JKCI, King Salman wafanikisha upasuaji wa moyo kwa watoto 16 kwa siku tatu
Mtaalam wa kuendesha mashine ya kusaidia moyo na mapafu kufanya kazi kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Sophia Lukonge akiendesha mashine hiyo wakati wa kambi maalum ya upasuaji wa moyo kwa watoto inayofanywa na wataalam wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao kutoka kituo cha King Salman Humanitarian and Relief cha nchini Saudi Arabia. Wataalam wa upasuaji wa moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa kituo cha King Salman Humanitarian Aid and Relief cha nchini Saudi Arabia wakimfanyia upasuaji wa moyo mtoto mwenye tundu lililopo kwenye moyo wakati wa kambi maalum ya matibabu inayoendelea katika Taasisi hiyo. Jumla ya watoto 30 wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji katika kambi hiyo. Picha na JKCI *********************************************************************** ...