Ziara ya Kujifunza: Viongozi wa Congo wapata huduma za kibingwa za Moyo JKCI
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimpima Shinikizo la damu (BP) Balozi wa Tanzania katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Mhe. Said Juma Mshana alipofika katika Taasisi hiyo leo kwaajili ya kufanya uchunguzi wa afya. Mtaalamu wa Maabara wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Jesca Mlay akimtoa damu Gavana wa jimbo la Maniema Mhe. Mussa Kabwankubi Moise alipofika katika Taasisi hiyo tawi la Oysterbay leo pamoja na ujumbe wa viongozi kutoka jimbo hilo kwaajili ya kufanya uchunguzi wa afya. Mtaalamu wa vipimo vya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Loyce Victor akimpima kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanyakazi (Echocardiograph – ECHO) mjumbe kutoka jimbo la Maniema wakati wajumbe hao walipotembelea JKCI tawi la Oysterbay leo kwaajili ya kufanya uchunguzi wa afya Gavana wa jimbo la Maniema Mhe. Mussa Kabwankubi Moise pamoja na wajumbe kutoka jimbo hilo wakisubiri kupata huduma alipofika katika Taasisi ya Moyo Ja...