JKCI yaandika historia yafanya upasuaji wa mshipa mkubwa wa damu (Aorta) kwa kutumia mtambo wa cathlab
Wataalam
wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na mwenzao kutoka nchini India Dkt.
Gireesh Mukund Warawdekar wakifanya upasuaji wa tundu dogo kwa kutumia mtambo
wa cathlab kuziba mshipa mkubwa wa damu (Aorta) ambao ulichanika kutokana na
ajali raia kutoka Jamhuri ya Watu wa China.
Wataalam
wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na mwenzao kutoka nchini India Dkt.
Gireesh Mukund Warawdekar wakifanya upasuaji wa tundu dogo kwa kutumia mtambo
wa cathlab kuziba mshipa mkubwa wa damu (Aorta) ambao ulichanika kutokana na
ajali raia kutoka Jamhuri ya Watu wa China.
Wataalam
wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na mwenzao kutoka nchini India Dkt.
Gireesh Mukund Warawdekar wakifanya upasuaji wa tundu dogo kwa kutumia mtambo
wa cathlab kuziba mshipa mkubwa wa damu (Aorta) ambao ulichanika kutokana na
ajali raia kutoka Jamhuri ya Watu wa China.
Picha Na
*************************************************************************************************************************
Wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa
kushirikiana na mwezao kutoka nchini India wameandika historia katika kutoa
huduma za matibabu ya moyo na mishipa ya damu baada ya kufanikiwa kumfanyia
upasuaji wa tundu dogo kwa kutumia mtambo wa cathlab mgonjwa ambaye mshipa wake
mkubwa wa damu (Aorta) ulichanika kufuatia ajali mbaya ya gari.
Matibabu hayo ya kibingwa ambayo hufanyika katika hospitali
chache barani Afrika yamefanyika kwa raia kutoka Jamhuri ya Watu wa China ambaye
mara baada ya kupata ajali alipewa rufaa kufika JKCI kwaajili ya matibabu.
Akizungumza kuhusiana na matibabu hayo Daktari bingwa wa
magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) George Longopa
alisema mgonjwa huyo alipata majeraha makubwa baada ya kupata ajali
ya gari iliyosababisha kuchanika kwa mshipa mkubwa wa damu (Aorta) unaosafirisha
damu kutoka kwenye moyo kwenda sehemu mbalimbali za mwili.
Dkt Longopa ambaye pia ni
Mkuu wa Idara ya Matibabu ya Moyo alisema mgonjwa huyo baada ya kupata huduma
za awali katika hospitali aliyoanzia, madaktari walibaini kuwa mgonjwa alikuwa
akipoteza damu nyingi, kupata maumivu makali hivyo kumpa rufaa ili aweze
kufanyiwa upasuaji JKCI.
Dkt. Longopa alisema
uchunguzi wa kina kwa kutumia mtambo wa CT Scan ulithibitisha kuwa mshipa
mkubwa wa damu (Aorta) ulikuwa umechanika kutokana na nguvu kubwa ya ajali hiyo
hali iliyohatarisha maisha yake.
“Baada ya kugundulika
kuwa mshipa mkubwa wa damu (Aorta) ulikuwa umechanika, mgonjwa alihamishiwa
JKCI kwaajili ya matibabu ya kibingwa zaidi. Alipofika hali yake ilikuwa mbaya
na alikuwa anaendelea kupoteza damu hivyo ilihitaji uamuzi wa haraka ili kuokoa
maisha yake”, alisema Dkt. Longopa
Kwa upande afisa Uuguzi
wa chumba cha upasuaji wa kutumia tundu dogo (Cathlab) wa Taasisi ya Moyo
Jakaya Kikwete (JKCI) Edna Kajuna alisema mgonjwa huyo alipokelewa akiwa katika
hali mbaya na kupelekwa katika chumba cha uangalizi maalumu (ICU) kabla ya kupelekwa
Cathlab kwaajili ya matibabu.
“Tunafurahi kuoana upasuaji wa mgonjwa wetu
umefanyika vizuri na sasa mgonjwa yupo wodini hali yake imeimarika, madhara
yote aliyoyapata baada ya ajali ile tumeweza kuyatatua”, alisema Edna
Mafanikio ya upasuaji huo
yanaendelea kuonesha uwezo wa JKCI katika kutoa huduma bingwa na za kisasa kwa
wagonjwa wa moyo na mishipa ya damu lakini pia kuimarisha ushirikiano kupitia
matibabu kwa wagonjwa kutoka nchi mbalimbali.
-
Mwisho -
Comments
Post a Comment