Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi
akizungumza na wafanyakazi wa Taasisi hiyo alipowatembelea katika ofisi yao kwa
ajili ya kusikiliza changamoto wanazopitia katika maeneo yao ya kazi wakati wa kuadhimisha
wiki ya utumishi wa umma leo Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
Prof. Mohamed Janabi akikagua taarifa za mgonjwa anayetibiwa katika Taasisi
hiyo wakati wa kuhitimisha maadhimisho ya wiki ya utumishi wa umma leo Jijini
Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Utawala na Rasilimali watu wa
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Ghati Chacha akimsikiliza mama ambaye
mtoto wake amelazwa katika wodi ya watoto wenye magonjwa ya moyo Fatuma Mohamed
alipotembelea wodi hiyo kwa ajili ya kusikiliza changamoto zinazowakabili
wakati wa kuhitimisha maadhimisho ya wiki ya utumishi wa umma leo Jijini Dar es
Salaam
Mkuu wa Idara ya Rasilimali watu wa Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) Abdulrahman Muya akizungumza na wagonjwa wanaosubiria kufanyiwa
kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (Echocardiograph) wakati wa
kuhitimisha maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma leo Jijini Dar es Salaam.
Mkuu
wa Idara ya Utawala wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Joachim Asenga
akisikiliza hoja mbalimbali zilizokua zikitolewa na wafanyakazi wa Taasisi hiyo
wakati wa kuhitimisha maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma leo Jijini Dar es
Salaam
Afisa
Utawala wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Adila Lugamara akizungumza na
mama wa mtoto aliyelazwa katika wodi ya watoto wenye magonjwa ya moyo Monica
Hussen wakati wa kuhitimisha wiki ya Utumishi wa Umma leo katika Taasisi hiyo
Jijini Dar es Salaam
Mkuu
wa Idara ya Utawala wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Joachim Asenga akimsikiliza
mzazi wa mtoto aliyelazwa katika wodi ya watoto wenye magonjwa ya moyo Zubeda
Dominic wakati wa kuhitimisha maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma leo
Jijini Dar es Salaam
Watumishi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
wakisikiliza hoja mbalimbali kwa wagonjwa walioudhuria kliniki katika Taasisi
hiyo wakati wa kuhitimisha wiki ya Utumishi wa Umma leo katika Taasisi hiyo
Jijini Dar es Salaam.
Picha na: Genofeva Matemu
**********************************************************************************
Comments
Post a Comment