Wizara ya Afya, JKCI na Children’s HeartLink waweka mikakati ya kuimarisha huduma za moyo kwa watoto nchini
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akiwa katika picha ya pamoja na wadau wa sekta ya afya na viongozi kutoka Wizara ya Afya mara baada ya mkutano na wadau hao kuweka mikakati ya kitaifa kuimarisha huduma za matibabu ya moyo kwa watoto uliofanyika jana katika ukumbi wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akielezea namna Taasisi hiyo inavyotoa huduma kwa watoto wenye magonjwa ya moyo wakati wa mkutano na wadau wa afya kuweka mikakati ya kitaifa kuimarisha huduma za matibabu ya moyo kwa watoto uliofanyika jana katika ukumbi wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi wa huduma za tiba Wizara ya Afya Dkt. Hamad Nyembea akizungumza wakati wa mkutano na wadau wa afya kuweka mikakati ya kitaifa kuimarisha huduma za matibabu ya moyo kwa watoto uliofanyika jana katika ukumbi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo jijini Dar es Salaam. M...