Mkazi wa Temeke apongeza huduma za upasuaji wa moyo alizofanyiwa JKCI
Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Agness Samuel akiangalia mapigo ya moyo ya mgonjwa Jonathan Mwanayongo aliyefanyiwa upasuaji wa kuzibua mishipa ya damu ya moyo bila kusimamisha moyo na wataalamu wa JKCI wakishirikiana na wenzao kutoka Hospitali ya Jaslok ya nchini India. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Agnes Samuel akimuhudumia mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji wa kuzibua mishipa ya damu ya moyo bila kusimamisha moyo Jonathan Mwanayongo. Mgonjwa huyo amefanyiwa upasuaji huo na wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao kutoka Hospitali ya Jaslok ya nchini India. *************************************************************************************************** Mkazi wa Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam Jonathan Mwanayongo ameipongeza Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kufanikisha upasuaji mkubwa wa moyo uliokuwa ufanyike nchini India. Akizungumza na Mwandishi wa habari hii Jonathan alisema amegundulika kuwa na matatizo la ...