JKCI yawataka wanamichezo, mashabiki kuchunguza afya ya moyo kuepuka vifo vya ghafla
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo Samuel Rweyemamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group na Makamu wa Rais wa Timu ya Mpira wa Miguu wa Azam FC Abdulkarimu Popat pamoja wakijadili namna wataweza kuboresha ushirikiano baina yao baada ya kutembelea taasisi hiyo jijini Dar es Salaam. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Gudila Swai akimpima mapigo ya moyo Diwani wa Kata ya Vingunguti na Meya Mstaafu wa jiji la Dar es Salaam Mhe. Omar Kumbilamoto aliyefika katika kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya moyo kwa mashabiki wa timu ya mpira wa miguu Azam FC iliyofanyika katika viwanja vya Hospitali hiyo jijini Dar es Salaam Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Helman Nicolaus akimpima kiwango cha sukari kwenye damu shabiki aliyefika katika kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya moyo kwa mashabiki wa timu ya mpira wa miguu wa Azam FC iliyofanyika katika viwanja vya Hospitali hiyo jij...