Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete inafanya upimaji wa magonjwa ya moyo na kisukari katika maonesho ya sabasaba
Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Magonjwa ya Moyo na daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tatizo Waane akimpa kitabu cha jinsi ya kuepukana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza mwananchi aliyetembelea banda la taasisi hiyo mwaka jana kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi wa magonjwa ya moyo wakati wa maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) yaliyofanyika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa. ********************************************************************************************************************************************** ********************************************************************************************************************************************* Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) inapenda kuwajulisha wananchi kuwa inashiriki maonesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam yanayofanyika katika Uwanja wa Maonyesho wa Biashara wa Mwalim...