JKCI yapima Wanamichezo 482, Yatoa elimu ya aya ya Moyo
Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dar Group ambaye pia ni mratibu wa magonjwa ya moyo kwa wanamichezo Eva Wakuganda akisalimiana na Mkuu wa Chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es salaam (DPA) Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Dkt. Lazaro Mambosasa wakati alipotembelea ofisini kwake kuaga na kuwasilisha ripoti ya mwenendo wa kambi maalumu ya siku tano ya upimaji wa magonjwa ya moyo kwa wanamichezo na Askari Polisi walioshiriki mashindano ya Dkt. Mambosasa Cup yaliyomalizika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dar Group Christina Yonatham akimsajili Askari Polisi wa Chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es salaam (DPA) wakati wa kambi maalumu ya upimaji wa magonjwa ya moyo kwa wanamichezo na Askari Polisi walioshiriki mashindano ya Dkt. Mambosasa Cup yaliyomalizika hivi karibuni katika Chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es salaam (DPA). Wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ...