Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) yawa kitivo cha 'kutengeneza' wataalamu mabingwa wa moyo ndani ya nchi
Mwenyekiti wa
Baraza la Wafanyakazi ambaye pia ni
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed
Janabi akizungumza na wajumbe wa baraza hilo wakati wa kikao cha nne cha baraza kilichofanyika leo jijini Dar
es salaam. Kulia ni Katibu Msaidizi wa Baraza hilo Renatha Miiruko.
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) imekuwa kitivo mahususi cha ufundishaji wataalamu mabingwa wa moyo ndani ya nchi kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), hivi sasa inatarajia kila mwaka 'kutengeneza'wahitimu 10.
Mkurugenzi Mtendaji wa
JKCI, Profesa Mohamed Janabi amesema hayo leo alipozungumza na waandishi wa
habari wakati wa Kikao cha nne cha Baraza la Wafanyakazi wa Taasisi hiyo .
Amesema hatua hiyo
itaisaidia Tanzania kupata wataalamu mabingwa wa moyo watakaosaidia kuendelea
kuimarisha huduma za matibabu hayo nchini.
“JKCI ni Taasisi pekee
kubwa ya umma inayotoa matibabu haya nchini, lakini hii si hospitali tu,
imekuwa pia sehemu kubwa ya mafunzo kwa madaktari na wauguzi, kwa kuwa sisi si
chuo, ndiyo maana tunashirikiana kwa ukaribu na MUHAS, mwaka huu watahitimu
wataalamu saba na kuanzia mwaka ujao wa masomo tunatarajia watahitimu wataalamu
10,” amesema.
Ameongeza “Kwa mfano
hizi digrii za pili za uzamili kwa mfano ‘masters in cardiology’ ya miaka
miwili, asilimia 96 ya walimu wanatoka JKCI kwa ushirikiano na MUHAS tunatoa
hizi kozi.
“Kuna kozi mpya ya upasuaji
wa kifua ambayo imeanzishwa walimu sita
kati ya wanane wanatoka JKCI, ni hatua kubwa ambayo taasisi imepitia kuwa
kitivo cha ‘uzalishaji’ wataalamu mabingwa wa moyo nchini.
“Zaidi ya asilimia 90
ya wataalamu mabingwa wa moyo nchini hivi sasa wapo JKCI, uwiano kwa nchi zetu
zote Afrika bado si mzuri, kwa mfano sisi ndiyo hospitali kubwa kuliko zote si
tu Tanzania bali katika Ukanda wote huu wa Afrika Mashariki na Kati”,.
“Juhudi zimefanyika
kubwa sasa hivi Dodoma (Hospitali ya Benjamin Mkapa - BMH) imeanzisha kitengo
cha moyo tunashirikiana nao kwa ukaribu vile vile Hospitali ya Rufaa ya KCMC
nayo imeanzisha kitengo na tunafanya nao kazi kwa ukaribu,” amebainisha.
Ameongeza “Hivyo kila
mwaka Tanzania tunatarajia ‘tutazalisha’ madaktari kati ya 10 na 13, hii ni
namba kubwa mno.
Kuhusu Baraza hilo la
wafanyakazi, Prof. Janabi ambaye pia ni Mwenyekiti wake amesema limekuwa la mafanikio likiwaunganisha uongozi
wa juu na wafanyakazi kuweza kufahamu huduma tunazotoa, changamoto ni zipi na
wapi tunaelekea, lina wawakilishi 62 kutoka kila idara.
“Tunajivunia utulivu
mkubwa uliopo kwenye Baraza hili, menejimenti inaongoza wafanyakazi 310 na wote
wanahitaji kupata huduma wanazostahili ili wananchi wapate huduma ambazo nchi
inafikiria kuzitoa kwao.
Awali, Katibu wa baraza
la wafanyakazi Dk. Samwel Rweyemamu
amesema baraza hilo limekuwa likihakikisha linasimamia kwa dhati maslahi ya
wafanyakazi ili kuimarisha morali ya utendaji kazi kwa maslahi mapana ya
wananchi wanaowahudumia.
“Kwa mfano kila mwaka tumekuwa tukitambua mfanyakazi bora, tumependekeza pia iwe wafanyakazi watatu bora kila mwaka, yaani mshindi wa kwanza, pili na tatu ili kuwapa motisho na hamasa wafanyakazi kuendelea kufanya vema zaidi,” amebainisha.
Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifuatilia mada ya sheria za kazi wakati wa kikao cha nne cha baraza hilo kilichofanyika leo jijini Dar es salaam.Jumla ya wajumbe 59 walihudhuria kikao hicho.
Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mary Haule akiuliza swali wakati wa kikao cha nne cha baraza la wafanyakazi wa Taasisi hiyo kilichofanyika leo jijini Dar es salaam.
Mfanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Roberth Luchemba akichangia mada ya sheria za kazi wakati wa kikao cha nne cha baraza la wafanyakazi wa Taasisi hiyo kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam. Jumla ya wajumbe 59 walihudhuria kikao hicho.
Comments
Post a Comment