Posts

JKCI yatoa huduma za uchunguzi wa afya Bonanza la NBC

Image
  Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Ditram Mgimba akimpima uwiano wa urefu kwa uzito (BMI) mkazi wa Dar es Salaam aliyefika katika viwanja vya Police Office Mess Oysterbay wakati wa bonanza la NBC kuelekea mbio za NBC zitakazofanyika Julai 26 mwaka huu kwaajili ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa na JKCI Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Moris Budotela akimuelezea umuhimu wa kupima afya mkazi wa Dar es Salaam aliyefika katika viwanja vya Police Office Mess Oysterbay wakati wa bonanza la NBC kuelekea mbio za NBC zitakazofanyika Julai 26 mwaka huu kwaajili ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa na JKCI. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Ditram Theodory Mgimba akimpima shinikizo la damu mkazi wa Dar es Salaam aliyefika katika viwanja vya Police Office Mess Oysterbay wakati wa bonanza la NBC kuelekea mbio za NBC zitakazofanyika Julai 26 mwaka huu kwaajili ya kuchangia matib...

Mhe. Fatma Nyangasa awahamasisha wananchi kupima afya kupitia Kampeni ya Jua Namba Zako

Image
Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Thabit Ramadhani akumueleza Mkuu wa Wilaya ya Kondoa Mhe. Fatma Almasi Nyangasa namna moyo unavyofanya kazi alipotembelea banda la Taasisi hiyo lililopo katika maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Idd Kimario akimpima Shinikizo la damu Mkuu wa Wilaya ya Kondoa Mhe. Fatma Almasi Nyangasa alipotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. Mkuu wa Wilaya ya Kondoa Mhe. Fatma Almasi Nyangasa akitazama mfano wa saani ya makundi ya chakula alipotembelea banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) lililopo katika maonesho ya 50 ya Biashara ya...

JKCI na BMH waimarisha utalii tiba, wafanya upasuaji wa moyo kwa watoto kutoka nchini Burundi

Image
Wataalamu wa upasuaji wa moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) wakimfanyia upasuaji wa moyo mtoto mwenye tundu kwenye moyo kutoka nchini Burundi wakati wa kambi maalumu ya upasuaji wa moyo kwa watoto iliyokuwa ikifanyika katika Hospitali hiyo iliyopo jijini Dodoma. Wataalamu wa kuhudumia wagonjwa wa dharura na wanaohitaji uangalizi maalumu (ICU) wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakimuhudumia mtoto kutoka nchini Burundi aliyefanyiwa upasuaji wa moyo katika kambi maalumu iliyofanywa na wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH) iliyopo jijini Dodoma. Wataalamu wa upasuaji wa moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) wakimfanyia upasuaji wa moyo mtoto mwenye tundu kwenye moyo kutoka nchini Burundi wakati wa kambi maalumu ya upasuaji wa moyo kwa watoto iliyokuwa ikifanyika katika Hos...

JKCI yapongezwa kwa kuanza kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050

Image
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Mhe. Prof. Kitila Mkumbo akiweka jiwe la msingi la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) tawi la Temeke kwa niaba ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mwigulu Nchemba jana wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi iliyofanyika katika Taasisi hiyo tawi la Dar Group lililopo Tazara jijini Dar es Salaam. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Mhe. Prof. Kitila Mkumbo, Naibu Waziri wa Afya Dkt. Florence Samizi na viongozi mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) tawi la Temeke iliyofanyika jana katika Hospitali ya JKCI Dar Group iliyopo Tazara jijini Dar es Salaam. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Mhe. Prof. Kitila Mkumbo akipokea zawadi kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Hassan Mahmoud Mshinda wakati wa hafla ya uwekaji jiwe la msingi la Taasis...

Wananchi wahimizwa kuzingatia lishe bora kujikinga na magonjwa ya moyo

Image
Afisa Lishe wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Emmanuel Lingindo akimuelezea kuhusu uwiano wa urefu kwa uzito (BMI) mwananchi aliyetembelea banda la Taasisi hiyo lililopo katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Abdulahman Njale akiwaonesha baadhi ya vifaa vinavyotumika katika chumba cha upasuaji wa moyo wananchi waliotembelea banda la Taasisi hiyo lililopo katika maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. *************************************************************************************************************** Vyakula vyenye mafuta mengi, sukari, chumvi kupita kiasi pamoja na vyakula vya wanga kwa wingi vyatajwa kuwa miongoni mwa vicho...

Wananchi wahimizwa kutumia kampeni ya “Jua Namba Zako” kupima afya zao SABASABA

Image
Mwenyekiti Tume ya Madini Dkt. Janeth Lekashingo akimsikiliza Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Edna Kajuna alipotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Juliaus Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.  Afisa Tehama wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Kliniki ya Oysterbay Suleiman Jafari akimuelezea namna shuka maalumu la Dozee linavyofanya kazi Mwenyekiti Tume ya Madini Dkt. Janeth Lekashingo alipotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Juliaus Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. Daktari wa wagonjwa wa dharura wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospital ya Dar Group Peace Masaoe akimuelezea huduma za dharura zinazotolewa na Taasisi hiyo Mwenyekiti Tume ya Madini Dkt. Janeth Le...

JKCI na BMH kuokoa maisha ya watoto wenye magonjwa ya moyo kutoka nchini Burundi

Image
Wataalamu wa upasuaji wa moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakishirikiana na wenzake wa Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) kumfanyia upasuaji wa moyo mtoto mwenye tundu kwenye moyo kutoka nchini Burundi wakati wa kambi maalumu ya upasuaji wa moyo kwa watoto inayofanyika katika Hospitali ya Benjamini Mkapa iliyopo jijini Dodoma. Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) Prof. Abel Makubi akizungumza na wataalamu wa upasuaji wa moyo kwa watoto kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) walipofika katika Hospitali hiyo kwaajili ya kubadilishana ujuzi pamoja na kufanya kambi maalumu ya upasuaji wa moyo kwa watoto. Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Stella Mongela akimpima kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (ECHO) mtoto kutoka nchini Burundi wakati wa kambi maalumu ya upasuaji wa moyo kwa watoto inayofanyika katika Hospitali ya Benjamini Mkapa iliyopo jijini Dodoma. Mkurugenzi Mtendaji w...