Posts

Showing posts from November, 2020

Daktari wa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Parvina Kazahura awa mshindi wa kwanza wa kundi la tafiti za kuzuia magojwa yasiyo ya kuambukiza

Image
  Katibu Mkuu wizara ya Afya Prof. Mabula Mchembe akimkabidhi Daktari wa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Parvina Kazahura cheti cha mshindi wa kwanza wa kundi la tafiti za kuzuia magojwa yasiyo ya kuambukiza ambaye alifanya utafiti wa kugundua mapema magonjwa ya valvu za moyo kwa watoto wa shule za msingi katika mkoa wa Dar es Salaam . Dkt. Parvina alikabidhiwa cheti hicho hivi karibuni wakati wa  kongamano la pili la kitaifa la sayansi la magonjwa yasiyoambukiza lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa mwalimu Julius Nyerere uliopo jijini Dar es Salaam. Katibu Mkuu wizara ya Afya Prof. Mabula Mchembe akimkabidhi Daktari wa Chuo Kikuu cha Dodoma   Azan Nyundo cheti cha mshindi wa kwanza wa utafiti alioufanya kuhusu tabia hatarishi za magonnjwa ya moyo kwa wagonjwa waliolazwa katika hospitali ya Mirembe wanaotumia dawa za magonjwa ya akili wakati wa   kongamano la pili la kitaifa la sayansi la magonjwa yasiyoambukiza lililomalizika  hivi karibuni  katika u

Kampuni ya Vunja bei yatoa zawadi za vyombo kwa wafayakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)

Image
  Mkurugenzi wa Kampuni ya Vunja bei Shija Kamanija akizungumza na wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) mara baada ya kufika katika taasisi hiyo kwa ajili ya kuwapa zawadi za vyombo na kuwauzia bidhaa hizo kwa bei naafuu. Kampuni hiyo ilifanya hivyo ikiwa ni moja ya njia ya kufikisha huduma wanayoitoa kiurahisi kwa wafanyakazi hao pamoja na kuwapa motisha ya kazi wanayoifanya ya kutibu wagonjwa wenye matatizo ya moyo. Mkurugenzi wa Kampuni ya Vunja bei Shija Kamanija akimpa zawadi ya boxi lenye glasi za kuywea juice Dominick Kanani  ambaye ni mfanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) mara baada ya kufika katika taasisi hiyo  kwa ajili ya kutoa  zawadi za vyombo na kuwauzia wafanyakazi bidhaa hizo kwa bei naafuu. Kampuni hiyo ilifanya hivyo ikiwa ni moja ya njia ya kufikisha huduma wanayoitoa kiurahisi kwa wafanyakazi hao pamoja na kuwapa motisha ya kazi wanayoifanya ya kutibu wagonjwa wenye matatizo ya moyo.                                                    

Wafanyakazi bora wa robo ya kwanza ya mwaka wa fedha wa 2020/21 wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete wapongezwa kwa utendaji mzuri wa kazi

Image
Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Utawala na Fedha wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) CPA Agnes Kuhenga akisoma majina ya wafanyakazi bora wa robo ya kwanza ya mwaka wa fedha wa 2020/21 wa Taasisi hiyo ambapo wafanyakazi watatu walichaguliwa na kupewa zawadi mbalimbali za kuwapongeza kutokana na   utendaji wao mzuri wa kazi. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akimkabidhi zawadi ya ngao mfanyakazi bora wa robo ya kwanza ya mwaka wa fedha wa 2020/21 aliyeshika nafasi ya kwanza George Msabila wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza wafanyakazi bora watatu iliyofanyika leo katika Taasisi hiyo. Mfanyakazi huyo pia alipewa zawadi ya fedha taslimu shilingi milioni moja na laki tano. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akimkabidhi zawadi ya cheti   mfanyakazi bora wa robo ya kwanza ya mwaka wa fedha wa 2020/21 aliyeshika nafasi ya pili Dkt. Henry Mayala wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza wafanyakazi bora w

Wanawake ‘watoa ya moyoni’ Jukwaa la Women Health Talk

Image
Miss Tanzania 2001 Happiness Magese akiuliza swali wakati wa Jukwaa la Women Health Talk 2020 lililofanyika Jijini Dar es Salaam lililoandaliwa na Doctor's Plaza Polyclinic kwa kushirikiana na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), GSM Tanzania, Hyatt Regency Hotel, MultiChoise Tanzania (DSTV), Ajanta Pharma na Masilamani KasMedics. Wanawake wanakabiliwa na changamoto nyingi ambazo hawana majibu yake, wengine hawajui wapi wanakoweza kupata ufumbuzi, hali inayowasababishia baadhi yao kujikuta wakipata magonjwa mbalimbali na hata unyanyaswaji wa kijinsi na kingono. Yamebainishwa hayo wakati wa majadiliano kwenye Jukwaa la Women Health Talk 2020 lililowakutanisha wanawake wa taaluma mbalimbali pamoja na wataalamu mabingwa wa magonjwa ya binadamu ikiwamo ya kina mama, moyo, saratani na kisukari. Akiwasilisha mada katika Jukwaa hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika lisilo la Kiserikali la Tanzania Health Promotion Support (THPS), Dk. Redempta Mbatia alisema wapo baadhi ya wanawake wali