Daktari wa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Parvina Kazahura awa mshindi wa kwanza wa kundi la tafiti za kuzuia magojwa yasiyo ya kuambukiza


 Katibu Mkuu wizara ya Afya Prof. Mabula Mchembe akimkabidhi Daktari wa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Parvina Kazahura cheti cha mshindi wa kwanza wa kundi la tafiti za kuzuia magojwa yasiyo ya kuambukiza ambaye alifanya utafiti wa kugundua mapema magonjwa ya valvu za moyo kwa watoto wa shule za msingi katika mkoa wa Dar es Salaam . Dkt. Parvina alikabidhiwa cheti hicho hivi karibuni wakati wa  kongamano la pili la kitaifa la sayansi la magonjwa yasiyoambukiza lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa mwalimu Julius Nyerere uliopo jijini Dar es Salaam.

Katibu Mkuu wizara ya Afya Prof. Mabula Mchembe akimkabidhi Daktari wa Chuo Kikuu cha Dodoma  Azan Nyundo cheti cha mshindi wa kwanza wa utafiti alioufanya kuhusu tabia hatarishi za magonnjwa ya moyo kwa wagonjwa waliolazwa katika hospitali ya Mirembe wanaotumia dawa za magonjwa ya akili wakati wa  kongamano la pili la kitaifa la sayansi la magonjwa yasiyoambukiza lililomalizika  hivi karibuni katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa mwalimu Julius Nyerere uliopo jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akieleza uzoefu wa taasisi hiyo katika kutoa huduma za matibabu ya kibingwa ya magojwa ya moyo kwa kipindi cha miaka mitano wakati wa  kongamano la pili la kitaifa la sayansi la magonjwa yasiyoambukiza lililomalizika hivi karibuni  katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa mwalimu Julius Nyerere uliopo jijini Dar es Salaam

 Salome Majaliwa kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) akiwaeleza wanafunzi wa shule ya Sekondari waliotembelea banda la Taasisi hiyo kuhusu huduma mbalimbali za matibabu ya moyo wanazozitoa wakati wa  kongamano la pili la kitaifa la sayansi la magonjwa yasiyoambukiza lililomalizika hivi karibuni  katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa mwalimu Julius Nyerere ulioko jijini Dar es Salaam.


Comments

Popular posts from this blog

Wataalamu wa JKCI kufanya upasuaji wa moyo nchini Zambia

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yamshukuru Rais Dkt.Samia kwa kuwapa magari