Serikali yazindua kitabu safari ya upandikizaji wa moyo Tanzania, JKCI yaweka historia mpya ya huduma za kibobezi
Waziri wa Afya Mhe.
Mohamed Omary Mchengerwa (Mb) akionesha kitabu cha mwongozo wa upandikizaji
moyo alichokizindua wakati wa hafla fupi ya kuzindua kitabu hicho iliyofanyika
katika viwanja vya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo jijini Dar es
Salaam.
Waziri wa Afya Mhe.
Mohamed Mchengerwa (Mb) akimkabidhi begi lenye vitendea kazi Mwenyekiti wa bodi
ya wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Hassan Mshinda baada
ya kuzindua bodi hiyo katika viwanja vya JKCI iliyopo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Afya Mhe.
Mohamed Mchengerwa (Mb) akimkabidhi begi lenye vitendea kazi Mjumbe wa bodi ya
wadhamini wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delilah Kimambo baada
ya kuzindua bodi hiyo katika viwanja vya JKCI iliyopo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Afya Mhe.
Mohamed Mchengerwa (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge, Mwenyekiti wa bodi ya
wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Hassan Mshinda na wajumbe wa bodi hiyo mara baada ya kuizindua
bodi hiyo katika viwanja vya JKCI iliyopo Jijini Dar es Salaam.
Na JKCI
************************************************************************************************************
Katika kuhakikisha wananchi wanaendelea kupata huduma za kibingwa bobezi nchini, Serikali kupitia Wizara ya Afya imezindua kitabu cha safari ya upandikizaji wa moyo nchini kuwasaidia wagonjwa ambao wanahitaji huduma hiyo.
Akizungumza wakati wa
uzinduzi wa kitabu hicho jijini Dar es Salaam Waziri wa Afya Mhe. Mohamed
Mchengerwa alisema Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais Dkt.
Samia Suluhu Hassan inaendelea kuimarisha Sekta ya Afya kwa kutoa huduma za kibingwa
bobezi katika matibabu moyo nchini.
“Niwapongeze JKCI kwa mpango
huu ambao unaashiria hatua kubwa katika kutoa huduma kwa wagonjwa wa moyo katika
ngazi ya kitaifa na kimataifa, kwasababu huduma hii ni kubwa sasa ni wakati
wakuanza kuweka miundmbinu bora, mifumo ya kisheria pamoja na ushirikiano wa
kimataifa”, alisema Mhe. Mchengerwa.
Kwa upande wake
Mwenyekiti wa Kamati ya upandikizaji wa moyo nchini kutoka Taasisi ya Moyo
Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Everist Nyawawa alisema watu milioni 64 duniani
wenye matatizo ya moyo wanahitaji kupandikiziwa moyo ili waweze kuendelea
kuishi.
Dkt. Nyawawa ambaye pia
ni daktari bingwa wa upasuaji wa moyo alisema uhitaji wa kupandikiza mayo kwa
wagonjwa wanaohitaji hudua hiyo inatokana na hatua za matibabu kwa wagonjwa
wenye tatizo la moyo kushindwa kufanya kazi (Heart Failure) ambao hulazimika
kupatiwa matibabu ya muda mrefu na kutumia dawa mara kwa mara.
“JKCI tumeamua
kuthubutu mambo yanayoonekana kuwa magumu ambayo yatawezekana kufanyika nchini
ili kuokoa maisha ya watu wengi, hatua hii muhimu italisaidia taifa kupunguza
gharama za kuwapeleka wagonjwa wanaohitaji kupandikiza moyo nje ya nchi”,
alisema Dkt. Nyawawa.
Dkt. Nyawawa alisema
ili kufanikisha safari ya upandikizaji wa moyo nchini jamii inatakiwa kupewa
elimu ya kutosha kuhusu huduma hiyo pamoja na kuzingatia sheria na taratibu
zilizowekwa.
Katika hatua nyingine Waziri
wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa alizindua rasmi Bodi ya Wadhamini ya JKCI na
kuitaka kuimarisha utawala bora na uwajibikaji pamoja na kusimamia vizuri
Taasisi hiyo ili mikakati iliyowekwa iweze kutimizwa kwa wakati.
Akizindua bodi hiyo Mhe. Mchengerwa aliwataka wajumbe
wa Bodi ya Wadhamini walioteuliwa kutekeleza majukumu yao kwa weledi, uadilifu
na uzalendo ili kuhakikisha taasisi hiyo inaendelea kuwa kielelezo cha ubora
katika huduma za moyo ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.





Comments
Post a Comment