Mhe. Makonda awahimiza wananchi wa Arusha kupima afya ya moyo
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Paul Makonda akiangalia daftari maalumu la usajiri wa wagonjwa alipotembelea banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa kambi maalumu ya kupima na kutibu magonjwa ya binadamu inayofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid uliopo jijini Arusha. Wapili kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Dkt. Peter Kisenge Afisa Uuguzi wa Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) ambayo inasimamiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Nadia Zuberi akimuonesha majibu ya sukari kwenye damu mwananchi aliyefika kufanya uchunguzi wa afya katika banda la JKCI wakati wa kambi maalumu ya kupima na kutibu magonjwa ya binadamu inayofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid uliopo jijini Arusha. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hania Bwahama akimpima shinikizo la damu (BP) mwananchi aliyefika kufanya uchunguzi wa afya katika banda la Taasisi hiyo wakati wa kambi maalumu ya kupima na kutibu magonjwa ya binada...