Gavana wa Mkoa wa Khomas nchini Namibia atembelea JKCI Kliniki ya Kariakoo
Gavana wa Mkoa wa Khomas nchini Namibia Mhe. Sam Shafiishuna Nujoma akitembelea maeneo ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Kliniki ya Kariakoo alipofanya ziara katika Taasisi hiyo leo kuona huduma zinazotolewa. Na JKCI *************************************************************************************************** Gavana wa Mkoa wa Khomas nchini Namibia, Mhe. Sam Shafiishuna Nujoma amefanya ziara katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Kliniki ya Kariakoo kuona huduma zinazotolewa na kuangalia namna wananchi wa jimbo hilo watakavyoweza kupata huduma katika Taasisi hiyo. Ziara hiyo imefanyika leo ambapo Mhe. Nujoma ameweza kuona vifaa vya kisasa vilivyowekezwa na Serikali katika kuboresha huduma bingwa bobezi za matibabu ya moyo nchini Tanzania. Mhe. Nujoma alisema kusogezwa kwa huduma karibu na wananchi ni njia mojawapo ya kuokoa maisha pale inapotokea dharura kama ambavyo JKCI imesogeza huduma hizo katika Soko Kuu la Kariakoo ambalo hutembelewa na wananchi kutoka nchi...