Kampeni ya “Jua Namba Zako” yawafikia Mashabiki wa Arsenal

Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Joyce Kyando akimuonesha shabiki wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Arsenal namba tano za afya zinazohimizwa na Wizara ya afya kuzingatia ili kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza wakati wa tukio la Ongea na Waziri wa Afya lililofanyika katika halfa ya kufurahia ushindi wa Timu ya Arsenal leo katika uwanja wa Posta Kijitonyama jijini Dar es Salaam. 

Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Henry Mimbo akimpima sukari kwenye damu shabiki wa Arsenal aliyefika katika banda la JKCI wakati wa tukio la Ongea na Waziri wa Afya lililofanyika katika halfa ya kufurahia ushindi wa Timu ya Arsenal leo katika uwanja wa Posta Kijitonyama jijini Dar es Salaam. 

Afisa Utafiti wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Loveness Mfanga akimpima urefu na uzito shabiki wa Arsenal aliyefika katika banda la JKCI wakati wa tukio la Ongea na Waziri wa Afya lililofanyika katika halfa ya kufurahia ushindi wa Timu ya Arsenal leo katika uwanja wa Posta Kijitonyama jijini Dar es Salaam.

Na JKCI

********************************************************************************************************

Mashabiki wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Arsenal wapata elimu kuhusu magonjwa yasiyoambukiza na kuzijua namba zao za afya wakati wa hafla ya kusherehekea ushindi wa timu hiyo iliyofanyika leo katika viwanja vya Posta Kijitonyama jijini Dar es Salaam.

Hafla hiyo imefanyika sambamba na tukio la Ongea na Waziri wa Afya kutoa motisha kwa mashabiki hao kufanyiwa uchunguzi wa afya, kuhamasisha kampeni ya Jua Namba Zako na kuikumbusha jamii kuwa na mtindo bora wa maisha.

Akizungumza wakati wa halfa hiyo Daktari kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Joyce Kyando alisema JKCI itaendelea kuihamasisha jamii kuzifahamu namba zao za afya na kujenga tabia ya kufanya uchunguzi wa afya mara kwa mara.

“Tunaamini mashabiki hawa wa Arsenal wakishazijua namba zao kupitia hafla hii watajenga tabia ya kupima afya mara kwa mara na kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza yakiwemo ya moyo”,

“Unaweza kumuona mtu anafanya mazoezi kila siku lakini bado akawa na mafuta mengi kwenye damu, hivyo tusiangalie muonekano wa nje tukajiona salama, tupende kufanya uchunguzi wa afya”, alisema Dkt. Joyce

Kwa upande wao mashabiki wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Arsenal walioshiriki hafla hiyo wameishukuru Wizara ya Afya kuiwezesha JKCI kufikisha huduma za uchunguzi wa afya kwa mashabiki hao.

Da hope shabiki wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Arsenal alisema wakati mashabiki wa timu hiyo wanapata burudani pia wamepata nafasi ya kufanya uchunguzi wa afya na ushauri kutoka kwa wataalamu mabingwa wa magonjwa ya moyo.

Naye Gideon Rwegelela shabiki wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Arsenal alisema kupitia hafla hiyo watanzania wengi wataelimika na kuzifahamu namba zao ambazo Wizara ya Afya imekuwa ikihimiza jamii kuzijua na kuchukua hatua.

 

Comments

Popular posts from this blog

Serikali yazindua kitabu safari ya upandikizaji wa moyo Tanzania, JKCI yaweka historia mpya ya huduma za kibobezi

Kutoka miaka 22 hadi kustaafu: Safari ya Lemmah yatoa somo kwa Watumishi wa Umma