Dkt. Kisenge: Waandishi wa habari tumieni kalamu zenu kuhamasisha jamii kujua namba zao za afya
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na waandishi wa habari kuhusu miradi ya maendeleo inayofanywa na Taasisi hiyo wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika leo katika Ukumbi wa Idara ya Habari - MAELEZO ulipo Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Jijini Dodoma. Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia hotuba iliyokuwa ikitolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge wakati wa mkutano na waandishi hao uliofanyika leo katika Ukumbi wa Idara ya Habari - MAELEZO ulipo Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Jijini Dodoma. Na JKCI *************************************************************************************************** Waandishi wa habari nchini wametakiwa kutumia kalamu zao na kushirikiana na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kuihamasisha jamii kujua namba zao za afya ili iweze kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza kujenga taifa imara na lenye afya b...