Ondoeni hofu Serikali inahakikisha mko salama kwa kutoa huduma bora za afya - Dkt. Mollel
Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Tulizo Shemu akimwelezea Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Godwin Mollel jinsi walivyomuhudumia mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji mdogo wa moyo wa bila kufungua kifua wakati wa ziara yake ya kikazi katika Taasisi hiyo iliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Godwin
Mollel akiwajulia hali wagonjwa waliolazwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) wakati wa ziara yake ya kikazi katika Taasisi hiyo leo Jijini
Dar es Salaam
Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambaye pia ni msimamizi wa wodi ya watoto Theresa Marombe akimwelezea Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Godwin Mollel namna ambavyo wodi hiyo inavyowahudumia watoto wakati wa ziara yake ya kikazi katika Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Godwin Mollel akimjulia hali mtoto Sophia Naminga anayetibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa ziara yake ya kikazi katika Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Dkt. Winnie Masakuya, na katikati ni daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto Naiz Majani
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akimwelezea Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Godwin Mollel namna ambavyo duka la dawa la Taasisi hiyo linavyohudumia wagonjwa wakati wa ziara yake ya kikazi katika Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Godwin Mollel akizungumza na wagonjwa wanaosubiri kuingia katika vyumba vya madaktari katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa ziara yake ya kikazi katika Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam.
Naibu
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Godwin
Mollel akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo
Jakaya Kikwete (JKCI) mara baada ya kumalizika kwa ziara yake ya kikazi aliyoifanya
leo katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Watano kulia ni
Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Prof. Mohamed Janabi
Na: JKCI
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Godwin Mollel amewataka wananchi kuondoa hofu kutokana
na changamoto za kiafya wanazopitia bali waamini wako salama kwani Serikali iko
kazini kwa kuhakikisha wanapata huduma bora za afya na hivyo kuwa salama.
Mhe. Mollel ameyasema hayo alipokuwa
akizungumza na wagonjwa wanaotibiwa kwenye Taasisi ya Moyo Jakaja Kikwete
(JKCI) wakati wa ziara yake ya kikazi ya kuwashukuru wafanyakazi wa afya aliyoifanya
leo katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.
Aliwasihi wagonjwa hao kufuata ushauri wa
kitaalamu wanaopewa na madaktari wanaowatibu na unaotolewa na Wizara ya Afya
kwa kufanya hivyo wataweza kuepukana na magonjwa ya kuambukiza na yasiyo ya
kuambukiza na hivyo kuwa na afya njema.
“Ninawaomba wananchi muondoe hofu kwani ukiwa
na hofu hata kinga za mwili zinashuka na hivyo kusababisha mwili kushindwa
kukabiliana na magonjwa pale ambapo utavamiwa na vijidudu”,.
“Pale ambapo utakutana na changamoto
mbalimbali za afya usisahau kufuata ushauri wa wataalamu wa afya na kumuomba Mungu akujalie afya njema kwani yeye
ndiye kila kitu katika maisha yetu”, alisisitiza Dkt. Mollel.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa
Taasisi hiyo Prof. Mohamed Janabi alimshukuru Naibu Waziri kwa kuwatembelea na
kupata muda wa kuzungumza na wagonjwa pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa
Taasisi hiyo.
Alisema mbali na Dunia kukabiliana
na ugonjwa unaosababisha Virus vya Corona (COVID 19) kwa mwaka jana wa 2020Taasisi
hiyo iliweza kutibu wagonjwa 99,046 ambapo
kati ya hao wagonjwa waliotibiwa na kurudi nyumbani (outpatient) walikuwa
94,079, waliolazwa (inpatients) walikuwa 3,306 waliofanyiwa upasuaji wa kutumia
tundu dogo 1262 na upasuaji wa kufungua kifua wagonjwa
399.
Alisema Taasisi hiyo
haina changamoto ya upatikanaji wa dawa na
vifaa tiba na kuongeza kuwa asilimia 52 ya mapato yao yanatokana na dawa zinazotolewa kwa wagonjwa, maabara na
vipimo vingine vya uchunguzi.
“Tunaishukuru
Serikali kwa kutambua
kazi kubwa inayofanywa na JKCI na kuhakikisha dawa
zinapatikana katika Hospitali yetu na hii inasaidia wagonjwa kupata huduma zote
za matibabu, vipimo na dawa bila ya usumbufu wowote”, alishukuru Prof. Janabi.
Comments
Post a Comment