Watu 1,005 wapimwa moyo na macho Arusha
Kaimu Mkurugenzi
wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete – Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre
(JKCI – ALMC) Dkt. Godwin Kivuyo akimjulia hali mwananchi aliyefika katika
kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa yasiyoambukiza iliyokuwa
ikifanyika katika Hospitali ya JKCI-ALMC na kumalizika jana jijini Arusha.
Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete – Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (JKCI – ALMC) Dkt. Godwin Kivuyo akizungumza na wananchi wa mkoa wa Arusha waliofika katika kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa yasiyoambukiza iliyokuwa ikifanyika katika Hospitali ya JKCI-ALMC na kumalizika jana jijini Arusha.
Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete – Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (JKCI - ALMC) Farida Kessy akimpima uwiano wa urefu kwa uzito mkazi wa Arusha aliyefika katika kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa yasiyoambukiza iliyokuwa ikifanyika katika Hospitali ya JKCI-ALMC na kumalizika jana jijini Arusha.
Afisa huduma kwa
wateja wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete – Hospitali ya Arusha Lutheran
Medical Centre (JKCI - ALMC) Agness Kiwia akitoa elimu kuhusu magonjwa
yasiyoambukiza kwa wakazi wa Arusha waliofika katika kambi maalumu ya uchunguzi
na matibabu ya magonjwa yasiyoambukiza iliyokuwa ikifanyika katika Hospitali
hiyo na kumalizika jana jijini Arusha.
Na JKCI
********************************************************************************************************************************
Jumla ya watu
1,005 wamepatiwa huduma za uchunguzi na matibabu ya magonjwa yasiyoambukiza
ikiwemo magonjwa ya moyo na macho wakati wa kambi maalumu ya matibabu iliyomalizika
jana mkoani Arusha
Kambi hiyo
maalumu ilikuwa ikifanywa na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete – Hospitali
ya Arusha Lutheran Medical Centre (JKCI–ALMC) na kudhaminiwa na GSM Foundation
kwa lengo la kuwafikia wananchi wa Kanda ya Kaskazini na kusogeza huduma hizo
karibu na wananchi.
Akizingumza
wakati wa kufunga kambi hiyo Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
– Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (JKCI–ALMC) Dkt. Godwin Kivuyo alisema
idadi ya wagonjwa waliopatiwa huduma imevuka lengo lililowekwa hatua
inayoonesha mwitikio mkubwa wa wananchi kutumia fursa zilizopo kupata huduma za
afya.
“Kambi hii imekuwa
na siku tano ambazo tulikuwa tumedhamiria kuona wagonjwa elfu moja angalau
wagonjwa kati ya 150 hadi 200 kwa siku, mpaka leo tumeweza kuona wagonjwa 1,005
hivyo kufikia lengo tulilojiwekea”, alisema Dkt. Kivuyo.
Dkt. Kivuyo
alisema kupitia kambi hiyo wataalamu wa JKCI – ALMC wameweza kufanya vipimo
zaidi ya 800 kuchunguza magonjwa ya moyo na macho.
Kwa upande wake Mratibu
kutoka GSM Foundation Julius Ndyakoha alisema GSM kufadhili kambi hiyo ni
sehemu ya kurudisha kwa jamii, kuunga mkono jitihada zinazofanywa na JKCI
pamoja na Serikali katika kuboresha upatikanaji wa huduma za afya nchini.
Julius alisema
GSM Foundation itaendelea kushirikiana na wadau pamoja na taasisi zinazotoa
huduma za afya ili kusaidia kufanikisha malengo ya kuongeza fursa ya upatikanaji
wa matibabu kwa wananchi.
Leonila Baha mkazi
wa Arusha mjini alisema utaratibu wa utoaji wa huduma katika kambi hiyo
umesaidia kupunguza muda wa kusubiri licha ya idadi kubwa ya wananchi
waliojitokeza.
“Kambi hii
imekuwa na utaratibu mzuri, huduma zimetolewa kwa haraka, wataalamu wa afya
walikuwepo wa kutosha na hakukuwa na kujuana ili mtu apate huduma hivyo kila
mtu ameondoka akiwa ameridhika na huduma”, alisema Leonila.
Leonia alisema wananchi
wanapaswa kujenga utamaduni wa kuchunguza afya zao mara kwa mara na kutopuuza
fursa za kupata huduma za afya pale zinapojitokeza.
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
Comments
Post a Comment