UFAFANUZI KUHUSU TAARIFA ZA MGONJWA ZINAZOSAMBAA MTANDAONI
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) inapenda kutoa ufafanuzi kuhusu taarifa za mgonjwa zinazosambaa mtandaoni kuhusu matibabu aliyokuwa akipatiwa katika Taasisi yetu. Mgonjwa huyo alipokelewa JKCI tarehe 25 Mei 2026 akiwa na matatizo makubwa ya moyo yaliyosababisha moyo kushindwa kufanya kazi kama inavyotakiwa. Mara baada ya kulazwa, alipatiwa matibabu ya kina kwa lengo la kuimarisha hali yake ili aweze kuendelea na hatua nyingine za matibabu ikiwemo upasuaji wa moyo. Katika kipindi cha matibabu jopo la wataalamu wakiwemo madaktari bingwa wa upasuaji wa moyo walikutana na mgonjwa pamoja na ndugu zake kuwaeleza kwa kina hali ya mgonjwa na hatari zilizokuwepo. Wataalamu walieleza kuwa kufanya upasuaji katika kipindi hicho kungeweza kuhatarisha zaidi maisha yake kutokana na hali yake kuwa dhaifu hivyo ilikubaliwa aendelee na matibabu ya kuimarisha afya yake. Licha ya juhudi kubwa zilizofanywa na wataalamu wetu na matibabu yote aliyokuwa akipatiwa hali ya mgonjwa...