Wataalamu kutoka nchini Namibia watembelea JKCI kuona huduma zinazotolewa
Mkurugenzi wa Idara ya Upasuaji wa Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Angela Muhozya akimpatia zawadi Kaimu Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Uwekezaji na Maendeleo ya nchini Namibia (NIPDB) Jessica Hauuanga wakati wataalamu kutoka nchini Namibia walipofanya ziara katika Taasisi hiyo kwaajili ya kujifunza na kuona namna watashirikiana katika kutoa huduma za matibabu ya moyo kwa wananchi wa Namibia. Fundi Sanifu wa Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Kulindwa Kasubi akielezea huduma zinazotolewa katika chumba cha upasuaji mdogo wa moyo kwa kutumia mtambo wa Cathlab kwa wajumbe kutoka nchini Namibia walipotembelea Taasisi hiyo kwaajili ya kujifunza na kuona huduma zinazotolewa ili wagonjwa kutoka nchini Namibia waanze kupata huduma katika Taasisi hiyo. Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Alex Joseph akizungumza na ujumbe kutoka nchini Namibia walipotembelea Taasisi hiyo kwaajili ya kujifunza na kuona huduma ...