JKCI yawataka wananchi kufanya uchunguzi wa afya, kujua namba zao

 

Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Edna Kajuna akimuelezea huduma za upasuaji wa moyo zinazotolewa na Taasisi hiyo Rais wa Shirikisho la Vyama vya Kinywa na Meno Duniani (FDI) Prof. Dkt. Nikolai Sharkov alipotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya kimataifa ya vifaa tiba na huduma za kinywa na meno (Dental Expo 2026) yanayofanyika katika viwanja vya Mlimani City Jijini Dar es Salaam.

Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Edna Kajuna akimuelezea mkazi wa Tabata Mussa Mrisho namna betri ya moyo (Pace maker) inavyofanya kazi alipotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa waonesho ya kimataifa ya vifaa tiba na huduma za kinywa na meno (Dental Expo 2026) yanayofanyika katika viwanja vya Mlimani City Jijini Dar es Salaam.

Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Edna Kajuna akitoa elimu ya ‘Jua Namba Zako’ kwa baadhi ya washiriki wa waonesho ya kimataifa ya vifaa tiba na huduma za kinywa na meno (Dental Expo 2026) yanayofanyika katika viwanja vya Mlimani City Jijini Dar es Salaam.


Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Edna Kajuna akimuonesha moja ya kifaa kinachotumika kuzibua mishipa ya moyo (Stent) Afisa Uhusiano na Masoko wa Prime your digital partner Eliwaja Peter alipotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya kimataifa ya vifaa tiba na huduma za kinywa na meno (Dental Expo 2026) yanayofanyika katika viwanja vya Mlimani City Jijini Dar es Salaam.

Na JKCI

*********************************************************************************************************

Wananchi wametakiwa kufanya uchunguzi wa afya mara kwa mara kufahamu hali zao kiafya ili waweze kuepukana na vifo vya gafla vinavyoendelea kukijitokeza katika jamii.

Hayo yalisemwa na Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Edna Kajuna wakati wa maonesho ya Dental Expo yanayofanyika katika viwanja vya Mlimani City jijini Dar es Salaam.

Edna alisema kutokana na ongezeko kubwa la magonjwa yasiyoambukiza JKCI imeanzisha kampeni ya “Jua Namba Zako” yenye lengo la kuwasaidia wananchi kufahamu viwango muhimu vya afya vinavyoonesha namna miili yao inavyofanya kazi.

“Tunaposema Jua Namba Zako tunamaanisha mwananchi anatakiwa kufahamu shinikizo la damu ambalo linapaswa kuwa 120/80, mapigo ya moyo 60 hadi 100 kwa dakika, kiwango cha sukari kwenye damu 5.2, Uwiano wa uzito na urefu (BMI) pamoja na kiwango cha mafuta kwenye damu”, alisema Edna.

Akizungumzia uhusiano uliopo kati ya magonjwa ya moyo na afya ya kinywa na meno Edna alisema ni muhimu kwa wagonjwa wa moyo kulinda afya ya kinywa ambayo mara nyingi uwasaidia wagonjwa kupona haraka wanapofanyiwa upasuaji wa moyo.

“Maonesho haya ni muhimu kwetu kama JKCI kwani mgonjwa anayetarajia kufanyiwa upasuaji wa moyo lazima afanyiwe uchunguzi wa afya ya kinywa kabla ya upasuaji kwasababu bakteria wanaoshambulia meno wanaweza kuhatarisha maisha yake”, alisema Edna.

Kwa upande wao wananchi waliofika katika banda la JKCI waliishukuru Taasisi hiyo kwa kutoa elimu ya namna ya kujikinga na magonjwa yasiombukiza kwani wamepata nafasi ya kuelewa kwa kina umuhimu wa kujua namba zao tano za afya.

“Sisi vijana wa rika hili ambalo tunatambulika kama Gez tumepata nafasi ya kuzifahamu namba hizi tano za afya, kupitia elimu hii tutachukua tahadhari ili kuishi maisha marefu”, alisema Eliwaja Peter Afisa Uhusiano na Mawasiliano kutoka Prime.

“Nimefika katika banda la JKCI na kufaidika na elimu inayotolewa kuhusu uhusiano wa afya ya kinywa na magonjwa ya moyo, leo nimeweza kupata uelewa kuwa yapo magonjwa ya moyo yanayoweza kusababishwa na magonjwa ya kinywa endapo hayatatibiwa na kupona”, alisema Mussa Mrisho Mkazi wa Tabata Bima.


 

 

Comments

Popular posts from this blog

Kutoka miaka 22 hadi kustaafu: Safari ya Lemmah yatoa somo kwa Watumishi wa Umma

Wanawake waaswa kulinda mioyo yao, kuepuka sukari na chumvi kupita kiasi