JKCI yawahamasisha Wananchi kujitokeza kupima Afya Kariakoo
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimfanyia kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi mwananchi aliyefika katika kambi maalumu ya upimaji wa afya bila malipo inayofanyika katika kliniki ya Taasisi hiyo iliyopo Soko kuu la Kariakoo ghorofa ya tano. Wananchi wakisubiri kupata huduma ya matibabu ya magonjwa mbalimbali wakati wa kambi maalum ya upimaji wa afya inayofanyika bila malipo katika Tawi la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) lililopo Soko Kuu la Kariakoo ghorofa la tano jiji Dar es Salaam. Daktari wa Afya ya Kinywa na Meno wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dar Group, Joachim Mvungi akitoa elimu ya jinsi ya kupiga mswaki kwa wananchi waliofika katika kambi maalum ya upimaji wa afya bila malipo inayofanyika katika Kliniki ya JKCI Soko Kuu la Kariakoo ghorofa la tano jiji Dar es Salaam. Daktari bingwa wa Macho wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dar Group, Fe...