Zaidi ya watu 150 wabainika na matatizo ya Moyo katika kambi ya uchunguzi Njombe
Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mahawa Asenga akimpima shinikizo la damu na mapigo ya moyo mwananchi aliyefika katika banda la JKCI Dar Group kwaajili ya kufanya uchunguzi wa afya wakati wa maonesho ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi yaliyomalizika hivi karibuni Mkoani Njombe. Jumla ya watu 386 wamefanyiwa uchunguzi wa afya katika maonesho hayo. Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Happiness Shirima akitoa elimu ya mtindo bora wa maisha kujilinda na magonjwa ya moyo kwa wananchi wa Mkoa wa Njombe waliofika katika banda la JKCI Dar Group kwaajili ya kufanya uchunguzi wa afya wakati wa maonesho ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi yaliyomalizika hivi karibuni Mkoani Njombe. Jumla ya watu 386 wamefanyiwa uchunguzi wa afya katika maonesho hayo. Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Moses Manumbu akisikiliza mapigo ya moyo ya mwananchi aliyefika katika banda la JK...