JKCI-ALMC na GSM Foundation wapongezwa kuendesha kambi ya matibabu mkoani Arusha
Fundi sanifu wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete – Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (JKCI – ALMC) Rosemary Leonard akimpima kipimo cha kuangalia jinsi mfumo wa umeme wa moyo unavyofanya kazi (Electrocardiography – ECG) mkazi wa Arusha aliyefika katika kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa yasiyoambukiza inayofanyika katika Hospitali ya JKCI-ALMC iliyopo jijini Arusha. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete – Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (JKCI - ALMC) Fabian Bura akimpima shinikizo la damu mkazi wa Arusha aliyefika katika kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa yasiyoambukiza inayofanyika katika Hospitali ya JKCI-ALMC iliyopo jijini Arusha. Daktari wa macho wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete – Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (JKCI - ALMC) Wilen Wilson akimpima kipimo cha miwani mkazi wa Arusha aliyefika katika kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa yasiyoambukiza inayofanyika katika Hospitali ya JKCI-...