Wananchi wahimizwa kuzingatia lishe bora kujikinga na magonjwa ya moyo
Afisa Lishe wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Emmanuel Lingindo akimuelezea kuhusu uwiano wa urefu kwa uzito (BMI) mwananchi aliyetembelea banda la Taasisi hiyo lililopo katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Abdulahman Njale akiwaonesha baadhi ya vifaa vinavyotumika katika chumba cha upasuaji wa moyo wananchi waliotembelea banda la Taasisi hiyo lililopo katika maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. *************************************************************************************************************** Vyakula vyenye mafuta mengi, sukari, chumvi kupita kiasi pamoja na vyakula vya wanga kwa wingi vyatajwa kuwa miongoni mwa vicho...