Mhe. Dkt. Kikwete apokea taarifa ya utekelezaji wa fedha za Gala Dinner za matibabu ya moyo kwa watoto
Rais Mstaafu wa awamu
ya nne Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge mara baada ya kupokea
taarifa ya fedha zilizokusanywa na Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Heart Team
Africa Foundation (HTAF) kupitia Gala Dinner ya kuchangia matibabu ya watoto
wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa JKCI.
Mtendaji Mkuu wa Heart
Team Africa Foundation (HTAF) Dkt. Naizihijwa Majani akitoa taarifa kwa Rais
Mstaafu wa awamu ya nne Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete kuhusu utekelezaji wa fedha
zilizokusanywa kupitia Gala Dinner ya kuchangia matibabu ya watoto wenye
magonjwa ya moyo iliyoandaliwa na HTAF.
Rais Mstaafu wa awamu
ya nne Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge alipomtembelea ofisini
kwake hivi karibuni kwaajili ya kumpa taarifa ya utekelezaji wa fedha
zilizokusanywa na Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Heart Team Africa Foundation
(HTAF) kupitia Gala Dinner ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya
moyo wanaotibiwa JKCI.
Na JKCI
**********************************************************************************************************
Comments
Post a Comment