Posts

Showing posts from August, 2020

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi azungumza na wagonjwa wanaotibiwa katika Taasisi hiyo

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akizungumza na wazazi kuhusu umuhimu wa kufanya kipimo cha kuchunguza moyo wa mtoto aliyepo tumboni kwa wamama wajawazito ( Fetal Echoc ardiogram ). Wazazi hao walifika katika Taasisi hiyo leo kwa ajili ya kuwaleta watoto wanaotibiwa Jkci kliniki.   Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akiwaeleza madhara ya mafuta mwilini   wagonjwa waliokuwa wanasubiri kufanyiwa vipimo vya kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi ( Echocardiogram - ECHO)   na Umeme wa moyo ( Electrocardiogram – ECG)   wanaotibiwa katika Taasisi hiyo.

Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete yapokea msaada wa mashine ya kupima umeme wa moyo (Electrocardiogram) yenye thamani ya shilingi milioni 17 kutoka kwa Jamii ya Ujerumani kwa magonjwa ya watoto ya Ukanda (Germany Society for tropical pediatrics) ambayo itatumika kwa ajili ya watoto

Image
  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akipokea msaada wa mashine ya kupima umeme wa moyo ( Electrocardiogram ) kutoka kwa Daktari bingwa wa magonjwa ya watoto Antke Zuechner wa Jamii ya Ujerumani kwa magonjwa ya watoto ya Ukanda (Germany Society for tropical pediatrics) ambayo itatumika kwa ajili ya watoto wanaotibiwa katika Taasisi hiyo. Thamani ya mashine hiyo ni shilingi milioni 17.   Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akimpulizia kisafisha mikono (hand sanitizer ) Daktari bingwa wa magonjwa ya watoto Antke Zuechner wa Jamii ya Ujerumani kwa magonjwa ya watoto ya Ukanda (Germany Society for tropical pediatrics)  mara baada ya kumkabidhi msaada wa mashine ya kupima umeme wa moyo ( Electrocardiogram )  kwa watoto wanaotibiwa katika Taasisi hiyo. Thamani ya mashine hiyo ni shilingi milioni 17. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akimshukuru Daktari

CRDB BENKI YACHANGIA MATIBABU YA WATOTO 100 WENYE MAGONJWA YA MOYO WANAOTIBIWA JKCI

Image
Wataalam wa afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakitoa huduma kwa wananchi walioshiriki mbio za CRDB Marathon kwa ajili ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa katika taasisi hiyo leo wakati wa mbio hizo zilizofanyika katika viwanja vya Farasi Oyster bay Jijini Dar es Salaam Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi hundi ya Shilingi milioni 200 iliyotolewa leo katika viwanja vya Farasi Oyster bay Jijini Dar es Salaam na Benki ya CRDB zilizokusanywa kutoka kwa washiriki wa mbio za CRDB Marathon kwa ajili ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa JKCI  Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi tuzo iliyotolewa leo katika viwanja vya Farasi Oyster bay Jijini Dar es Salaam na Benki ya CRDB kutambua huduma zinazofa

Klabu ya Mazoezi ya Xtreme Workout Bootcamp watembelea wodi ya watoto JKCI

Image
Wanachama wa klabu ya mazoezi ya Xtreme workout bootcamp wakifanya usafi katika jengo la watoto wenye magonjwa ya moyo walipotembelea watoto waliolazwa katika jengo hilo kwa ajili ya kutoa zawadi kwa watoto pamoja na kuchangia gharama za kutengeneza kadi mbili za bima ya afya kwa watoto leo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Jijini Dar es Salaam  Wanachama wa klabu ya mazoezi ya Xtreme workout bootcamp wakifanya usafi katika jengo la watoto wenye magonjwa ya moyo walipotembelea watoto waliolazwa katika jengo hilo kwa ajili ya kutoa zawadi kwa watoto pamoja na kuchangia gharama za kutengeneza kadi mbili za bima ya afya kwa watoto leo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Jijini Dar es Salaam  Mama mwenye mtoto aliyelaza katika wodi ya watoto wenye magonjwa ya moyo Halima Selemani akipokea zawadi za mwanae kutoka kwa wanachama wa klabu ya mazoezi ya Xtreme workout bootcamp waliotembelea JKCI kwa ajili ya kufanya usafi katika jengo la watoto pamoja na kut