Serikali yagharamia milioni 758 matibabu ya Wagonjwa wa Moyo
Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Stella Mongela akimpima mtoto kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (Echocardiography - ECHO) ******************************************************************************************************************* Serikali imegharamia jumla ya shilingi milioni 758,178,091 kwa ajili ya matibabu ya wagonjwa wa moyo wasiokuwa na uwezo wa kulipia huduma hizo pamoja na kusamehe gharama za miili ya marehemu waliokuwa wakipatiwa matibabu katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI). Akizungumza na mwandishi wa habari hii jijini Dar es Salaam kuhusu siku 100 za utekelezaji wa ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kugharamia matibabu ya kibingwa kwa wagonjwa wa moyo wasiokuwa na uwezo, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Dkt. Peter Kisenge, alisema serikali ya awamu ya sita imeendelea kuweka mkazo katika kuwasaidia wananchi wenye uhitaji ...