Kampeni ya “Jua Namba Zako” yawafikia Mashabiki wa Arsenal
Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Joyce Kyando akimuonesha shabiki wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Arsenal namba tano za afya zinazohimizwa na Wizara ya afya kuzingatia ili kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza wakati wa tukio la Ongea na Waziri wa Afya lililofanyika katika halfa ya kufurahia ushindi wa Timu ya Arsenal leo katika uwanja wa Posta Kijitonyama jijini Dar es Salaam. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Henry Mimbo akimpima sukari kwenye damu shabiki wa Arsenal aliyefika katika banda la JKCI wakati wa tukio la Ongea na Waziri wa Afya lililofanyika katika halfa ya kufurahia ushindi wa Timu ya Arsenal leo katika uwanja wa Posta Kijitonyama jijini Dar es Salaam. Afisa Utafiti wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Loveness Mfanga akimpima urefu na uzito shabiki wa Arsenal aliyefika katika banda la JKCI wakati wa tukio la Ongea na Waziri wa Afya lililofanyika katika halfa ya kufurahia ushindi wa Timu ya Arsenal leo katika uwanja wa Posta...