Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete inafanya upimaji wa magonjwa ya moyo na kisukari katika maonesho ya sabasaba
*******************************************************************************************************************************************************************************************************************************************************************************************
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) inapenda kuwajulisha wananchi kuwa inashiriki maonesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam yanayofanyika katika Uwanja wa Maonyesho wa Biashara wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere uliopo barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 28/06/2022 hadi tarehe 13/07/2022.
Katika maonesho haya tunafanya
upimaji wa afya ya moyo kwa watoto na watu wazima. Pia tunatoa
chanjo ya UVIKO-19 kama kinga ya ugonjwa huu pamoja na kufanya kipimo cha kuchunguza
UVIKO -19 (rapid test) kwa wale wanaosumbuliwa na tatizo katika njia ya
kupumulia.
Tuna
wataalamu wa lishe ambao wanatoa elimu ya lishe bora ambayo inawapa wananchi
uelewa na kufuata mtindo bora wa maisha ambao utawasaidia kuepukana na
magonjwa ya moyo na kisukari ambayo ni magonjwa yasiyoambukiza na mtu anaweza
kuyaepuka kwa kufuata ushauri wa kitaalamu wa lishe.
Kwa wale watakaokutwa na matatizo ya moyo watapatiwa matibabu hii ikiwa ni pamoja na kupewa rufaa ya kuja kutibiwa katika Taasisi yetu.
Madaktari wetu mabingwa wa magonjwa ya moyo Peter Kisenge, Tulizo
Shem, Tatizo Waane, Baraka Ndelwa na Pedro Pallangyo chini ya uongozi wa Prof.
Mohamed Janabi watakuwepo katika banda letu kwaajili ya kutoa huduma kwa
wananchi. Nyote mnakaribishwa.
“Tunajali Afya ya moyo yako”.
Imetolewa na :
Anna Nkinda
Mkuu wa
Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano
Taasisi ya
Moyo Jakaya Kikwete
28/06/2022
Comments
Post a Comment