Posts

Showing posts from March, 2021

Hakikisheni huduma za matibabu ya moyo za kibingwa zinawafikia wananchi walioko vijijini – Mhe. Nyongo

Image
  Kamati ya kudumu ya Bunge ya huduma na maendeleo ya Jamii imeitaka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kuhakikisha huduma za matibabu ya moyo za kibingwa wanazozitoa zinawafikia wananchi walioko vijijini. Agizo hilo limetolewa jana na Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Stanslaus Nyongo wakati akizungumza na menejimenti ya Taasisi hiyo mara baada ya kumaliza ziara ya kukagua matumizi ya fedha zinazotolewa na  Serikali kama zinatumika ipasavyo pamoja na kuona huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa. Mhe. Nyongo ambaye pia ni Mbunge wa Maswa Mashariki alisema kamati yake  imeridhishwa na huduma zinazotolewa na Taasisi hiyo na kuishukuru Serikali kwa kuanzisha kituo hicho kinachotoa huduma za kimataifa ambacho kimekuwa mkombozi na kuwasaidia  watu wengi wakiwemo watanzania na  wasio watanzania. Alisema huko vijijini kuna watu wakiwemo watoto wanamatatizo ya moyo ni vyema nao wakapata  huduma za matibabu hayo ambazo hivi sasa zinapatikana hapa nchini. Pia wananchi waelimishwe kuhusu mag

Fanyeni kazi zenu za kuokoa maisha ya wagonjwa kwa kumtanguliza Mungu kwanza– Mchungaji Rose Shaboka.

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Klabu ya Simba Barbara Gonzalez akizungumza na wanawake wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa sherehe ya kuadhimisha siku ya wanawake Duniani iliyofanyika tarehe 08/03/2021 katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti wa chama cha wanawake wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Angella Muhozya akiwapongeza wanawake wa JKCI kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kutoa huduma kwa wagonjwa wanaotibiwa katika taasisi hiyo wakati wa sherehe ya kuadhimisha siku ya wanawake Duniani iliyofanyika tarehe 08/03/2021 katika Taasisi hiyo. Mtaalam wa afya ya Jamii kutoka Doctor’s Plaza Polyclinic Sophia Byanaku akiwapa motisha wanawake wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa sherehe ya kuadhimisha siku ya wanawake Duniani iliyofanyika tarehe 08/03/2021 katika Taasisi hiyo. Mchungaji kutoka kanisa la New Day Church Rose Shaboka akizungumza na wanawake wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa sherehe ya kuadhimisha siku ya wanawak

Hakikisheni watoto wanapata tiba sahihi pindi wanapougua – Mtaalamu kutoa PASS

Image
Kikundi cha wanawake kutoka Taasisi binafsi ya kuwezesha Sekta ya Kilimo Tanzania (PASS) wakimsikiliza mama ambaye mtoto wake amelazwa katika wodi ya watoto wenye magonjwa ya moyo walipotembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kulipia gharama za upasuaji kwa watoto wawili, kuwakatia kadi za bima watoto kumi pamoja na kutoa mahitaji madogo madogo kwa watoto waliolazwa katika wodi hiyo leo Jijini Dar es Salaam.  Mama ambaye mtoto wake anasumbuliwa na maradhi ya moyo Anganile Mwaisaka akitoa machozi ya furaha baada ya kikundi cha wanawake kutoka Taasisi binafsi ya kuwezesha Sekta ya Kilimo Tanzania (PASS) kutoa msaada wa Tshs. 2,000,000 ambazo ni gharama za kufanyiwa upasuaji wa moyo kwa mtoto huyo leo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Jijini Dar es Salaam. Meneja Rasilimali watu na Utawala kutoka Taasisi binafsi ya kuwezesha Sekta ya Kilimo Tanzania (PASS) Elita Naimani pamoja na Mkuu wa Idara ya  Watoto wenye magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwe

Jumla ya watu 561 wamepimwa viashiria vya magonjwaya moyo bila malipo katika upimaji maalumuliofanywa na wataalamu wa magonjwa ya moyo wanawake waTaasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)

Image
Mtunza kumbukumbu za afya kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Nuru Muhidini akimjazia fomu kwa ajili ya kufanyiwa vipimo vya afya ya moyo mkazi wa Mbagala wakati wataalam wa afya wanawake wa Taasisi hiyo walipokuwa wakitoa huduma ya vipimo hivyo bila malipo leo kwenye Viwanja wa Mbagala Zakheem katika kuadhimisha siku ya Wanawaje Duniani. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hildergard Karau akimpima shinikizo la damu makazi wa Mbagala aliyefika katika viwanja vya Mbagala Zakheem leo kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi wa afya ya moyo uliofanywa na wataalam wa afya wanawake wa JKCI katika kuadhimisha siku ya Wanawake Duniani. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Getrude Yombo akimpima wingi wa sukari mwilini mkazi wa Mbagala aliyefika katika viwanja vya Mbagala Zakheem kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi wa afya ya moyo uliofanywa na wataalam wa afya wanawake wa JKCI kwa muda wa siku mbili wakati wa kuadhimisha siku ya Wanawake Duniani. Daktari kuto

Wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wawawekea wagonjwa wanne ambao uwezo wa moyo wao kusukuma damu uko chini ya asilimia 50 kifaa cha kuusadia moyo kufanya kazi vizuri (Cardiac Resynchronization Therapy Device – CRT-D)

Image
  Wagonjwa wanne wenye matatizo ya kutanuka kwa moyo, uwezo wa moyo kusukuma damu kuwa chini ya asilimia 50, mfumo wa umeme wa moyo kuwa na shida iliyopelekea moyo kutokufanya kazi sawasawa wamewekewa kifaa cha  kuusadia moyo kufanya kazi vizuri kijulikanacho kitaalamu kwa jina la Cardiac Resynchronization Therapy Device – CRT-D. Wagonjwa hao waliwekewa kifaa hicho katika kambi maalum ya matibabu iliyofanywa  kwa muda wa siku mbili na wataalamu wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo jijini Dar es Salaam. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mtaalamu m bobezi wa moyo na mzibuaji wa mishipa ya damu ya moyo  wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)  ambaye pia ni mratibu wa kambi hiyo Yona Gandye alisema wagonjwa waliowekewa vifaa hivyo mfumo wao wa umeme wa moyo ulikuwa na hitilafu kubwa hali iliyopeleka moyo kushindwa kusukuma damu ya kutosha mwilini. “Wengi wao walikuwa wanalalamika kuchoka kutwa nzima na hivyo  kushindwa kufanya shughuli zao vizuri na

Upimaji wa magonjwa ya moyo katika viwanja vya mbagala Zakheem Tarehe 4-5/03/2021

Image
 

Wachezaji 24 wa Timu ya Serengeti Boys wapimwa vipimo vya Moyo

Image
Mtaalam kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Nuru Lugawa akimpima uzito na urefu mchezaji wa timu ya taifa chini ya miaka 17 Serengeti Boys Mohamed Mbarak wakati wachezaji wa timu hiyo walivyofika JKCI kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi wa afya ya moyo kabla ya kushiriki mashindano ya kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) yatakayofanyika nchini Morocco katikati ya mwezi mwezi huu. Mtaalam kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Nuru Lugawa akimpima uzito na urefu mchezaji wa timu ya taifa chini ya miaka 17 Serengeti Boys Mohamed Mbarak wakati wachezaji wa timu hiyo walivyofika JKCI kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi wa afya ya moyo kabla ya kushiriki mashindano ya kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) yatakayofanyika nchini Morocco katikati ya mwezi mwezi huu. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Gudila Swai akimpima shinikizo la damu mchezaji wa timu ya taifa chini ya miaka 17 Serengeti Boys Silverster Otto wakati wachezaji wa timu hiyo walipofika JKCI kwa ajili ya