JKCI yaweka kambi ya matibabu ya moyo mkoani Manyara
Kaimu Mganga Mfawadhi wa
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Manyara (MRRH) Dkt. Yesige Mutajwaa akizungumza na
wataalamu wa afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa kambi
maalumu ya siku 5 ya uchunguzi na matibabu ya moyo ijulikanayo kama Mhe. Dkt.
Samia Suluhu Hassan tiba mkoba inayofanywa na wataalamu wa JKCI kwa
kushirikiana na wenzao wa MRRH
Wataalamu wa afya kutoka
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiwa katika kikao cha pamoja na wenzao
wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Manyara (MRRH) wakati wa kambi maalumu ya siku
5 ya uchunguzi na matibabu ya moyo ijulikanayo kama Mhe. Dkt. Samia Suluhu
Hassan tiba mkoba inayofanywa na wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao
wa MRRH.
****************************************************************************************************
Na Picha JKCI
Wananchi wa Mkoa wa Manyara
na mikoa ya jirani wametakiwa kujitokeza kwa wingi kufanya uchunguzi wa
magonjwa ya moyo wakati wa kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu inayofanywa
na wataalamu kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na
wenzao wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Manyara (MRRH).
Kambi hiyo maalumu ya siku
tano ijulikanayo kama Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tiba mkoba inafanyika katika
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Manyara (MRRH) iliyopo Mkoani Manyara.
Akizungumza wakati wa kuanza
kwa kambi hiyo Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Manyara (MRRH)
Dkt. Yasige Mutajwaa aliwaahidi wataalamu wa JKCI kutoa ushirikiano wa hali ya juu wakati wa kambi hiyo ili
kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za kibingwa za uchunguzi na matibabu ya
moyo.
“Wataalamu wetu watashirikiana
nanyi ili kwa pamoja tuweze kutekeleza lengo la kuwasogezea huduma bingwa
wananchi mahali walipo na kuweza kuwapa elimu kuhusu magonjwa ya moyo kwani magonjwa
hayo yamekuwa yakiongezeka katika jamii zetu”, alisema Dkt. Mutajwaa
Kwa upande wake daktari kutoka
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Pedro Pallangyo alisema kambi hiyo ni
sehemu ya juhudi za kusogeza huduma za kibingwa za uchunguzi na matibabu ya moyo
karibu na wananchi ili waweze kufanyiwa uchunguzi wa mapema na kupata matibabu
stahiki lakini pia kupata elimu ya kujikinga na magonjwa ya moyo.
“Hii ni mara yetu ya pili
kufanya kambi kama hii mkoani Manyara, mwitikio wa wananchi kushiriki katika
kambi hizi kwaajili ya kufanya uchunguzi wa afya umekuwa mkubwa hivyo kutupa
motisha ya kuendelea kuwapa huduma hizi”, alisema Dkt. Pedro
Kambi hiyo itafanyika hadi
tarehe 23 mwezi Agosti mwaka huu ambapo wananchi watafanyiwa vipimo vikubwa vya
moyo, kuonana na wataalamu mabingwa bobezi wa moyo na wale watakaokutwa na
matatizo ya moyo yanayohitaji uchunguzi zaidi kupewa rufaa kufika JKCI kwaajili
ya matibabu zaidi.
-
Mwisho -
Comments
Post a Comment