TAARIFA KWA UMMA

TAHADHARI KUHUSU WAGONJWA WANAOCHANGISHA FEDHA ZA MATIBABU YA MOYO KWA AJILI YA KUTIBIWA KATIKA TAASISI YA MOYO JAKAYA KIKWETE (JKCI) 

Uongozi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) unapenda kuutahadharisha Umma kuwa waangalifu na wagonjwa wanaochangisha fedha kwa ajili ya kutibiwa katika Taasisi hii. Ndugu Mwananchi, inawezekana wagonjwa hao wanaochangisha fedha za matibabu wanakuwa tayari wamepata msamaha wa matibabu kutoka kwa Taasisi au wasamaria wema wamewalipia.

Kama utakutana na tangazo la aina hiyo kabla hujamsaidia mhusika tafadhali wasiliana na uongozi wa Taasisi kupitia namba 0222152392/0782-042010/0688-027982 ili kupata ufafanuzi.


Imetolewa na:



Anna Nkinda
Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
19/06/2020


Comments

Popular posts from this blog

JKCI na Burkina Faso zasaini makubaliano ya ushirikiano katika kutoa tiba ya magonjwa ya moyo

Wanawake waaswa kulinda mioyo yao, kuepuka sukari na chumvi kupita kiasi

Msumbiji kushirikiana na JKCI katika tiba ya moyo