Benki ya CRDB yachangia shilingi milioni 100 matibabu ya watoto wanaotibiwa JKCI.
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akimkabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni 100 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge leo katika viwanja vya Posta Kijitonyama vilivyopo jijini Dar es Salaam. Hundi hiyo imetolewa na Benki ya CRDB kupitia fedha zilizokusanywa kwa washiriki wa mbio za CRDB msimu wa saba kwaajili ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa JKCI. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akifanya mazoezi ya viongo pamoja na baadhi ya viongozi walioshiriki katika mbio za CRDB msimu wa saba zilizofanyika leo katika viwanja vya Posta Kijitonyama vilivyopo jijini Dar es Salaam. Benki ya CRDB imechangia shilingi milioni 100 matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa JKCI kupitia mbio hizo Baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifurahia mara baada ya kushiriki mbio za CRDB z...