JKCI yafanya upasuaji wa Nikaidoh kwa mtoto wa miaka miwili
Wataalamu wa upasuaji wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakimfanyia upasuaji wa moyo mtoto wa miaka miwili (Nikaidoh Operation) kwa kushirikiana na daktari bingwa wa upasuaji wa moyo kutoka Uturuki Ahmet Sasmazel wa Mradi wa Liitle Aid wa Shirika la Muntada Aid jijini Dar es Salaam. Mama wa mtoto Deus Mgonzo, Witness Kibuga akiwa na Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Idd Kimaro katika chumba cha ungalizi wa watoto (PICU) alipolazwa mtoto huyo jijini Dar es Salaam Picha na JKCI *********************************************************************************************************** Na Mwandishi Maalumu-Dar es Salaam Kwa mara ya kwanza watalamu wa upasuaji wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na mwenzao kutoka Mradi wa Little Heart wa Shirika la Muntada lililopo nchini Uingereza Dkt. Ahmet Sasmazel wamemfanyia upasuaji wa moyo mtoto aliyezaliwa na mishipa miwili mikubwa ya damu inayotoka kwenye moyo kupishana (Nikaido...