Posts

Huduma za kibingwa za Moyo zawafikia wakazi wa Njombe

Image
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Njombe Dkt. Juma Mfanga akizungumza na Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group walioko Mkoani Njombe wanaotoa huduma za uchunguzi na matibabu ya magonjwa mbalimbali kwenye maonesho ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi yanayofanyika katika Viwanja vya Shule ya Msingi Mji Mwema vilivyopo mkoani humo. Daktari bingwa wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Moses Manumbu akimsikiliza mwananchi aliyefika katika banda la JKCI Hospitali ya Dar Group kwaajili ya kupata huduma za uchunguzi na matibabu ya magonjwa mbalimbali zinazotolewa na taasisi hiyo katika maonesho ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi yanayofanyika katika Viwanja vya Shule ya Msingi Mji Mwema vilivyopo mjini Njombe. Wananchi wakipata huduma za uchunguzi na matibabu ya magonjwa mbalimbali katika banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group wakati wa maonesho ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi yanayofanyika katika Viwanja vya Shule ya Msingi Mji Mwema...

JKCI yawajengea uwezo viongozi katika usimamizi wa vihatarishi kwaajili ya ufanisi wa malengo

  Menejimenti ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)   inahudhuria mafunzo maalumu ya siku mbili yanayolenga   kuwajengea uwezo wa kutambua na kudhibiti vihatarishi vinavyoweza kujitokeza na kuathiri taasisi hiyo katika utoaji wa huduma bora kwa wagonjwa wanaowahudumia. Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Dkt. Peter Kisenge   wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo Mkuu wa Kitengo cha Sheria Adv.   Maulid Kikondo alisema ni takwa la kisheria kwa taasisi za umma na binafsi kuwajengea uwezo viongozi wake ili waweze kutambua na kudhibiti hatari katika maeneo yao ya kazi sambamba na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi. Adv. Kikondo alisema mafunzo hayo ni muhimu kwa viongozi katika kulinda taasisi dhidi ya vihatarishi vinavyoweza kujitokeza ili waweze kufahamu mbinu bora za kukabiliana navyo na kuepusha usumbufu au kusitishwa kwa huduma za afya kwa wananchi. “Taasisi inapokuwa na viongozi wenye uelewa wa kutosha kuhusu usimamizi wa h...

Jamii yahimizwa kutambua vihatarishi vya magonjwa ya moyo mapema

Image
Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Rafael Kwileka akimsomea majibu mwananchi aliyefika katika kambi maalumu ya uchunguzi wa afya ya siku tatu inayofanywa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Jumuiya ya Wafanyabiashara Kariakoo katika kliniki ya JKCI iliyopo Kariakoo jijini Dar es Salaam.  Mhudumu wa Afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Halima Shaban akimpima uwiano wa urefu na uzito mwananchi aliyejitokeza kufanya uchunguzi wa afya wakati wa kambi maalumu ya siku tatu ya uchunguzi wa afya inayofanywa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Jumuiya ya Wafanyabiashara Kariakoo katika kliniki ya JKCI iliyopo Kariakoo jijini Dar es Salaam.  Mtunza kumbukumbu za afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Emiliana Roshy akimsajiri mwananchi aliyejitokeza kufanya uchunguzi wa afya wakati wa kambi maalumu ya siku tatu ya uchunguzi wa afya inayofanywa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Jumu...

Kutoka miaka 22 hadi kustaafu: Safari ya Lemmah yatoa somo kwa Watumishi wa Umma

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimkabidhi mfano wa hundi ya zawadi ya kustaafu  aliyekuwa Mkuu wa Kitengo cha Ununuzi na Ugavi JKCI Dar Group Iddi Lemmah wakati wa hafla fupi ya kumuaga iliyofanyika jana katika ukumbi wa Taasisi ya hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasiliamali Watu wa JKCI, Ghati Chacha. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimkabidhi tuzo ya shukrani kutokana na mchango wake alioutoa katika taasisi hiyo aliyekuwa Mkuu wa Kitengo cha Ununuzi na Ugavi JKCI Dar Group Iddi Lemmah ambaye amestaafu kwa mujibu wa sheria wakati wa hafla fupi ya kumuaga iliyofanyika jana katika ukumbi wa Taasisi ya hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasiliamali Watu wa JKCI  Ghati Chacha. Mkurugenzi wa Utawala na Rasiliamali Watu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Ghati Chacha akimkabidhi cheti cha shukrani kutokan...

JKCI yaimarisha ufanisi kwa mafunzo ya Usalama na Afya kwa wafanyakazi

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akiwaeleza wafanyakazi wa Taasisi hiyo umuhimu wa kuzingatia usalama wa wagonjwa wanaowahudumia pamoja na wao wenyewe wakati wa mafunzo ya umuhimu wa fidia kwa wafanyakazi na usalama mahali pa kazi yaliyofanyika leo jijini Dar es Salaam. Afisa Mkaguzi Mazingira ya Kazi kutoka Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) Simon Lwaho akitoa elimu kuhusu usalama wa wafanyakazi mahala pa kazi kwa wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI). Afisa Matekelezo kutoka Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Calvin Urassa akitoa elimu na kuainisha aina za fidia zinazotolewa na mfuko huo kwa wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) yaliyotolewa leo katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifuatilia mafunzo ya usalama na afya mahala pa kazi yaliyokuwa yakitolewa na mtaalamu kutoka (OSHA) pamoja na mafunzo ya umu...

Utafiti JKCI wachambua uhusiano kati ya dawa za moyo za SGLT2i na Afya ya njia ya mkojo

Image
Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Samueli Rweyemamu akimpima kipimo cha kuangali jinsi moyo unavyofanya kazi mkazi wa Kitunda. ****************************************************************************************************************** Utafiti mpya uliofanyika katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) jijini Dar es Salaam umebaini kuwepo kwa ongezeko la maambukizi ya njia ya mkojo (UTI) miongoni mwa wagonjwa wa moyo wanaotumia dawa aina ya Sodium-Glucose Co-Transporter 2 Inhibitors (SGLT2i) zikiwemo dapagliflozin na empagliflozin. Dawa hizo ambazo zimekuwa msaada mkubwa katika matibabu ya magonjwa ya moyo na figo sasa zinaibua mjadala mpya kufuatia kuhusishwa na hatari ya kuongezeka kwa maambukizi ya UTI kwa baadhi ya wagonjwa. Utafiti huo uliofanywa na Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa JKCI Dar Group Samueli Rweyemamu kwa kushirikiana na wataalamu wenzake na kuchapishwa katika Jarida la PLOS ONE la nc...

Msaada wa Rais Samia wamfungulia milango ya matibabu: Mtoto mwenye tatizo la Moyo aanza safari JKCI

Image
 Wataalamu wa upasuaji wa Moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifanya upasuaji wa kuziba tundu la moyo wa mtoto. ***************************************************************************************************************************************************************************************************** Mtoto Selina Daudi anayekabiliwa na changamoto ya tundu kwenye moyo ameanza rasmi safari ya matibabu katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kufuatia kupatiwa msaada wa kifedha na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. Selina anayeishi na mama yake Aisha Said katika eneo la Chanika jijini Dar es Salaam anatarajiwa kupata huduma za kibingwa zitakazomsaidia kurejea katika hali yake ya kawaida kiafya. Akizungumzia hatua hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Peter Kisenge alisema msaada uliotolewa na Mhe. Rais Dkt. Samia umefungua ukurasa mpya wa matumaini kwa mtoto huyo huku gharama za matibabu zikifikia zaidi ya shil...