Posts

Showing posts from May, 2022

Wananchi 437 wamefanyiwa uchunguzi wa magonjwa ya moyo na kisukari ambapo asilimia 60 wamekutwa na matatizo

Image
Mwananchi wa Halmashauri ya Chalinze akisoma jarida la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa upimaji maalum unliofanywa kwa wananchi hao kwa ajili ya kuchunguza magonjwa ya moyo na kisukari katika Hopitali ya  Halmashauri hiyo iliyopo Msoga  wilayani Bagamoyo mkoani Pwani. Afisa kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Aliston Jovin akiwagawia vipeperushi vinavyoelezea huduma za matibabu zinazotolewa na JKCI wananchi waliofika katika Hospitali ya Halmashauri ya Chalinze iliyopo Msoga kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi wa magonjwa ya moyo uliofanywa na wataalam wa moyo kutoka JKCI katika Halmashauri hiyo iliyopo wilayani Bagamoyo mkoani Pwani. Afisa Uuguzi kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Rahabu Tamba akimpima urefu na uzito mwananchi aliyefika katika Hospitali ya Halmshauri ya Chalinze iliyopo Msoga wilayani Bagamoyo kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa magonjwa ya moyo uliokua ukifanywa na wataalam wa moyo kutoka JKCI kwa wananchi wa Chalinze.  Daktari kutoka Taas

Daktari bingwa wa moyo aonya madhara yatokanayo na kuacha kutumia dawa za presha

Image
Mganga Mkuu wa Hospitali ya Halmashauri ya Chalinze Dkt. Allen Mlekwa akiwatambulisha wataalam wa afya kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa wananchi wa Chalinze kabla ya kuanza kwa upimaji wa magonjwa ya moyo na kisukari unaofanyika  katika Hospitali ya Halmashauri ya Chalinze ya Msoga Mkoani Pwani.  Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Anna Nkinda akitoa elimu ya magonjwa ya moyo na namna ya kuyaepuka kwa wananchi wa Halmashauri ya Chalinze kabla ya kuanza kwa upimaji wa magonjwa ya moyo na sukari unaofanywa na wataalam wa JKCI katika Hospitali ya Halmashauri ya Chalinze iliyopo Msoga Mkoani Pwani.  Meneja wa kampuni ya waingizaji wa wasambazaji wa dawa za binadamu ya Sun Pharma nchini Tanzania Sapajan Sorajam akiwaambia wananchi dawa ambazo kampuni hiyo itazitoa bila malipo kwa watu watakaokutwa na magonjwa ya moyo, kisukari na shinikizo la juu la damu wakati wa upimaji uliyofanywa na wataalam wa JKCI kwa wananchi wa H

Wataalamu wa magonjwa ya moyo kufanya upimaji wa moyo na kisukari bila malipo

Image

Wataalamu wa moyo waongezewa ujuzi wa jinsi ya kufanya kipimo cha kuangalia moyo unavyofanya kazi kwa kutumia mashine ya Echocardiogram (ECHO).

Image
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tatizo Waane akizungumza na washiriki wa mafunzo ya upimaji wa moyo wa kuchunguza wagonjwa ambao mioyo yao imeshindwa kufanya kazi vizuri kwa kutumia mashine ya Echocardiogram yaliyotolewa na kampuni ya usambazaji wa mashine za Echo ya Mindray iliyopo nchini China. Mafunzo hayo yalitolewa jana katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Meneja mfumo wa picha za matibabu kutoka kampuni ya usambazaji wa mashine za Echo ya Mindray iliyopo nchini China Li Li akiwafundisha madaktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) namna ya kuwachunguza wagonjwa ambao mioyo yao imeshindwa kufanya kazi vizuri kwa kutumia mashine ya Echocardiogram wakati wa mafunzo maalum ya siku moja yaliyotolewa kwa madaktari.    Baadhi ya Madaktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifuatilia mafunzo ya namna ya kuwachunguza wagonjwa ambao mioyo yao imeshindwa kufanya kazi vizuri yaliyokuwa yakitolewa na Men

Madaktari bingwa wa magonjwa ya moyo kufanya upimaji wa kisukari,moyo kwa wananchi wa mkoa wa Pwani

Image

Wauguzi JKCI washiriki bonanza la kuadhimisha siku ya wauguzi

Image
Maafisa Wauguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakivuta kamba wakati wa mashindano ya mchezo huo kati yao na wauguzi wa Hospitali ya Mloganzila uliofanyika leo katika viwanja vya Chuo cha Polisi Kurasini jijini Dar es Salaam ambapo wauguzi wa JKCI walishika nafasi ya pili. Mshindano hayo yalihusisha wauguzi kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Hospitali ya Taifa Muhimbili Upanga na Mloganzila na Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI). Timu ya mpira wa miguu ya maafisa wauguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuanza kwa mchezo baina yao na wauguzi kutoka Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI) Katika mchezo huo timu ya JKCI ilifungwa mabao matatu na timu ya wauguzi kutoka MOI   Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Agnes Lugendo akiwachachafya wachezaji wa timu ya mpira wa pete ya Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI) wakati wa mashindano ya mchezo huo yaliyofanyika leo katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Polisi Kurasini jijini

Ufahamu ugonjwa wa shinikizo la juu la damu

Image
  Mkurugenzi wa Huduma ya Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Robert Mallya akimpima Salome Majaliwa shinikizo la damu (BP) ikiwa ni maadhimisho ya siku ya shinikizo ja juu la damu duniani ambayo kila mwaka hufanyika tarehe 17 mwezi wa tano. Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)   Gudila Swai akionesha mashine inayopima shinikizo la damu (BP) na kiwango cha oxygen mwilini ikiwa ni maadhimisho ya siku ya shinikizo la juu la damu duniani ambayo hufanyika kila mwaka tarehe 17 mwezi wa tano. Mfamasia wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Miraji Dhahiri akiwa ameshika dawa za shinikizo la juu la damu zinazotolewa kwa wagonjwa wanaotibiwa katika taasisi hiyo wakati wa maadhimisho ya siku ya shinikizo la juu la damu duniani ambayo hufanyika kila mwaka tarehe 17 mwezi wa tano. Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa  Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mohamed Aloyce  akimpima Rebecca Kengele ambaye ni msimamizi wa masijala za Taasisi hiyo shinikizo la damu (BP)