Mapinduzi sekta ya Afya: JKCI yaleta teknolojia ya Roboti ya bilioni 5.5
Mtaalamu wa Maabara wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mariam Steven akiangalia hatua za upimaji wa sampuli za damu zinavyofanyika katika maabara ya kisasa ya taasisi hiyo inayotumia teknolojia ya roboti. Mtaalamu wa Maabara wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Glory Mtui akiiruhusu roboti kuendelea na upimaji wa sampuli za damu kwa kutumia teknolojia ya roboti inayotumika katika maabara ya kisasa ya taasisi hiyo. Mtaalamu wa Maabara wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Glory Mtui akipanga sampuli za damu tayari kwa upimaji kwa kutumia teknolojia ya roboti inayotumika katika maabara ya kisasa ya taasisi hiyo. ************************************************************************************************************************************************************************************************************************ Sekta ya afya nchini imepiga hatua kubwa kufuatia Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kuanza kutumia maabara ya kisasa yenye teknolojia y...