwenye maonesho ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi yanayofanyika katika Viwanja vya Shule ya Msingi Mji Mwema Mjini Njombe. Daktari bingwa wa magonjwa yatokanayo na kazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Elius Birago akimueleza  Waziri wa Kazi Mhe. Deus Clement Sanga huduma zinazotolewa na Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi yanayofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Mji Mwema Mjini Njombe. Daktari bingwa wa magonjwa yatokanayo na kazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Elius Birago akimpa zawadi Mganga Mkuu wa Mkoa wa Njombe Dkt. Juma Mfanga alipotembelea banda la Taasisi hiyo wa...

Wafanyakazi JKCI Watakiwa Kujituma Ili Kuongeza Kipato Chao

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dr. Peter Kisenge akizungumza na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa taasisi hiyo wakati wa mkutano wa baraza hilo uliofanyika leo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Fedha na Mipango wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) CPA. Agnes Kuhenga akisoma mapato na matumizi wakati wa Mkutano wa Baraza la kumi la Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) uliofanyika jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi kutoka Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya Tanzania (TUGHE) Makao Makuu Taifa Shedrack Mgodo akizungumza na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa taasisi hiyo wakati wa mkutano wa baraza hilo uliofanyika leo jijini Dar es Salaam. Wajumbe   wa Baraza la Wafanyakazi la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)   wakimsikiliza   Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Dkt. Peter Kisenge alipokuwa akizungumza   nao wakati wa Mkutano wa Baraza la kumi la JKCI lililofanyika leo jijini Dar es...

Huduma za Moyo zawafikia wananchi Njombe, DC atoa ombi Maalumu

Image
Mkuu wa Wilaya ya Njombe Mhe. Juma Sweda akimsikiliza daktari bingwa wa magonjwa yatokanayo na kazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Elius Birago alipotembelea banda la Taasisi hiyo lililopo katika maonesho ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi ili kuona huduma za matibabu zinazotolewa. Daktari wa kinywa na meno wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Joachim Mvungi akichunguza kinywa cha mwananchi aliyejitokeza kufanya uchunguzi wa afya wakati wa maonesho ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi yanayofanyika katika Viwanja vya Shule ya Msingi Mji Mwema Mkoani Njombe. Afisa Masoko wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Rajabu Hamis akiwaelezea wakazi wa Njombe huduma zinazotolewa na Taasisi hiyo walipotembelea banda la JKCI lililopo katika maonesho ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi yanayofanyika katika Viwanja vya Shule ya Msingi Mji Mwema Mkoani Njombe. Na JKCI ******************************************************************************...

JKCI, Israel waimarisha huduma za upasuaji wa Moyo kwa watoto 252

Image
Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Naizihijwa Majani akitoa historia ya JKCI kwa balozi wa Israel nchini Tanzania Mhe. Gideon Behar wakati alipotembelea Taasisi hiyo hiyo hivi  karibuni kwaajili ya kuona huduma za kibingwa za matibabu ya moyo zinazotolewa  pamoja na uwekezaji mkubwa uliofanywa na serikali ya Tanzania katika matibabu ya moyo.  Balozi wa Israel nchini Tanzania Mhe. Gideon Behar akiongea na waandishi wa habari wakati alipotembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) hivi karibuni kwaajili ya kuona huduma za kibingwa za matibabu ya moyo zinazotolewa pamoja na   uwekezaji mkubwa uliofanywa na serikali ya Tanzania katika matibabu ya moyo.  Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Naizihijwa Majani akimkabidhi zawadi Balozi wa Israel nchini Tanzania Mhe. Gideon Behar  alipotembelea JKCI hivi karibuni kwaajili ya kuona huduma za kibingwa za matibabu ya moyo zinazotolewa p...