Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete yapokea msaada wa mashine ya kupima umeme wa moyo (Electrocardiogram) yenye thamani ya shilingi milioni 17 kutoka kwa Jamii ya Ujerumani kwa magonjwa ya watoto ya Ukanda (Germany Society for tropical pediatrics) ambayo itatumika kwa ajili ya watoto
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akipokea msaada wa mashine ya kupima umeme
wa moyo (Electrocardiogram) kutoka kwa Daktari
bingwa wa magonjwa ya watoto Antke Zuechner wa Jamii ya Ujerumani kwa magonjwa
ya watoto ya Ukanda (Germany Society for tropical pediatrics) ambayo itatumika
kwa ajili ya watoto wanaotibiwa katika Taasisi hiyo. Thamani ya mashine hiyo ni shilingi milioni 17.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akimpulizia kisafisha mikono (hand
sanitizer ) Daktari bingwa wa magonjwa ya watoto Antke Zuechner wa Jamii ya
Ujerumani kwa magonjwa ya watoto ya Ukanda (Germany Society for tropical
pediatrics) mara baada ya kumkabidhi msaada
wa mashine ya kupima umeme wa moyo (Electrocardiogram) kwa watoto wanaotibiwa katika Taasisi hiyo.
Thamani ya mashine hiyo ni shilingi milioni 17.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akimshukuru Daktari bingwa wa magonjwa ya
watoto Antke Zuechner wa Jamii ya Ujerumani kwa magonjwa ya watoto ya Ukanda
(Germany Society for tropical pediatrics)
kwa msaada wa mashine ya kupima umeme wa moyo (Electrocardiogram) kwa watoto wanaotibiwa katika Taasisi hiyo.
Kushoto ni Mkuu wa kitengo cha magonjwa ya moyo kwa watoto Dkt. Sulende Khuboja
akifuatiwa na Mkuu wa kitengo cha Mafunzo na Utafiti Dkt. Naiz Majani.
Comments
Post a Comment