Wauguzi JKCI washiriki bonanza la kuadhimisha siku ya wauguzi


Maafisa Wauguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakivuta kamba wakati wa mashindano ya mchezo huo kati yao na wauguzi wa Hospitali ya Mloganzila uliofanyika leo katika viwanja vya Chuo cha Polisi Kurasini jijini Dar es Salaam ambapo wauguzi wa JKCI walishika nafasi ya pili. Mshindano hayo yalihusisha wauguzi kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Hospitali ya Taifa Muhimbili Upanga na Mloganzila na Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI).

Timu ya mpira wa miguu ya maafisa wauguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuanza kwa mchezo baina yao na wauguzi kutoka Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI) Katika mchezo huo timu ya JKCI ilifungwa mabao matatu na timu ya wauguzi kutoka MOI


 Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Agnes Lugendo akiwachachafya wachezaji wa timu ya mpira wa pete ya Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI) wakati wa mashindano ya mchezo huo yaliyofanyika leo katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Polisi Kurasini jijini Dar es Salaam ambapo timu ya JKCI ilifungwa mabao Kumi kwa tisa na timu hiyo.

***********************************************************

Comments

Popular posts from this blog

Wataalamu wa JKCI kufanya upasuaji wa moyo nchini Zambia

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yamshukuru Rais Dkt.Samia kwa kuwapa magari