Posts

Kwa mara ya kwanza abiria wanaosafiri na treni ya SGR kunufaika na huduma za uchunguzi wa magonjwa ya moyo

Image
  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo itakayofanywa kwa abiria wanaotumia treni ya SGR katika kuadhimisha siku ya moyo duniani. Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Mhandisi Machibya Shiwa akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo itakayofanywa kwa abiria wanaotumia treni ya SGR katika kuadhimisha siku ya moyo duniani Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akiwa   katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Mhandisi Machibya Shiwa wakati wa uzinduzi wa kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo itakayofanywa kwa abiria wanaotumia treni ya   SGR katika kuadhimisha siku ya moyo duniani. Picha na JKCI ******************************************...

Wahitimu 15 wa mafunzo ya kuhudumia wagonjwa wa dharura kutumia ujuzi walioupata kuokoa maisha

Image
 Mkurugenzi wa upasuaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Angela Muhozya na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Huduma kwa Umma Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Zawadi George wakiwa katika picha ya pamoja na wauguzi waliohitimu mafunzo ya miezi sita ya kuwahudumia wagonjwa wa dharura na mahututi wakati wa hafla fupi ya kuhitimisha mafunzo hayo iliyofanyika katika ukumbi wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Jumla ya wauguzi 15 kutoka nchi za Tanzania, Rwanda na Zambia wamehitimu mafunzo hayo .  Mkurugenzi wa upasuaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Angela Muhozya akimpatia cheti muuguzi ambeye amehitimu mafunzo ya miezi sita ya kuwahudumia wagonjwa wa dharura na mahututi kutoka Hospital ya King Faisal Rwanda Alphonse Nsabimana wakati wa hafla fupi ya kuhitimisha mafunzo hayo iliyofanyika katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Jumla ya wauguzi 15 kutoka nchi za Tanzania, Rwanda na Zambia wamehitimu mafunzo hayo. Mkurugenzi wa upasuaji w...

JKCI yawataka wanamichezo, mashabiki kuchunguza afya ya moyo kuepuka vifo vya ghafla

Image
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo Samuel Rweyemamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group na Makamu wa Rais wa Timu ya Mpira wa Miguu wa Azam FC Abdulkarimu Popat pamoja wakijadili namna wataweza kuboresha ushirikiano baina yao baada ya kutembelea taasisi hiyo jijini Dar es Salaam. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Gudila Swai akimpima mapigo ya moyo Diwani wa Kata ya Vingunguti na Meya Mstaafu wa jiji la Dar es Salaam Mhe. Omar Kumbilamoto aliyefika katika kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya moyo kwa mashabiki wa timu ya mpira wa miguu Azam FC iliyofanyika katika viwanja vya Hospitali hiyo jijini Dar es Salaam Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Helman Nicolaus akimpima kiwango cha sukari kwenye damu shabiki aliyefika katika kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya moyo kwa mashabiki wa timu ya mpira wa miguu wa Azam FC iliyofanyika katika viwanja vya Hospitali hiyo jij...

Watoto 29 wafanyiwa upasuaji wa moyo JKCI

Image
Mkurugenzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Dar Group Dkt. Tulizo Shemu na Balozi wa Saudi Arabia nchini Tanzania, Mhe. Yahya Ahmad wakiwa katika picha ya pamoja na wataalamu kutoka Kituo cha King Salman Humanitarian Aid and Relief Center cha nchini Saud Arabia wakati wa hafla fupi ya kuhitimisha kambi maalumu ya upasuajia wa moyo kwa watoto iliyomalizika jana katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Jumla ya watoto 29 wamefanyiwa upasuaji wa moyo Mkurugenzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Dkt. Tulizo Shemu na Balozi wa Saudi Arabia nchini Tanzania Mhe. Yahya Ahmad wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa JKCI wakati wa hafla fupi ya kuhitimisha kambi maalumu ya upasuajia wa moyo kwa watoto iliyomalizika jana katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Jumla ya watoto 29 wamefanyiwa upasuaji wa moyo   Balozi wa Saudi Arabia nchini Tanzania Mhe. Yahya Ahmad akizungumza wakati wa hafla fupi ya kuhiti...

DC Ubungo, msanii wa mziki G Nako wahamasisha wananchi kujua Namba Zao za Afya

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimpima shinikizo la damu msanii wa Bongo Fleva George Mdemu almaarufu kama G Nako alipofika katika Taasisi hiyo tawi la Oysterbay kwaajili ya kufanya uchunguzi wa afya.  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe. Albert Msando pamoja na msanii wa bongo fleva George Mdemu almaarufu kama G Nako alipofika katika Taasisi hiyo tawi la Oysterbay kwaajili ya kufanya uchunguzi wa afya.  Mtaalamu wa Maabara wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) tawi la Osterbay Jesca Mlay akimtoa damu msanii wa bongo fleva George Mdemu maarufu kama G Nako alipofika katika Taasisi hiyo tawi la Oysterbay kwaajili ya kufanya uchunguzi wa afya.  Picha Na JKCI *************************************************************************************************************************************************************** Mkuu wa Wilaya ya Ubu...

JKCI, King Salman wafanikisha upasuaji wa moyo kwa watoto 16 kwa siku tatu

Image
Mtaalam wa kuendesha mashine ya kusaidia moyo na mapafu kufanya kazi kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Sophia Lukonge akiendesha mashine hiyo wakati wa kambi maalum ya upasuaji wa moyo kwa watoto inayofanywa na wataalam wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao kutoka kituo cha King Salman Humanitarian and Relief cha nchini Saudi Arabia. Wataalam wa upasuaji wa moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa kituo cha King Salman Humanitarian Aid and Relief cha nchini Saudi Arabia wakimfanyia upasuaji wa moyo mtoto mwenye tundu lililopo kwenye moyo wakati wa kambi maalum ya matibabu inayoendelea katika Taasisi hiyo. Jumla ya watoto 30 wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji katika kambi hiyo.             Picha na JKCI ***********************************************************************                                          ...

TPDC Marathon 2026 kuokoa maisha ya watoto 100 wenye magonjwa ya moyo

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Derick Moshi wakati wa uzinduzi wa TPDC Marathon uliofanyika leo katika hoteli ya Johari Rotana iliyopo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa TPDC Marathon kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa JKCI leo katika hoteli ya Johari Rotana iliyopo jijini Dar es Salaam. Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Derick Moshi akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa TPDC Marathon itakayofanyika tarehe 29 Novemba, 2026 katika viwanja vya Polisi Officers Mess iliyopo Masaki kwaajili ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI). Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya K...