Mchengerwa asema JKCI nguzo huduma za afya AFCON

Mkurugenzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimkabidhi kitabu Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa kinachohusu watoto waliozaliwa kabla ya muda (watoto njiti) alipotembelea hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) katika ziara yake ya kuangalia maandalizi ya kitiba kuelekea mashindano ya AFCON 2027 aliyoifanya katika hospitali hiyo.

Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa akipokea ua kutoka kwa Victoria Komba alipotembelea hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) ambayo kwa sasa inasimamiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ikiwa ni maandalizi ya kitiba kuelekea mashindano ya AFCON 2027.
Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) Salehe Mwinchete akimueleza Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa kuhusu vifaa vya kisasa vinavyosaidia kuwatunza watoto waliozaliwa kabla ya muda (watoto njiti) katika ziara yake ya kuangalia maandalizi ya kitiba kuelekea mashindano ya AFCON 2027 aliyoifanya katika hospitali hiyo.
Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa akipanda mti katika Hospital ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) inayosimamiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ikiwa ni kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kusherehekea siku yake ya kuzaliwa. Mhe. Mchengerwa alipanda mti huo alipotembelea hospitali hiyo kwaajili ya ziara ya kuangalia maandalizi ya kitiba kueleka AFCON 2027.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mhe. Amos Makalla, akipanda mti katika Hospital ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) inayosimamiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ikiwa ni kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kusherehekea siku yake ya kuzaliwa.
Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa akizungumza na wafanyakazi wa afya na wananchi wa Arusha alipotembelea hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) ambayo kwasasa inasimamiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) katika ziara yake ya kuangalia ikiwa ni maandalizi ya kitiba kuelekea mashindano ya AFCON 2027.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akisoma taarifa ya utendaji kazi wa taasisi hiyo kwa Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa alipotembelea hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) ambayo kwasasa inasimamiwa na JKCI, kwaajili ya kuangalia maandalizi ya kitiba kuelekea mashindano ya AFCON 2027.
***********************************************************************************************************************************************************************************************
Tanzania iko tayari kutoa huduma za afya za kibingwa na kibobezi kupitia
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na Hospitali ya Arusha Lutheran Medical
Centre (ALMC), hatua inayoonesha dhamira ya dhati ya nchi katika kuimarisha
maandalizi ya kitabibu kuelekea Michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON)
2027.
Kauli
hiyo ilitolewa na Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa, leo jijini Arusha
wakati wa ziara yake ya kutembelea ALMC ambayo hivi sasa inasimamiwa na JKCI
ikiwa ni maandalizi ya kitabibu kuelekea AFCON 2027.
Mhe. Waziri Mchengerwa alisema zaidi ya kuwa tukio la michezo,
AFCON 2027 pia itakuwa ni fursa adhimu ya kimkakati kwa Tanzania kujitangaza
kimataifa katika sekta mbalimbali ikiwemo utalii, afya na uwekezaji.
“Hivi sasa tunajiandaa na michuano ya AFCON, kupitia maandalizi
haya, serikali inaendelea kuwekeza katika miundombinu ya afya, kuimarisha uwezo
wa wataalamu wa tiba na kuhakikisha uwepo wa huduma za dharura za kiwango cha
juu zitakazokidhi mahitaji ya wachezaji, wageni na wananchi kwa ujumla,”alisema
Mhe. Waziri Mchengerwa.
Alibainisha kuwa ushirikiano kati ya taasisi hizo kupitia Kanisa
la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) ni wa kimkakati, wenye tija kwa sasa
na wenye manufaa makubwa kwa mustakabali wa sekta ya afya nchini.
Akizungumza
kuhusu changamoto ya magonjwa yasiyoambukiza, Mhe. Waziri Mchengerwa alinukuu
takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) zinazoonesha kuwa zaidi ya vifo
milioni 17.5 duniani, sawa na asilimia 32 husababishwa na magonjwa ya moyo,
huku Mkoa wa Arusha ukiwa ni miongoni
mwa mikoa yenye idadi kubwa ya wagonjwa wa magonjwa hayo.
Alitoa wito kwa wananchi kujiunga na Mfuko wa Bima ya Afya kwa
Wote huku akisisitiza kuwa ni kinga muhimu ya kifedha na nyenzo ya kuokoa
maisha wakati ambapo hauna fedha za matibabu.
Kwa
upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Amos Makalla, alisema mkoa huo
umejipanga kikamilifu katika maandalizi ya kitabibu kuelekea AFCON 2027, huku akibainisha
kuwa JKCI iko tayari kutoa huduma za matibabu ya moyo kwa wananchi pamoja na
wageni watakaohudhuria michuano hiyo.
Mkurugenzi
Mtendaji wa JKCI Dk. Peter Kisenge, alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuimarisha sekta ya afya
kupitia utekelezaji wa miradi ya kimkakati. Alisema taasisi hiyo tayari
imewahudumia zaidi ya wagonjwa 26,000 kupitia huduma ya tiba mkoba na ina
matawi saba nchini.
Dk.
Kisenge aliongeza kuwa JKCI imeanza kutumia teknolojia ya akiliunde (Artificial
Intelligence – AI) pamoja na mifumo ya kidijitali kufuatilia maendeleo ya
wagonjwa baada ya matibabu, sambamba na kufanya upasuaji mkubwa wa moyo wa kufungua
kifua na upasuaji wa kisasa wa matundu madogo.
“Tupo
katika mpango wa kuanzisha maabara kubwa yenye vifaa vya kisasa ikiwemo MRI na
CT Scan. Tayari mwekezaji kutoka China ameonesha nia ya kuwekeza katika
hospitali hii,” alisema.
Dkt. Kisenge ambaye pia ni daktari bingwa wa moyo na mtaalamu wa
kupandikiza vifaa visaidizi vya moyo alisema JKCI imepokea maombi ya
ushirikiano kutoka nchi za Kongo na Burkina Faso katika huduma za magonjwa ya
moyo na tiba utalii, hatua inayotarajiwa kuongeza mapato ya serikali na kuiweka
Tanzania katika ramani ya huduma za afya za kibingwa barani Afrika.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dk. Seif Shekalaghe alisema
ushirikiano kati ya serikali, taasisi za dini na sekta binafsi ni nguzo muhimu
katika kuboresha huduma za afya na kuhakikisha maandalizi ya AFCON 2027
yanafanikiwa kwa viwango vya juu.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Hospitali ya ALMC, Peter Maduki alisema ushirikiano kati ya JKCI na Dayosisi ya Kaskazini Kati ya KKKT ni wa kipekee na umechangia kwa kiwango kikubwa kuboresha huduma za afya kwa wananchi wa Mkoa wa Arusha na Tanzania kwa ujumla.


.jpeg)


Comments
Post a Comment