DC Mkude awahamasisha wananchi kupima afya kambi ya ALMC

Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Salehe Mwinchete akimueleza Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Joseph Mkude Jinsi wanavyopima utendaji kazi wa moyo kwa kutumia mashine ya ECHO wakati wa  kambi maalumu ya upimaji na matibabu ya magonjwa mbalimbali yakiwemo ya moyo inayofanyika Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC).


Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Joseph Mkude akimsalimia mmoja ya mwananchi wa jiji la Arusha aliyefika kufanyiwa uchunguzi na matibabu ya moyo katika kambi maalumu ya matibabu ya magonjwa mbalimbali yakiwemo ya moyo inayofanyika katika Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Center (ALMC).

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Dkt. Peter Kisenge akimsalimia mkazi wa Arusha aliyefika kufanyiwa uchunguzi na matibabu ya moyo katika kambi maalumu ya matibabu ya magonjwa mbalimbali yakiwemo ya moyo inayofanyika katika Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Center (ALMC).

Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hania Bwahama akimpima mkazi  wa Arusha kipimo cha kuangalia sukari kwenye damu  katika kambi maalumu ya upimaji na matibabu ya magonjwa mbalimbali yakiwemo ya moyo inayofanyika katika Hospitali Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) iliyopo jijini Arusha.

Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Joseph Mkude akizungumza na waandishi wa habari alipotembelea kambi maalumu ya matibabu ya magonjwa mbalimbali ikiwemo ya moyo inayofanyika katika Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Center (ALMC).

Comments

Popular posts from this blog

JKCI na Burkina Faso zasaini makubaliano ya ushirikiano katika kutoa tiba ya magonjwa ya moyo

Wanawake waaswa kulinda mioyo yao, kuepuka sukari na chumvi kupita kiasi

Msumbiji kushirikiana na JKCI katika tiba ya moyo