WASAMARIA WEMA WAJITOKEZA KUCHANGIA GHARAMA ZA MATIBABU KWA WATOTO WAWILI WANAOTIBIWA JKCI


Mkuu wa kitengo cha Ustawi wa Jamii na Lishe wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Asha Salum akimkabidhi Mr. Jackson Msilambo Tsh. 4,370,000/= zilizotolewa na Mchungaji Rose Shaboka kutoka kanisa la New Day Church kwa ajili ya gharama za matibabu ya mtoto wake anayetibiwa JKCI. 


Baba wa mtoto anayetibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mr. Jackson Msilambo akimpa mkono wa shukrani Mchungaji Rose Shaboka kutoka kanisa la New Day Church baada ya kukabidhiwa Tsh. 4,370,000 kwa ajili ya gharama za matibabu ya mtoto wake anayetibiwa JKCI.


Mchungaji wa kanisa la New Day Church Rose Shaboka akimjulia hali mtoto wa Jackson Msilambo baada ya kuchangia gharama za matibabu ya mtoto huyo anayetibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI). Pia Mchungaji Rose amechangia kiasi cha Tsh. 500,000/= kama gharama za matibabu pamoja na gharama za kupatiwa bima ya afya kwa mtoto mwingine anayetibiwa JKCI.

Comments

Popular posts from this blog

Wateja wa CRDB kutibiwa JKCI kwa punguzo la asilimia 50%

Wanawake wa JKCI SACCOS wanaongoza kwa kumiliki hisa

JKCI, MOI NA MNH waitwa Comoro kutoa huduma za matibabu ya kibingwa