Posts

Showing posts from February, 2021

Serikali yawashukuru wataalamu wa afya nchini kwa kutoa huduma bora za matibabu kwa wagonjwa - Dkt. Mollel

Image
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Godwin Mollel akizungumza na wagonjwa wanaotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa ziara yake ya kikazi katika Taasisi hiyo Jana Jijini Dar es Salaam Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Godwin Mollel akizungumza na madaktari wa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) waliokuwa wakiwaudumia wagonjwa waliolazwa wodini wakati wa ziara yake ya kikazi katika Taasisi hiyo Jana Jijini Dar es Salaam. Na: JKCI Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Godwin Mollel amewashukuru wataalamu wa afya nchini kwa moyo wao wa uzalendo wa kutoa huduma bora za matibabu kwa wagonjwa. Mhe. Mollel ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaja Kikwete (JKCI) aliowakuta wanawatibu wagonjwa wodini na kliniki wakati wa ziara yake ya kikazi aliyoifanya leo katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Dkt

Ondoeni hofu Serikali inahakikisha mko salama kwa kutoa huduma bora za afya - Dkt. Mollel

Image
Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Tulizo Shemu akimwelezea Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Godwin Mollel jinsi walivyomuhudumia mgonjwa aliyefanyiwa  upasuaji mdogo wa moyo wa bila kufungua kifua  wakati wa ziara yake ya kikazi katika Taasisi hiyo iliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam. Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Godwin Mollel akiwajulia hali wagonjwa waliolazwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa ziara yake ya kikazi katika Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambaye pia ni msimamizi wa wodi ya watoto Theresa Marombe akimwelezea Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Godwin Mollel namna ambavyo wodi hiyo  inavyowahudumia watoto wakati wa ziara yake ya kikazi katika Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,

TUENDELEE KUMUOMBA MUNGU NA TUCHUKUE TAHADHARI - WAZIRI MKUU

Image
 

Ushirikiano kati ya Tanzania na Saud Arabia katika sekta ya afya

Image

TAASISI NA VYUO VYA AFYA ZATAKIWA KUSHIRIKIANA ILI KUBORESHA TIBA ASILI NCHINI

Image
Taasisi za Sekta ya Afya na Vyuo vya afya nchini vimetakiwa kushirikiana kwa pamoja ili kuboresha tiba asili ambayo imekuwa na mchango mkubwa katika kupambana na magonja ya kuambukiza na yasiyoambukiza. Wito huo umetolewa leo na Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Bw. Edward Mbaga alipokuwa akifungua kikao kazi cha viongozi wa taasisi zilizo chini ya Wizara ya Afya na Vyuo vya taaluma ya afya nchini kilicholenga kuboresha ushirikiano na kuangalia namna ya kuongeza rasilimali katika kuboresha tiba asili nchini.   “Tumekutana hapa ili kuwa pamoja tujadili jinsi ya kushirikiana katika kupata frdha za kugharamia uzalishaji na kufanya tafiti za kutambua usalama, ubora na ufanisi wa dawa za tiba asili nchini” amese Bw. Mbaga wakati akifungua kikao kazi hicho.   Amesema kuwa Jamii imekuwa ikitumia huduma za tiba asili kwa ajili ya kutibu magonjwa mbalimbali na baadhi ya wananchi wanatumia huduma zote mbili kwa maana ya tiba ya kisasa na tiba asili katika kutibu magonjwa.   “Kuna umuhimu mkubwa

Wafanyakazi bora wa robo ya pili ya mwaka wa fedha 2020/21 wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete wapongezwa kwa utendaji mzuri wa kazi

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akimkabidhi zawadi ya ngao mfanyakazi bora wa robo ya pili ya mwaka wa fedha 2020/2021 aliyeshika nafasi ya kwanza Mtoka David Mtoka wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza wafanyakazi bora watatu iliyofanyika leo katika Taasisi hiyo. Mfanyakazi huyo pia alipewa zawadi ya fedha taslimu shilingi milioni mbili Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akimkabidhi cheti mfanyakazi bora wa robo ya pili ya mwaka wa fedha 2020/2021 aliyeshika nafasi ya pili Mohamed Songoro wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza wafanyakazi bora watatu iliyofanyika leo katika Taasisi hiyo. Mfanyakazi huyo pia alipewa zawadi ya fedha taslimu shilingi milioni moja na laki tano Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akimkabidhi cheti mfanyakazi bora wa robo ya pili ya mwaka wa fedha 2020/2021 aliyeshika nafasi ya tatu Lucas Jilulu wakati wa hafla fupi ya ku