Serikali kufungua tawi la JKCI – Chato
Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu akiingia bungeni leo jijini Dodoma kwaajili ya kuwasilisha hotuba ya makadirio ya bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha wa 2024/25. Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu na Naibu Waziri wa Afya Mhe. Dkt. Godwin Mollel wakiwa wameshika hotuba ya makadirio ya bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha wa 2024/25 kabla haijasoma leo bungeni jijini Dodoma. ************************************************************************************************************************************************************************************** Serikali imepanga kufungua tawi la Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Kanda ya Ziwa katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Chato (JKCI- Chato) iliyopo mkoani Geita. Hayo yamesemwa leo bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu wakati akiwasilisha hotuba ya makadirio ya bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha wa 2024/25. Katika kutekeleza hilo Wizara ya Afya moja ya vipaumbele vyake kwa mwaka wa fedha wa 2