Fanyeni kazi zenu za kuokoa maisha ya wagonjwa kwa kumtanguliza Mungu kwanza– Mchungaji Rose Shaboka.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Klabu ya Simba Barbara Gonzalez akizungumza na wanawake wa Taasisi
ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa sherehe ya kuadhimisha siku ya wanawake
Duniani iliyofanyika tarehe 08/03/2021 katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar
es Salaam.
Mtaalam wa afya ya Jamii kutoka Doctor’s Plaza Polyclinic Sophia Byanaku akiwapa motisha wanawake wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa sherehe ya kuadhimisha siku ya wanawake Duniani iliyofanyika tarehe 08/03/2021 katika Taasisi hiyo.
Mchungaji
kutoka kanisa la New Day Church Rose Shaboka akizungumza na wanawake wa Taasisi
ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa sherehe ya kuadhimisha siku ya wanawake
Duniani iliyofanyika tarehe 08/03/2021 katika Taasisi hiyo.
Baadhi
ya wanawake wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifuatilia mada
mbalimbali zilizokuwa zikiendelea wakati wa sherehe ya kuadhimisha siku ya
wanawake Duniani iliyofanyika tarehe 08/03/2021 katika Taasisi hiyo.
Baadhi
ya wanawake wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakicheza muziki wakati wa
sherehe ya kuadhimisha siku ya wanawake Duniani iliyofanyika tarehe 08/03/2021 katika
Taasisi hiyo.
Wahudumu
wa afya nchini wametakiwa kufanya kazi yao ya kuokoa maisha ya wagonjwa kwa kumtanguliza Mungu kwanza kwani wamebeba dhamana ya maisha ya
watu.
Wito
huo umetolewa hivi karibuni na mchungaji Rose Shaboka wa kanisa la New Day
Church wakati akizungumza na wanawake wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
katika sherehe ya maadhimisho ya siku ya
wanawake Duniani yaliyofanyika katika Taasisi hiyo.
Mchungaji
Rose alisema wahudumu wa afya ni watu wa muhimu sana katika jamii na hata
biblia inawatambua kutokana na huduma ya
matibabu wanayoitoa hata Luka ambaye alikuwa mwanafunzi wa Yesu alikuwa ni tabibu.
“Dhamana
ya uhai wa maisha ya watu mliyoibeba ni kubwa,kama mtakosea kumtibu
mgonjwa na kumpa dozi isiyo sahihi
atapoteza maisha fanyeni kazi yenu mkijua kuwa mnamtumikia Mungu ambaye atawalipa kutokana na huduma
mnayoitoa”,.
“Kataeni
kutumika kufanya mambo ambayo ni kinyume na maadili yenu ya kazi kama vile Farao alivyotaka kuwatumia wakunga kuwaua
watoto wa kiume wa Israel wakati wanawazalisha wanawake wa kiebrabia lakini
wakunga hao walikataa na kufuata taratibu zao za kazi na hawakuwaua watoto
wale”, alisema Mchungaji Rose.
Alisema
amekuwa akifurahia kuwasaidia watoto wanaotoka katika familia zisizokuwa na
uwezo na kuwalipia gharama za matibabu
kwani yeye ni mama na ana watoto ndiyo
maana anasaidia watoto tangu mwaka 2020 alianza kutoa huduma hiyo.
Mchungaji
Rose pia aliwaambia kina mama hao kuijuilsha jamii inayowazunguka siyo magonjwa
yote yanaponywa katika maombi bali kuna magonjwa mengine ni lazima yatibiwe katika
vituo vya kwani hivi sasa kuna maadhi ya
watu wanafikiri wakiumwa watapona Kanisani na siyo Hospitali.
Kwa
upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa klabu ya Simba Barbara Gonzalez alisema mwanamke akipewa nafasi ya uongozi
anaweza kuongoza na kupata mafanikio
mazuri hii ni kutokana na changamoto
mbalimbali za maisha wanazokabiliana nazo kila siku.
Barbara
alisema wakati anaanza kufanya kazi katika klabu hiyo kubwa barani Afrika kuna
baadhi ya watu walimbeza na kusema hataweza kufanya kitu chochote lakini kwa miezi
michache aliyofanya hapo mafanikio makubwa yamepatikana ameonesha anawezana ataendelea kusonga mbele.
“Jambo
la muhimu ni kutokukata tamaa angalia watu wengine wanaofanya vitu vizuri
jifunze kutoka kwao, siyo kitu rahisi kufanya kazi wewe ndiye unayetengeneza
mazingira na mahusiano mazuri na wenzako vitu ambavyo vitakufanya ufanikiwe”, .
“Nitakuwa
mfano kwa wasichana wadogo nitajitahidi kuwasaidia ili wajifunze kutoka kwangu na
kupata uzoefu hii itawafanya waweze kujiamini na kuamini hapo baadaye watakuwa
viongozi wazuri”,alisema Barbara.
Alisema katika sekta ya michezo nchini na
Barani Afrika klabu ya Simba ni mfano mzuri wa kuigwa kwa kuwajali wanawake na
kuwapa uongozi yeye akiwa ni mfano mmojawapo na hivi karibuni walimchagua mwanamke kuwa
kiongozi wa Simba Queens ambaye wanaamini atakuza sekta hiyo ya mpira wa miguu
kwa wanawake.
Naye
mtaalamu wa Afya ya Jamii kutoka Doctor’s Plaza Polyclinic Sophia Byanaku
aliwapongeza wanawake wa hao wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete kwa kazi ngumu wanayoifanya ya kuokoa maisha
ya watu.
Sophia
alisema jambo la muhimu ni kuwaelimisha wanawake wanaotibiwa au kuuguza ndugu
zao wanaotibiwa katika Taasisi hiyo kutumia mitandao ya kijamii kufanya mambo yenye
tija ambayo yatawaletea mafanikio katika familia zao.
“Hivi
sasa wanawake wengi wanacheza michezo mbalimbali ya fedha hii ikiwa ni pamoja
na ujenzi , kununua vyombo, nguo na vitu vingine lakini wakipata matatizo ya
kiafya wanakosa kupata huduma kwa wakati kwa kuwa hawana bima za afya”,.
“Wakati
umefika sasa tuwaelimishe wanawake wenzetu wacheze pia michezo ya kuchangiana
fedha kwa ajili ya kukata bima za afya ili pindi watakapoumwa waweze kupata
huduma za matibabu kwa wakati kuliko kuanza kuchangisha fedha za kusaidiwa
kulipia gharama za matibabu”, alisisitiza Sophia.
Comments
Post a Comment