TAKUKURU yachangia milioni 20.89 matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akipokea hundi ya shilingi milioni 20.89 kutoka kwa Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Ilala Faustine Maijo kwaajili ya kusaidia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza wakati wa hafla fupi ya kupokea hundi ya shilingi milioni 20.89 kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwajili ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Ilala Faustine Maijo akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi hundi ya shilingi milioni 20.89 kwaajili ya kuwasaidia watoto wenye magonjwa ya moyo wanao...