Watu 253 wafanyiwa uchunguzi wa afya mkutano wa e-GA
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akimpatia tuzo Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi wa Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) ambayo kwa sasa inasimamiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Salehe Mwinchete kutambua na kuthamini mchango wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa kufunga kikao kazi cha sita cha Serikali Mtandao kilichofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Arusha (AICC) jijini Arusha. Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Sahiya Yahya akimsikiliza mmoja wa wafanyakazi aliyepata huduma wakati wa kambi maalumu ya siku tatu ya uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha sita cha Serikali Mtandano kilichofanyika katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Arusha (AICC) jijini Arusha. Mtaalamu wa vipimo vya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Beatrice Mwakabende akimpima mmoja wa wafanyakazi aliyefika katika kambi maalumu ya siku tatu ya uch...