Huduma za Moyo zawafikia wananchi Njombe, DC atoa ombi Maalumu
Mkuu wa Wilaya ya Njombe Mhe. Juma Sweda akimsikiliza daktari bingwa wa magonjwa yatokanayo na kazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Elius Birago alipotembelea banda la Taasisi hiyo lililopo katika maonesho ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi ili kuona huduma za matibabu zinazotolewa. Daktari wa kinywa na meno wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Joachim Mvungi akichunguza kinywa cha mwananchi aliyejitokeza kufanya uchunguzi wa afya wakati wa maonesho ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi yanayofanyika katika Viwanja vya Shule ya Msingi Mji Mwema Mkoani Njombe. Afisa Masoko wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Rajabu Hamis akiwaelezea wakazi wa Njombe huduma zinazotolewa na Taasisi hiyo walipotembelea banda la JKCI lililopo katika maonesho ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi yanayofanyika katika Viwanja vya Shule ya Msingi Mji Mwema Mkoani Njombe. Na JKCI ******************************************************************************...