Posts

JKCI yaimarisha ufanisi kwa mafunzo ya Usalama na Afya kwa wafanyakazi

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akiwaeleza wafanyakazi wa Taasisi hiyo umuhimu wa kuzingatia usalama wa wagonjwa wanaowahudumia pamoja na wao wenyewe wakati wa mafunzo ya umuhimu wa fidia kwa wafanyakazi na usalama mahali pa kazi yaliyofanyika leo jijini Dar es Salaam. Afisa Mkaguzi Mazingira ya Kazi kutoka Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) Simon Lwaho akitoa elimu kuhusu usalama wa wafanyakazi mahala pa kazi kwa wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI). Afisa Matekelezo kutoka Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Calvin Urassa akitoa elimu na kuainisha aina za fidia zinazotolewa na mfuko huo kwa wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) yaliyotolewa leo katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifuatilia mafunzo ya usalama na afya mahala pa kazi yaliyokuwa yakitolewa na mtaalamu kutoka (OSHA) pamoja na mafunzo ya umu...

Utafiti JKCI wachambua uhusiano kati ya dawa za moyo za SGLT2i na Afya ya njia ya mkojo

Image
Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Samueli Rweyemamu akimpima kipimo cha kuangali jinsi moyo unavyofanya kazi mkazi wa Kitunda. ****************************************************************************************************************** Utafiti mpya uliofanyika katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) jijini Dar es Salaam umebaini kuwepo kwa ongezeko la maambukizi ya njia ya mkojo (UTI) miongoni mwa wagonjwa wa moyo wanaotumia dawa aina ya Sodium-Glucose Co-Transporter 2 Inhibitors (SGLT2i) zikiwemo dapagliflozin na empagliflozin. Dawa hizo ambazo zimekuwa msaada mkubwa katika matibabu ya magonjwa ya moyo na figo sasa zinaibua mjadala mpya kufuatia kuhusishwa na hatari ya kuongezeka kwa maambukizi ya UTI kwa baadhi ya wagonjwa. Utafiti huo uliofanywa na Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa JKCI Dar Group Samueli Rweyemamu kwa kushirikiana na wataalamu wenzake na kuchapishwa katika Jarida la PLOS ONE la nc...

Msaada wa Rais Samia wamfungulia milango ya matibabu: Mtoto mwenye tatizo la Moyo aanza safari JKCI

Image
 Wataalamu wa upasuaji wa Moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifanya upasuaji wa kuziba tundu la moyo wa mtoto. ***************************************************************************************************************************************************************************************************** Mtoto Selina Daudi anayekabiliwa na changamoto ya tundu kwenye moyo ameanza rasmi safari ya matibabu katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kufuatia kupatiwa msaada wa kifedha na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. Selina anayeishi na mama yake Aisha Said katika eneo la Chanika jijini Dar es Salaam anatarajiwa kupata huduma za kibingwa zitakazomsaidia kurejea katika hali yake ya kawaida kiafya. Akizungumzia hatua hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Peter Kisenge alisema msaada uliotolewa na Mhe. Rais Dkt. Samia umefungua ukurasa mpya wa matumaini kwa mtoto huyo huku gharama za matibabu zikifikia zaidi ya shil...

Mapinduzi sekta ya Afya: JKCI yaleta teknolojia ya Roboti ya bilioni 5.5

Image
Mtaalamu wa Maabara wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mariam Steven akiangalia hatua za upimaji wa sampuli za damu zinavyofanyika katika maabara ya kisasa ya taasisi hiyo inayotumia teknolojia ya roboti.  Mtaalamu wa Maabara wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Glory Mtui akiiruhusu roboti kuendelea na upimaji wa sampuli za damu kwa kutumia teknolojia ya roboti inayotumika katika maabara ya kisasa ya taasisi hiyo.  Mtaalamu wa Maabara wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Glory Mtui akipanga sampuli za damu tayari kwa upimaji kwa kutumia teknolojia ya roboti inayotumika katika maabara ya kisasa ya taasisi hiyo. ************************************************************************************************************************************************************************************************************************ Sekta ya afya nchini imepiga hatua kubwa kufuatia Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kuanza kutumia maabara ya kisasa yenye teknolojia y...

Dkt. Kisenge: Waandishi wa habari tumieni kalamu zenu kuhamasisha jamii kujua namba zao za afya

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na waandishi wa habari kuhusu miradi ya maendeleo inayofanywa na Taasisi hiyo wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika leo katika Ukumbi wa Idara ya Habari - MAELEZO ulipo Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Jijini Dodoma. Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia hotuba iliyokuwa ikitolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge wakati wa mkutano na waandishi hao uliofanyika leo katika Ukumbi wa Idara ya Habari - MAELEZO ulipo Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Jijini Dodoma. Na JKCI *************************************************************************************************** Waandishi wa habari nchini wametakiwa kutumia kalamu zao na kushirikiana na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kuihamasisha jamii kujua namba zao za afya ili iweze kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza kujenga taifa imara na lenye afya b...

Matumizi ya shisha na sigara kusababisha magonjwa ya moyo, matatizo ya mapafu na saratani

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza wakati wa hafla fupi ya kuzindua taarifa ya mwaka 2025 kuhusu   Kampuni za Tumbaku zinavyoingilia Sera ya Afya nchini iliyofanywa na Chama cha Kudhibiti Tumbaku Tanzania (TTCF) katika ukumbi wa JKCI iliyopo jijini Dar es Salaam. Na JKCI ************************************************************************************************* Vijana na wananchi kwa ujumla wametakiwa kutunza afya zao na kujiepusha na matumizi ya tumbaku hususani sigara na shisha yanayoweza kupelekea magonjwa ya moyo, matatizo ya mapafu na saratani hivyo kusababisha vifo vya ghafla. Rai hiyo imetolewa na Mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge hivi karibuni wakati wa hafla fupi ya kuzindua taarifa ya mwaka 2025 kuhusu   Kampuni za Tumbaku zinavyoingilia Sera ya Afya nchini iliyofanywa na Chama cha Kudhibiti Tumbaku Tanzania (TTCF) katika ukumbi wa JKCI iliyopo jijini Dar es...

Ushirikiano wataalamu wa JKCI na China kuokoa maisha na kupunguza rufaa za wagonjwa wa moyo kwenda nje ya nchi

Image
Mkurugenzi wa upasuaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Angela Muhozya akizungumza wakati wa hafla fupi ya kuwaaaga madaktari bingwa wa moyo kutoka Jamhuri ya Watu wa China waliokuwa wakifanya kazi katika Taasisi hiyo kwa kipindi cha miaka miwili. Hafla hiyo imefanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa JKCI iliyopo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi wa upasuaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Angela Muhozya akimkabidhi zawadi daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto kutoka Jamhuri ya watu wa China Zhao Lijian wakati wa hafla fupi ya kuwaaaga madaktari kutoka China iliyofanyika leo katika ukumbi wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi wa upasuaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Angela Muhozya akimkabidhi cheti daktari bingwa wa wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu kutoka Jamhuri ya watu wa China Zhang Mingming wakati wa hafla fupi ya kuwaaaga madaktari kutoka wa China iliyofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa JKCI iliyo...