JKCI yaweka kambi ya matibabu Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Dodoma
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejmenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Juma Mkomi akizungumza na Maafisa kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) alipotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyoanza leo jijini Dodoma. Afisa Utafiti wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Makrina Komba akimpima uwiano wa urefu kwa uzito Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejmenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Juma Mkomi alipotembelea banda la Taasisi hiyo lililopo katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma. Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Daud Gwilenza akimsikiliza mwananchi aliyetembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika Viwanja vya Chinangali jijini Dodoma. Na JKCI ******************************************************************************************************* Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) yafikisha Kampeni y...