JKCI yaimarisha ufanisi kwa mafunzo ya Usalama na Afya kwa wafanyakazi
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akiwaeleza wafanyakazi wa Taasisi hiyo umuhimu wa kuzingatia usalama wa wagonjwa wanaowahudumia pamoja na wao wenyewe wakati wa mafunzo ya umuhimu wa fidia kwa wafanyakazi na usalama mahali pa kazi yaliyofanyika leo jijini Dar es Salaam. Afisa Mkaguzi Mazingira ya Kazi kutoka Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) Simon Lwaho akitoa elimu kuhusu usalama wa wafanyakazi mahala pa kazi kwa wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI). Afisa Matekelezo kutoka Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Calvin Urassa akitoa elimu na kuainisha aina za fidia zinazotolewa na mfuko huo kwa wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) yaliyotolewa leo katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifuatilia mafunzo ya usalama na afya mahala pa kazi yaliyokuwa yakitolewa na mtaalamu kutoka (OSHA) pamoja na mafunzo ya umu...