Posts

Showing posts from May, 2026

Dkt. Kisenge awapongeza Wafanyakazi JKCI, Asisitiza ufanisi na weledi kazini

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimkabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni tano Mfanyakazi Hodari wa taasisi hiyo kwa mwaka wa fedha wa 2025/2026 Afisa Tawala Adila Musa wakati wa hafla ya kuwatambua na kuwapongeza wafanyakazi Hodari iliyofanyika jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimkabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni mbili Mfanyakazi Hodari wa taasisi hiyo nafasi ya pili kwa mwaka wa fedha wa 2025/2026 Mkaguzi wa Hesabu za Ndani Sitty Hamis wakati wa hafla ya kuwatambua     na kuwapongeza wafanyakazi Hodari iliyofanyika jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimkabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni moja na nusu Mfanyakazi Hodari wa taasisi hiyo nafasi ya tatu kwa mwaka wa fedha wa 2025/2026 Afisa Muuguzi Edna Kajuna wakati wa hafla ya kuwatambua na kuwapongeza wafanyakazi hodari ili...

JKCI na TBS waungana kuboresha Afya ya Wafanyakazi kupitia upimaji wa Moyo

Image
Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Agnes Kajangwa akimpima kiwango cha sukari kwenye damu Mkurugenzi wa Uandaaji Viwango wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) David Ndibalema Lugome wakati wa kambi maalumu ya upimaji wa magonjwa ya moyo iliyolenga kuongeza uelewa kuhusu magonjwa hayo na njia za kujikinga ili kuboresha afya na ufanisi kazini kwa wafanyazi wa shirika hilo. Jumla ya Wafanyakazi 68 walipata huduma ambapo nane kati yao walipewa rufaa ya kwenda kutibiwa katika Tawi la JKCI Oysterbay. Afisa Masoko wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Agness Mndasha akimkabidhi vipeperushi vya taasisi hiyo Afisa Utumishi Mwandamizi wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Mariam Mbarouk wakati wa kambi maalumu ya upimaji wa magonjwa ya moyo iliyolenga kuongeza uelewa kuhusu magonjwa hayo na njia za kujikinga ili kuboresha afya na ufanisi kazini kwa wafanyazi wa shirika hilo. Jumla ya Wafanyakazi 68 walipata huduma ambapo nane kati yao walipewa rufaa ya kwenda ku...