Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) yanunua mashine mbadala ya mapafu na moyo (Heart lung machine) itakayotumika wakati wa upasuaji mkubwa wa kusimamisha moyo yenye thamani ya shilingi 383,596,000/=.
Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) David Wapalila akiwa ameishika mashine mbadala ya mapafu na moyo (Heart lung machine) itakayotumika wakati wa upasuaji mkubwa wa kusimamisha moyo. Mashine hiyo ya kisasa yenye thamani ya shilingi 383,596,000/= imenunuliwa na Taasisi hiyo kwa ajili ya kuboresha huduma za upasuaji wa moyo. JKCI ina jumla ya mashine za aina hiyo nne. Picha ya mashine mbadala ya mapafu na moyo (Heart lung machine) itakayotumika wakati wa upasuaji mkubwa wa kusimamisha moyo ambayo Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) imeinunua kwa thamani ya shilingi 383,596,000/= kwa ajili ya kuboresha huduma za upasuaji wa moyo.