Posts

Showing posts from October, 2020

TUGHE- JKCI yaishukuru menejimenti ya JKCI kwa uongozi sikivu

Image
Mhadhiri wa chuo kikuu cha Tumaini Dkt. Mtaki akitoa mada ya sheria za kazi  kwa wajumbe wa kikao cha nne cha  baraza la wafanyakazi wa   Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam. Baraza huru na uongozi sikivu wa menejimenti ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)   inayoongozwa na Mkurugenzi Mtendaji, Profesa Mohamed Janabi ni mafanikio makubwa ambayo uongozi wa Baraza la nne la Wafanyakazi wa Taasisi hiyo umejivunia hatua ambayo imetajwa kuimarisha utendaji kazi na kuboresha huduma kwa wananchi. Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo wakati wa kikao cha nne cha   baraza   baraza la wafayakazi kilichofanyika Protea Hotel jijini hapa, Katibu wa chama cha wafanyakazi wa Serikali kuu na Afya (TUGHE)   tawi la   JKCI, Joyce Mugala amesema Menejimenti hiyo imekuwa ikipokea hoja zao na kuzifanyia kazi kwa wakati. “Limekuwa baraza lenye mafanikio, tumeona Mkurugenzi Mtendaji amekuwa akipokea na kufanya yale tunayojadili na kutupa mrejesho kwa

Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) yawa kitivo cha 'kutengeneza' wataalamu mabingwa wa moyo ndani ya nchi

Image
Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi  ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akizungumza na wajumbe wa baraza hilo wakati wa kikao cha  nne cha baraza kilichofanyika leo jijini Dar es salaam. Kulia ni Katibu Msaidizi wa Baraza hilo Renatha Miiruko. Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) imekuwa kitivo mahususi cha ufundishaji wataalamu mabingwa wa moyo ndani ya nchi kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), hivi sasa inatarajia kila mwaka 'kutengeneza'wahitimu 10. Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Profesa Mohamed Janabi amesema hayo leo alipozungumza na waandishi wa habari wakati wa Kikao cha nne cha Baraza la Wafanyakazi wa Taasisi hiyo . Amesema hatua hiyo itaisaidia Tanzania kupata wataalamu mabingwa wa moyo watakaosaidia kuendelea kuimarisha huduma za matibabu hayo nchini. “JKCI ni Taasisi pekee kubwa ya umma inayotoa matibabu haya nchini, lakini hii si hospitali tu, imekuwa pia seh

Madaktari Bingwa watatu wa China waagwa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) baada ya kumaliza muda wao wa kufanya kazi nchini

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi pamoja na wafanyakazi wa taasisi hiyo wakiwa katika picha ya pamoja na madaktari bingwa wa moyo kutoka nchini China mara baada kumaliza kuwaaga kutokana na  muda wao wa kufanya kazi  kwa zaidi ya miaka miwili katika Taasisi hiyo kumaliza. Mwezi wa sita mwaka 2018 Serikali ya China ilitoa madaktari bingwa kuja kufanya kazi hapa nchini wakiwemo madaktari bingwa watatu wa magonjwa ya moyo. Na Mwandishi Maalum – Dar es Saam Oktoba 16, 2020 Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), imewaaga madaktari bingwa watatu wa magonjwa ya moyo ambao walitolewa na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China kuja Tanzania kutoa huduma za matibabu ya moyo. Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China kila baada ya miaka miwili huwa inatoa wataalamu wake kwenda nchi mbalimbali Barani Afrika kutoa huduma za matibabu. Madaktari hao akiwamo   daktari bingwa wa wagonjwa walioko katika chumba cha uangalizi maalum (ICU), daktari bingwa wa m

Warembo wa Miss Tanzania kutengeneza maktaba ya watoto Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)

Image
Miss Tanzania (2000) Jacqueline  Mengi akimsikiliza Winifrida Kusekwa ambaye mtoto wake Collean Yakwala amelazwa  katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya matibabu  wakati mamiss  Tanzania wa miaka mbalimbali  walipotembelea Taasisi hiyo leo kwa ajili ya kuona huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa pamoja na kuangalia ni jinsi gani wanaweza kuwasaidia watoto wanaotibiwa katika Hospitali hiyo.  Na Anna Nkinda Warembo waliowahi kushinda taji la Miss Tanzania miaka mbalimbali, wakiongozwa na Miss Tanzania wa mwaka 2000, Jaqueline Ntuyabaliwe wameahidi kutengeneza maktaba na kuweka vitabu kwa ajili ya watoto wanaotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).  Akizungumza mbele ya Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Profesa Mohamed Janabi, Jaqueline amesema mwaka huu anatimiza miaka 20 tangu aliposhinda taji hilo kwa kushirikiana na wenzake ameona vema kutengeneza maktaba hiyo ili kuisadia jamii.   “Nimefika hapa ili kuwasilisha wa

Shinikizo la damu ni tatizo lenye idadi kubwa ya wagonjwa kwa asilimia 70 Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)

Image
Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Sauli Philemon akimpima kiwango cha sukari mwilini mwananchi aliyefika  katika viwanja vya Tanganyika Packers vilivyopo Kawe wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam wakati wa maadhimisho ya siku ya moyo Duniani. Katika maadhimisho hayo wananchi walipata bila malipo huduma za Upimaji,ushauri, matibabu ya moyo na rufaa ya moja kwa moja kwa wale waliokutwa na matatizo ya moyo yaliyohitaji matibabu ya kibingwa. Septemba 30, 2020 - Dar es Salaam Shinikizo la damu ni tatizo linaloongoza kwa kushika namba moja kwa idadi kubwa ya wagonjwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambapo takwimu zinaonesha asilimia 70 wanakabiliwa na tatizo hilo.  Yalielezwa hayo jana na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo wa JKCI, Samweli Rweyemamu alipofanya mahojiano na waandishi wa habari katika Viwanja vya Tanganyika Packers wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Moyo Duniani ambayo hufanyika Septemba 29, kila mwaka.  Dk. Rweyemamu alisema wapo pia wagonjw