Afisa muuguzi mstaafu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) akabidhiwa zawadi ya hundi ya shilingi milioni tisa, cheti na ngao kutokana na utumishi wake uliotukuka
Afisa Uuguzi ambaye amestaafu leo kwa mujibu wa sheria za
utumishi wa umma Husna Mzunga akipokea
mfano wa hundi yenye thamani ya Tshs. 9,000,000/= kutoka kwa Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi ikiwa ni
ishara ya kumpongeza kwa utumishi wake
uliotukuka wakati wa hafla fupi ya kumuaga iliyofanyika leo katika ukumbi wa mikutano
wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.
Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Winnie
Masakuya akimlisha keki Afisa Uuguzi mstaafu kutoka JKCI Husna Mzunga wakati wa
hafla fupi ya kumuaga iliyofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa taasisi
hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.
Afisa Uuguzi ambaye amestaafu leo kwa mujibu wa sheria za utumishi wa umma Husna Mzunga akimlisha keki
Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Robert
Mallya wakati wa hafla fupi ya kumuaga iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano
wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es
Salaam.
Afisa Uuguzi ambaye amestaafu leo katika Utumishi wa Umma Husna Mzunga akiwa katika picha ya pamoja na wauguzi wenzake mara baada ya kumalizika kwa hafla fupi ya kumpongeza iliyofanyika leo katika ukumbi wa mikutani wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo jijini Dar es Salaam.
Picha na: JKCI
********************************************************************************************
Comments
Post a Comment