Posts

Mkutano wa CardioTan Imaging 2026 Kujadili Matumizi ya Akili Unde matibabu ya moyo

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na waandishi wa habari leo kuhusu Mkutano wa nne wa Kimataifa wa Magonjwa ya Moyo – CardioTan Imaging 2026 utakaofanyika tarehe 4 hadi 6 mwezi Juni mwaka huu katika ukumbi wa Blue Sapphire Jijini Dar es Salaam.  Mwenyekiti wa Mkutano wa nne wa Kimataifa wa Magonjwa ya Moyo – CardioTan Imaging 2026, Iddi Lemah akizungumza na waandishi wa habari leo kuelekea mkutano huo utakaofanyika tarehe 4 hadi 6 mwezi Juni mwaka huu katika Ukumbi wa Blue Sapphire jijini Dar es Salaam. Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Engerasia Kifai akizungumza na waandishi wa habari kuhusu umuhimu wa Mkutano wa Nne wa Kimataifa wa Magonjwa ya Moyo – CardioTan Imaging 2026 utakaofanyika tarehe 4 hadi 6 mwezi Juni mwaka huu katika Ukumbi wa Blue Sapphire jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Idara ya magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tatizo Waane akiz...

Kampeni ya “Jua Namba Zako” yawafikia Mashabiki wa Arsenal

Image
Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Joyce Kyando akimuonesha shabiki wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Arsenal namba tano za afya zinazohimizwa na Wizara ya afya kuzingatia ili kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza wakati wa tukio la Ongea na Waziri wa Afya lililofanyika katika halfa ya kufurahia ushindi wa Timu ya Arsenal leo katika uwanja wa Posta Kijitonyama jijini Dar es Salaam.  Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Henry Mimbo akimpima sukari kwenye damu shabiki wa Arsenal aliyefika katika banda la JKCI wakati wa tukio la Ongea na Waziri wa Afya lililofanyika katika halfa ya kufurahia ushindi wa Timu ya Arsenal leo katika uwanja wa Posta Kijitonyama jijini Dar es Salaam.  Afisa Utafiti wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Loveness Mfanga akimpima urefu na uzito shabiki wa Arsenal aliyefika katika banda la JKCI wakati wa tukio la Ongea na Waziri wa Afya lililofanyika katika halfa ya kufurahia ushindi wa Timu ya Arsenal leo katika uwanja wa Posta...

JKCI yapongezwa kupambana dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza

Image
Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Edna Kajuna akitoa elimu kuhusu magonjwa ya moyo kwa wanafunzi wa chuo cha KAM College walipotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya Dental Expo 2026 yaliyomalizika leo katika viwanja vya Mlimani City vilivyopo jijini Dar es Salaam. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Edna Kajuna akitoa elimu ya namna ya kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza kwa wananchi waliotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya Dental Expo 2026 yaliyomalizika leo katika viwanja vya Mlimani City vilivyopo jijini Dar es Salaam. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Edna Kajuna akimuonesha jinsi moyo unavyokuwa mwananchi aliyetembelea banda la JKCI wakati wa maonesho ya Dental Expo 2026 yaliyomalizika leo katika viwanja vya Mlimani City vilivyopo jijini Dar es Salaam. Na JKCI ********************************************************************************************************* Washiriki wa maonesho ya ...

JKCI yawataka wananchi kufanya uchunguzi wa afya, kujua namba zao

Image
  Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Edna Kajuna akimuelezea huduma za upasuaji wa moyo zinazotolewa na Taasisi hiyo Rais wa Shirikisho la Vyama vya Kinywa na Meno Duniani (FDI) Prof. Dkt. Nikolai Sharkov alipotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya kimataifa ya vifaa tiba na huduma za kinywa na meno (Dental Expo 2026) yanayofanyika katika viwanja vya Mlimani City Jijini Dar es Salaam. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Edna Kajuna akimuelezea mkazi wa Tabata Mussa Mrisho namna betri ya moyo (Pace maker) inavyofanya kazi alipotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa waonesho ya kimataifa ya vifaa tiba na huduma za kinywa na meno (Dental Expo 2026) yanayofanyika katika viwanja vya Mlimani City Jijini Dar es Salaam. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Edna Kajuna akitoa elimu ya ‘Jua Namba Zako’ kwa baadhi ya washiriki wa waonesho ya kimataifa ya vifaa tiba na huduma za kinywa na meno (Dental Expo 2026) yanayofanyik...

Gavana wa Mkoa wa Khomas nchini Namibia atembelea JKCI Kliniki ya Kariakoo

Image
Gavana wa Mkoa wa Khomas nchini Namibia Mhe. Sam Shafiishuna Nujoma akitembelea maeneo ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Kliniki ya Kariakoo alipofanya ziara katika Taasisi hiyo leo kuona huduma zinazotolewa. Na JKCI *************************************************************************************************** Gavana wa Mkoa wa Khomas nchini Namibia, Mhe. Sam Shafiishuna Nujoma amefanya ziara katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Kliniki ya Kariakoo kuona huduma zinazotolewa na kuangalia namna wananchi wa jimbo hilo watakavyoweza kupata huduma katika Taasisi hiyo. Ziara hiyo imefanyika leo ambapo Mhe. Nujoma ameweza kuona vifaa vya kisasa vilivyowekezwa na Serikali katika kuboresha huduma bingwa bobezi za matibabu ya moyo nchini Tanzania. Mhe. Nujoma alisema kusogezwa kwa huduma karibu na wananchi ni njia mojawapo ya kuokoa maisha pale inapotokea dharura kama ambavyo JKCI imesogeza huduma hizo katika Soko Kuu la Kariakoo ambalo hutembelewa na wananchi kutoka nchi...

Shilingi bilioni 500 zaokolewa matibabu ya moyo kufanyika nchini

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge na Mtendaji Mkuu wa Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Heart Team Africa Foundation (HTAF) Dkt. Naizihijwa Majani wakifurahia wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kitaifa ya kuchangisha fedha kwaajili ya matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo ijulikanayo “Kutoa ni Moyo” leo katika ukumbi wa JKCI iliyopo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na wadau wakati wa hafla fupi ya kuzindua kampeni ya kitaifa ya kuchangisha fedha kwaajili ya matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo ijulikanayo “Kutoa ni Moyo” inayofanywa na Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Heart Team Africa Foundation (HTAF). Mtendaji Mkuu wa Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Heart Team Africa Foundation (HTAF) Dkt. Naizihijwa Majani akitoa taarifa ya fedha zilizokusanywa na Taasisi hiyo kusaidia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wakati wa hafla fupi ya kuzindua kampeni ya ki...

Mhe. Dkt. Kikwete apokea taarifa ya utekelezaji wa fedha za Gala Dinner za matibabu ya moyo kwa watoto

Image
Rais Mstaafu wa awamu ya nne Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge pamoja na Mtendaji Mkuu wa Heart Team Africa Foundation (HTAF) Dkt. Naizihijwa Majani walipomtembelea ofisini kwake hivi karibuni kwa lengo la kumpa taarifa ya utekelezaji wa fedha zilizokusanywa kupitia Gala Dinner ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo. Rais Mstaafu wa awamu ya nne Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge mara baada ya kupokea taarifa ya fedha zilizokusanywa na Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Heart Team Africa Foundation (HTAF) kupitia Gala Dinner ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa JKCI. Mtendaji Mkuu wa Heart Team Africa Foundation (HTAF) Dkt. Naizihijwa Majani akitoa taarifa kwa Rais Mstaafu wa awamu ya nne Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete kuhusu utekelezaji wa fedha zilizoku...