Posts

Watu 350 wapimwa moyo Muleba

Image
Wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiwa katika picha ya pamoja na wenzao wa Hospital ya Ndolage iliyopo Wilaya ya Muleba Mkoani Kagera wakati wa kambi maalumu ya siku sita ya matibabu ya moyo kwa wananchi wa mkoa huo. **************************************************************************************************************** Watu 350 wamefanyiwa uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kupitia uratibu uliofanywa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (ELCT) Dayosisi ya Kaskazini Magharibi. Upimaji huo umefanyika kwa siku sita katika Hospitali ya Ndolage iliyopo Wilaya ya Muleba mkoani Kagera mwezi Agosti mwaka huu ikiwa ni jitihada zinazofanywa na JKCI kusogeza huduma za kibingwa karibu na wananchi katika ngazi ya Wilaya pamoja kutekeleza Mkataba wa Makubaliano uliosainiwa kati ya JKCI na Hospitali ya Ndolage. Akitoa taarifa ya Kambi hiyo Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwet...

Benki ya CRDB yachangia shilingi milioni 100 matibabu ya watoto wanaotibiwa JKCI.

Image
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akimkabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni 100 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge leo katika viwanja vya Posta Kijitonyama vilivyopo jijini Dar es Salaam. Hundi hiyo imetolewa na Benki ya CRDB kupitia fedha zilizokusanywa kwa washiriki wa mbio za CRDB msimu wa saba kwaajili ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa JKCI.  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akifanya mazoezi ya viongo pamoja na baadhi ya viongozi walioshiriki katika mbio za CRDB msimu wa saba zilizofanyika leo katika viwanja vya Posta Kijitonyama vilivyopo jijini Dar es Salaam. Benki ya CRDB imechangia shilingi milioni 100 matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa JKCI kupitia mbio hizo   Baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifurahia mara baada ya kushiriki mbio za CRDB z...

Wafungwa zaidi ya 600 Gereza kuu Ukonga kupimwa moyo

Image
  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza na Mkuu wa Kitengo cha Afya Nsajigwa Mwankenja na baadhi ya askari magereza wa Gereza Kuu Ukonga wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa kambi maalumu ya upimaji na matibabu ya magonjwa ya moyo inayoendelea kwa wafungwa wa Gereza hilo. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kambi maalumu ya upimaji na matibabu ya magonjwa ya moyo inayofanyika kwa wafungwa wa Gereza Kuu Ukonga leo jijini Dar es Salaam.  Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza na Mkuu wa Kitengo cha Afya Nsajigwa Mwankenja akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kambi maalumu ya upimaji na matibabu ya magonjwa ya moyo inayofanyika kwa wafungwa wa Gereza Kuu Ukonga leo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akisaini kitabu cha wageni alipofika k...

Kampuni ya WATU yatoa vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi milioni 11 kwa JKCI

Image
  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akipokea vifaa tiba aina ya Syringe Pump System vyenye thamani ya shilingi milioni 11 kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja kutoka Kampuni ya Mikopo ya Simu na Vyombo vya Moto (WATU) Patricia Sempinge wakati kampuni hiyo ilipochangia mashine hizo   ili kuongeza ufanisi wa huduma kwa wagonjwa wa moyo wanaotibiwa JKCI.  Mkurugenzi wa Idara ya Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Robert Mallya akipokea baadhi ya zawadi kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja kutoka Kampuni ya Mikopo ya Simu na Vyombo vya Moto (WATU) Patricia Sempinge wakati kampuni hiyo ilivyochangia mashine hizo ili kuongeza ufanisi wa huduma kwa wagonjwa wa moyo wanaotibiwa JKCI.  Mfanyakazi wa Kampuni ya Mikopo ya Simu na Vyombo vya Moto (WATU) akimpatia mzazi wa mtoto aliyelazwa katika wodi ya watoto wenye magonjwa ya moyo zawadi wakati wafanyakazi wa kampuni hiyo walipotembelea Ta...

Wanawake wenye matatizo ya kifafa cha mimba epukeni kubadilisha wenza: Dkt. Raya

Image
  Daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake na wajawazito wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Raya Chambali akitoa elimu kuhusu magojwa ya wanawake kwa wagonjwa wanaopata huduma katika Hospitali hiyo iliyopo Temeke jijini Dar es Salaam.  Daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake na wajawazito wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Raya Chambali akiandika taarifa za mgonjwa aliyefika kupata huduma katika hospitali hiyo iliyopo Temeke jijini Dar es Salaam.  *************************************************************************************                                        *************************************** Na JKCI Wanawake wenye matatizo ya kupata kifafa cha mimba wakati wa ujauzito wameshauriwa kutobadilisha mwenza baada ya kujifunga mtoto wa kwanza ili kuepuka vifo vinavyotokana na ugonjwa huo. Rai hiyo imetolewa...

Benki ya NBC kuchangia kiasi cha shilingi bilioni 1 matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo

Image
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba akimkabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni 200 Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi  wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Naizihijwa Majani kwaajili ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa JKCI iliyotolewa na Benki ya NBC kupitia mbio za NBC zilizofanyika jana jijini Dodoma. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba akisalimiana na Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Naizihijwa wakati wa mbio za NBC zilizofanyika jana katika  uwanja wa michezo Jamhuri uliopo jijini Dodoma.   Mjumbe wa bodi ya wadhamini wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Kassim Hussein akishiriki katika mazoezi ya viungo wakati wa mbio za NBC zilizofanyika jana katika uwanja wa michezo Jamhuri uliopo jijini Dodoma kwaajili ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa JKCI.  Wafanyakazi wa Taasis...

Watu 1,089 wamefanyiwa uchunguzi wa magonjwa ya moyo kambi maalumu ya Mhe. Makonda

Image
Wananchi kutoka mikoa mbalimbali ya Kaskazini wakiwa katika foleni ya kupata huduma za uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo wakati wa kambi maalumu ya kupima na kutibu magonjwa ya binadamu iliyoandaliwa na Ofisi ya Mbunge wa Arusha mjini Mhe. Paul Makonda na kufanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha. Jumla ya watu 1,089 wamepimwa moyo. Daktari wa Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) ambayo inasimamiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Adda Justine akimpatia maelekezo mwananchi aliyefika kufanya uchunguzi wa afya wakati wa kambi maalumu ya kupima na kutibu magonjwa ya binadamu iliyoandaliwa na Ofisi ya Mbunge wa Arusha mjini Mhe. Paul Makonda na kufanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha. Jumla ya watu 1,089 wamepimwa moyo. Mbunge wa jimbo la Arusha mjini Mhe. Paul Makonda akizungumza na wananchi waliokuwa wakisubiri kupata huduma katika banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa kambi maalumu ya kupima na kutibu m...