RC MAKALA: Kampeni ya kupima afya bure imekuwa na mafanikio makubwa







-         Awataka wananchi kuanza matibabu kwa wale waliogundulika na magonjwa yasiyoambukiza

-         Awashukuru Clouds Media Group, Madaktari na wadau wengine waliofanikisha kampeni ya Afya Check

-         Aelekeza uwepo wa Hospitali tembezi kwa madaktari bingwa katika kila Wilaya.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Amos Makalla leo Juni 13 amehitimisha zoezi la siku kumi za upimaji Afya bure ambapo mpaka kufikia siku ya jana Juni 12 zaidi ya wananchi 7,030 walihudumiwa na madaktari bingwa na wabobezi kutoka Hospitali kubwa za Mkoa huo.

Akihitimisha zoezi hilo RC Makalla amesema zoezi hilo limekuwa na mafanikio makubwa ambapo kati ya wananchi 7,030 waliohudumiwa wananchi 1,522 walipima Shinikizo la damu, 247 Kisukari, 808 walipimwa tatizo la moyo, uchangiaji wa damu unit 203, kipimo cha ultrasound 1,726, 189 tezi dume,949 walipata chanjo ya Uviko – 19, 601 walipima Saratani ya shingo ya kizazi, 1,369 walipima tatizo la meno na macho wananchi 1,673.

Kutokana na mwamko kuwa mkubwa, RC Makalla amemuelekeza Katibu Tawala wa Mkoa huo kuanzisha huduma ya Hospitali inayotembea “Mobile hospital” kwa kutumia gari maalum litakalokuwa limesheheni madaktari bingwa.

Aidha RC Makalla ametumia zoezi hilo kutoa wito kwa wananchi kujiwekea utaratibu wa upimaji afya mara kwa mara kutokana na takwimu kuonyesha wananchi wengi waliogundulika kuwa na matatizo ya afya hawakuwa wakitambua.

Hata hivyo RC Makalla amewasisitiza wananchi kufanya mazoezi ili kujiepusha na hatari ya kupata magonjwa yasiyoambukizwa ikiwemo kisukari, shinikizo la damu, saratani na magonjwa mengine.

Pamoja na hayo RC Makalla amewashukuru wadau waliofanikisha zoezi hilo wakiwemo Clouds Media Group kupitia kipindi cha afya check ambao ndio waratibu wa zoezi hilo.



 

Comments

Popular posts from this blog

Wataalamu wa JKCI kufanya upasuaji wa moyo nchini Zambia

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yamshukuru Rais Dkt.Samia kwa kuwapa magari