Posts

Showing posts from September, 2020

Taarifa kwa Umma; Kuelekea maadhimisho Siku ya Moyo Duniani Septemba 29, 2020

Image
 

Wakazi wa Temeke wachangamkia huduma za uchunguzi, matibabu ya moyo iliyotolewa na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Jukwaa la One Stop Jawabu

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi  akimpima shinikizo la damu (BP) mwananchi  aliyetembelea banda la Taasisi hiyo kwa ajili ya kufanya  uchunguzi wa magonjwa ya moyo katika viwanja vya MwembeYanga wilayani Temeke kupitia jukwaa la One Stop Jawabu  ambapo JKCI ilitoa bila malipo huduma za upimaji,  matibabu na ushauri wa magonjwa ya moyo kwa watu 150. SEPTEMBA 24, 2020 – DAR ES SALAAM Mwitiko wa wakazi wa Wilaya ya Temeke, jijini hapa kwenda kufanyiwa uchunguzi na matibabu dhidi ya magonjwa ya moyo katika viwanja vya mwembe yanga, umekuwa mkubwa.   Wananchi hao wamepata fursa hiyo ya kuchunguzwa na kutibiwa bila malipo pamoja na kupewa ushauri wa lishe jinsi gani wanaweza kuendelea kutunza afya ya moyo na mwili kwa ujumla ili kuepuka magonjwa yasiyoambukiza. Akizungumza katika Viwanja vya Mwembe Yanga, Wilayani humo, katika Jukwaa hilo lililoratibiwa na Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Godwin Gondwe, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakay

Watu 150 wachunguzwa afya ya moyo wilaya ya temeke, jukwaa la One Stop Jawabu na wataalamu mabingwa wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete

Image
Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Aloycia Lyimo akimpima kiwango cha sukari mwilini mwananchi aliyetembelea banda la Taasisi hiyo jana katika viwanja vya MwembeYanga wilayani Temeke kupitia jukwaa la One Stop Jawabu  ambapo JKCI  ilitoa bila malipo huduma za upimaji,  matibabu na ushauri wa magonjwa ya moyo kwa watu 150.  Septemba 24, 2020 – DAR ES SALAAM Jumla ya watu 150 wamejitokeza na kufanyiwa uchunguzi na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), watu 37 kati ya hao wamekutwa na shinikizo la damu, 19 walikuwa hawajijui hali zao hapo kabla. Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo wa JKCI, Samweli Rweyemamu alisema hayo alipozungumza na waandishi wa habari alipokuwa akieleeza tathmini kuhusu huduma ya uchunguzi na tiba waliyoitoa kwa wakazi wa Temeke, Septemba 18 na 23, mwaka huu, Viwanja vya Mwembe Yanga na Zakheem, kwenye Jukwaa la One Stop Jawabu. “Mwamko na mwitiko wa wananchi umekuwa mkubwa, juzi kule Zakheem tuliona watu 103, pamoja na leo jumla

Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) yawaibua watu 21 wenye shida mbalimbali za moyo, 18 wakutwa na Shinikizo la Damu, zaidi ya asilimia 50 wana uzito uliopitiliza, Jukwaa la One Stop Jawabu - MBAGALA

Image
Daktari wa  Taasisi ya  Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Samwel Rweyemamu akimpatia dawa mwananchi aliyetembelea banda la Taasisi hiyo kwa ajili ya kufanya  uchunguzi wa magonjwa ya moyo na kukutwa  na tatizo.  Uchunguzi huo ulifanyika hivi karibuni katika viwanja vya Mbagala Zakheem wilayani Temeke kupitia jukwaa la  One Stop Jawabu  ambapo wananchi 103 walifika katika banda hilo na kupewa huduma za ushauri na upimaji wa magonjwa ya moyo.  DAR ES SALAAM TAASISI ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), imewaibua watu 21 wenye matatizo mbalimbali ya moyo, 18 wamekutwa na shinikizo la damu, walipochunguzwa afya zao katika Viwanja vya Mbagala Zakheem wilayani Temeke kwenye jukwaa la One Stop Jawabu. Akizungumza na waandishi wa habari, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo wa JKCI, Samweli Rweyemamu alisema watu 16 kati ya 18 waliokutwa na shinikizo la damu walikuwa hawajitambui kwamba wanakabiliwa na tatizo hilo. “Hii ni sawa na asilimia 18, yupo mmoja ambaye tumemkuta ana shinikizo la damu 200 chini y

Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) yaanzisha kliniki maalum kwa wagonjwa wa sikoseli wanaokabiliwa na magonjwa ya moyo

Image
Mwakilishi wa Mganga mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Dkt. Ayoub Kibao, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi na Mkuu wa Idara ya Tiba wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili  (MUHAS) ambaye pia ni Mkuu wa Utafiti katika programu ya sikoseli na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Figo, Paschal Ruggajo wakikata utepe kuashiria ufunguzi wa kliniki  maalum ya wagonjwa wenye sikoseli  ambao pia wanakabiliwa na magonjwa ya moyo iliyoko katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete jijini Dar es Salaam. Na Mwandishi Maalum – Dar es Salaam 16/09/2020 Kliniki maalum kwa ajili ya kuhudumia wagonjwa wa sikoseli ambapo wanaokabiliwa pia na magonjwa ya moyo imeanzishwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI). Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kliniki hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Pro. Mohamed Janabi amesema wameshirikiana na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) kupitia Programu yake ya Sikoseli. Prof. Janabi, amesema

Waumini wa Jumba la Ufalme wa Mashahidi wa Yehova waishukuru JKCI kwa kumfanyia upasuaji mkubwa wa moyo na kumbadilisha ‘aortic valve’ ambayo inatoa damu kutoka kwenye moyo kwenda mwilini na kumuwekea valvu nyingine ya chuma muumini wa dhehebu hilo bila ya kumuongezea damu

Image
Mwanakamati wa Halmashauri ya Mahusiano na Hospitali wa Jumba la Ufalme wa Mashahidi wa Yehova, Godliving Makundi akizungumza wakati wa mkutano baina yao na uongozi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) uliofanyika leo jijini Dar es Salaam. Wanakamati hao walitembelea JKCI kwa ajili ya kuwashukuru kwa kumfanyia muumini wa dhehebu hilo upasuaji mkubwa wa moyo wa kubadilisha valvu bila ya kumuongezea damu. Kulia ni Mkurugenzi wa JKCI Prof. Mohamed Janabi. Baadhi ya viongozi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na Wanakamati wa Halmashauri ya Mahusiano na Hospitali wa Jumba la Ufalme wa Mashahidi wa Yehova wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Prof. Mohamed Janabi akizungumza jinsi Taasisi hiyo inavyoheshimu imani za dini mbalimbali wakati wa mkutano baina yao uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akizungumza jambo na Mwanakamati wa Halmashauri ya Mahusiano na Hospitali wa Jumba la Ufalme wa Mash