Watu 350 wapimwa moyo Muleba
Wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiwa katika picha ya pamoja na wenzao wa Hospital ya Ndolage iliyopo Wilaya ya Muleba Mkoani Kagera wakati wa kambi maalumu ya siku sita ya matibabu ya moyo kwa wananchi wa mkoa huo. **************************************************************************************************************** Watu 350 wamefanyiwa uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kupitia uratibu uliofanywa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (ELCT) Dayosisi ya Kaskazini Magharibi. Upimaji huo umefanyika kwa siku sita katika Hospitali ya Ndolage iliyopo Wilaya ya Muleba mkoani Kagera mwezi Agosti mwaka huu ikiwa ni jitihada zinazofanywa na JKCI kusogeza huduma za kibingwa karibu na wananchi katika ngazi ya Wilaya pamoja kutekeleza Mkataba wa Makubaliano uliosainiwa kati ya JKCI na Hospitali ya Ndolage. Akitoa taarifa ya Kambi hiyo Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwet...