Serikali yamuokoa Mama wa Kivule kwa matibabu ya moyo ya shilingi milioni 29 JKCI
Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Zaina Mlingo akimpima shinikizo la damu Mama Anna Mwansasu mkazi wa Kisamvule jijini Dar es Salaam ambaye amefanyiwa upasuaji mdogo wa kupandikiziwa kifaa cha CRT (Cardiac Resynchronization Therapy) ambacho kinausaidia moyo kupiga mapigo yake kwa mpangilio sahihi. Gharama ya matibabu hayo ni zaidi ya shilingi milioni 29 ambapo serikali ya awamu ya sita ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imelipia. ***************************************************************************************************************************************************************************************************** Mkazi wa Kivule jijini Dar es Salaam Mama Anna Mwansasu , ameishukuru Serikali ya awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumsaidia kugharamia matibabu ya kubadilishiwa kifaa cha CRT (Cardiac Resynchronization Therapy) ambacho kinausaidia moyo kupiga mapigo yake kwa mpangilio sahihi...