Serikali yaokoa Mil.500 kwa Upasuaji wa moyo JKCI
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimpatia tuzo ya shukrani Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mratibu wa Shirika la Open Heart International (OHI) la nchini Australia Darren Wolfers kutokana na ushirikiano uliopoa baina ya JKCI na shirika hilo katika kutoa huduma za matibabu ya moyo kwa watanzania na mafunzo kwa wataalamu wa afya. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza wakati wa kufunga kambi maalumu ya upasuaji wa moyo iliyofanywa na wataalam wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa Shirika la Open Heart International (OHI) la nchini Australia ambapo wagonjwa 17 wamefanyiwa upasuaji katika kambi hiyo. Mkurugenzi wa Idara ya Upasuaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Angela Muhozya akitoa neno la shukrani wakati wa kufunga kambi maalumu ya upasuaji wa moyo iliyofanywa na wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao kutoka Shirika la O...