Watu 303 wapimwa moyo mkoani Manyara
Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Evelyne Furumbe akimpima kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (Echocardiography - ECHO) mtoto wakati wa kambi maalumu ya siku 5 ya uchunguzi na matibabu ya moyo ijulikanayo kama Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tiba mkoba iliyokuwa ikifanywa na wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Manyara (MRRH) na kimalizika hivi karibuni. Mtaalamu wa vipimo vya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Loyce Gideon akimpima kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi mkazi wa Manyara aliyefika katika kambi maalumu ya siku 5 ya uchunguzi na matibabu ya moyo ijulikanayo kama Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tiba mkoba iliyokuwa ikifanywa na wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Manyara (MRRH) na kumalizika hivi karibuni. Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Geofrey Mohammed akiz...