Gavana wa Mkoa wa Khomas nchini Namibia atembelea JKCI Kliniki ya Kariakoo
Na JKCI
***************************************************************************************************
Gavana wa Mkoa wa Khomas nchini Namibia, Mhe. Sam Shafiishuna
Nujoma amefanya ziara katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Kliniki ya Kariakoo
kuona huduma zinazotolewa na kuangalia namna wananchi wa jimbo hilo
watakavyoweza kupata huduma katika Taasisi hiyo.
Ziara hiyo imefanyika leo ambapo Mhe. Nujoma ameweza kuona vifaa vya kisasa vilivyowekezwa na Serikali katika kuboresha huduma bingwa bobezi za matibabu ya moyo nchini Tanzania.
Mhe. Nujoma alisema kusogezwa kwa huduma karibu na wananchi ni njia mojawapo ya
kuokoa maisha pale inapotokea dharura kama ambavyo JKCI imesogeza huduma hizo katika
Soko Kuu la Kariakoo ambalo hutembelewa na wananchi kutoka nchi mbalimbali.
Rajabu alisema tangu kuanzishwa kwa tawi hilo idadi ya watu wanaotembelea katika kliniki hiyo imekuwa ikiongezeka na kupunguza hadha ya wafanyabiashara kufuata huduma za afya mbali na eneo la biashara.

Comments
Post a Comment