Wanawake wenye matatizo ya kifafa cha mimba epukeni kubadilisha wenza: Dkt. Raya
Daktari
bingwa wa magonjwa ya wanawake na wajawazito wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
(JKCI) Hospitali ya Dar Group Raya Chambali akiandika taarifa za mgonjwa
aliyefika kupata huduma katika hospitali hiyo iliyopo Temeke jijini Dar es
Salaam.
************************************************************************************* ***************************************
Na JKCI
Wanawake wenye matatizo
ya kupata kifafa cha mimba wakati wa ujauzito wameshauriwa kutobadilisha mwenza
baada ya kujifunga mtoto wa kwanza ili kuepuka vifo vinavyotokana na ugonjwa
huo.
Rai hiyo imetolewa na
daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake na wajawazito wa Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) Hospital ya Dar Group Raya Chambali wakati akitoa elimu kwa
wanawake wajawazito wanaotibiwa na Hospitali hiyo.
Dkt. Raya alisema
baadhi ya vifo vya wanawake wajazito hutokana na kifafa cha mimba kinachosababishwa
na tatizo la shinikizo la damu kuwa juu kipindi cha ujauzito.
“Kifafa cha mimba
kinaweza kuepukika endapo mama atazingatia ushauri wa watalaamu wa afya na
kutobadilisha mwenza wa kuzaa naye kwasababu ugonjwa huo ni wa kijenetiki ambao
chanzo chake hutoka kwa mwanaume” alisema Dkt. Raya
Aidha Dkt. Raya aliwataka
wanawake kuwa na tabia ya kufanya maandalizi ya mapema ya kitatibu kabla ya
kupata ujauzito ili waweze kuuandaa mwili na kuwa salama kubeba ujauzito.
“Mama akizingatia
ushauri wa kitalaamu kuna uwezekano mdogo wa kupata shinikizo la juu la damu na
kuepuka kifafa cha mimba kwani atashauriwa kuzingatia lishe bora na kupunguza
matumizi ya chumvi nyingi wakati wa ujauzito”, alisema Dkt. Raya
Naye mama wa watoto
watatu anayepata huduma katika Hospitali ya JKCI Dar Group Judith Nelson
alisema amewahi kupata tatizo la kifafa cha uzazi mara baada ya kujifungua
mtoto wa kwanza lakini baada ya kupata ushauri kutoka kwa madaktari wa JKCI Dar
Group tatizo hilo halijawahi kumrudia tena.
“Ni kweli
usipobadilisha mwenza unakuwa katika hali salama ya kutokupata tena kifafa cha
uzazi na mimba, kwa sasa nimeweza kupata watoto wengine wawili na sijapata
ugonjwa huo kwasababu nilizingatia ushauri wa daktari” alisema Judith.
Judith alisema tatizo
la kifafa cha mimba ni hatari kwa afya ya mama na mtoto kwani kinaweza sababisha
kiharusi kwa mama kutokana na shinikizo la damu kuwa juu sana, lakini pia
kupelekea mtoto kuzaliwa kabla ya wakati.
.jpeg)
.jpeg)
Comments
Post a Comment