Asilimia 30 ya watu wenye magonjwa yasiyoambukiza wanaotibiwa JKCI hutoka Kanda ya Kaskazini
Daktari wa macho wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete – Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (JKCI – ALMC) John Moteswa akimuonesha Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya GSM Foundation Faith Gugu kifaa maalum kinachotumika kufanya uchunguzi wa macho (Slit Lamp) alipotembelea kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa yasiyoambukiza inayofanyika katika Hospitali ya JKCI-ALMC jijini Arusha. Kaimu Mkurugenzi wa Tiba na Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Dharura wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete – Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (JKCI – ALMC) Peter Mabula akimueleza Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya GSM Foundation Faith Gugu huduma zinazotolewa katika kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa yasiyoambukiza inayofanyika katika Hospitali ya JKCI-ALMC jijini Arusha. Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete – Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (JKCI – ALMC) Veronica Masandika akimpima mapigo ya moyo mwananchi aliyefika kupata huduma ya uchunguzi na matibabu ya magonj...