Benki ya NBC kuchangia kiasi cha shilingi bilioni 1 matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba akimkabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni 200 Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Naizihijwa Majani kwaajili ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa JKCI iliyotolewa na Benki ya NBC kupitia mbio za NBC zilizofanyika jana jijini Dodoma. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba akisalimiana na Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Naizihijwa wakati wa mbio za NBC zilizofanyika jana katika uwanja wa michezo Jamhuri uliopo jijini Dodoma. Mjumbe wa bodi ya wadhamini wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Kassim Hussein akishiriki katika mazoezi ya viungo wakati wa mbio za NBC zilizofanyika jana katika uwanja wa michezo Jamhuri uliopo jijini Dodoma kwaajili ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa JKCI. Wafanyakazi wa Taasis...