Makonda aishukuru JKCI kwa kufanya upimaji wa moyo kwa wakazi wa Arusha
.jpg)
Daktari Bingwa wa Watoto kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Rose Chengo akimweleza aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Paul Makonda kuhusu watoto wanaotibiwa katika kambi maalum ya madaktari bingwa na wabobezi wa magonjwa mbalimbali inayofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid. Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Makonda akimsalimia mwananchi aliyefika kupata huduma ya uchunguzi na matibabu ya moyo katika banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa kambi maalum ya madaktari bingwa na wabobezi wa magonjwa mbalimbali inayofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid. Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Paul Makonda akisalimiana na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mohamed Aloyce anayetoa huduma za matibabu ya moyo kwa wananchi wa mkoa huo zinazotolewa katika kambi maalum ya madaktari bingwa na wabobezi wa magonjwa mbalimbali inayofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha. K...