Mkurugenzi wa Hospitali ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Dkt. Tulizo Shemu akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mafanikio ya hospitali hiyo kwa mwaka 2025 leo wakati wa mkutano huo uliofanyika katika hospitali hiyo iliyopo Tazara jijini Dar es Salaam. Baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group wakisikiliza wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu mafanikio ya hospitali hiyo kwa mwaka 2025 uliofanyika leo JKCI Hospitali ya Dar Group iliyopo Tazara jijini Dar es Salaam. Na: JKCI *********************************************************************************************************** Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group imetoa huduma za upimaji na matibabu ya magonjwa mbalimbali kwa watu 138,699 kwa mwaka 2025. Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Hospitali ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Dkt. Tu...