Posts

Showing posts from October, 2021

319 wachunguzwa moyo Dodoma Festival

Image
  Afisa muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Lilian Peter akimsikiliza  mwananchi  aliyetembelea banda la Taasisi hiyo  kwa ajili ya kupata huduma za upimaji na matibabu ya moyo zilizokuwa zinazotolewa na wataalamu wa JKCI  katika tamasha la Karibu Dodoma festival lililofanyika katika viwaja vya Chinangali park jijini Dodoma wakati  akimpima kiwango cha sukari mwilini. Mkuu wa wilaya ya Dodoma Jabir Shekimweri akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wadau wa sekya ya Afya mara baada ya kumalizika kwa tamasha la Karibu Dodoma festival lililofanyika    katika viwanja vya Chinangali park. Tamasha hilo lilienda sambamba na zoezi la upimaji wa afya. Mkuu wa wilaya ya Dodoma Jabir Shekimweri akimkabidhi Mkuu wa kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Anna Nkinda cheti cha ushiriki wa tamasha la Karibu Dodoma festival lililomalizika jana katika viwanja vya Chinangali park. Mhasibu wa Taasisi ya Moyo Ja...

Pinda: Huduma za afya kibingwa zipelekwe kila Kanda

Image
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Dkt. Doroth Gwajima akizungumza kuhusu umuhimu wa kusogeza huduma za matibabu ya kibingwa kwa wananchi alipotembelea  banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kuona huduma za upimaji na matibabu ya moyo zilizokuwa zinazotolewa na wataalamu wa taasisi hiyo katika tamasha la Karibu Dodoma festival lililofanyika katika viwanja vya Chinangali park. Kushoto ni Mkurugenzi wa JKCI Prof. Mohamed Janabi. Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Geophrey Pinda ameiomba wizara ya Afya kusogeza huduma za matibabu ya  kibingwa ya kuwafuata wananchi mahali walipo katika ngazi ya mikoa na kanda kwa kufanya hivyo wananchi wengi watafikiwa na huduma hizo. Pinda ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Kavuu alitoa ombi hilo kwa waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Doroth Gwajima katika tamasha la Karibu Dodoma festival lililofanyika katika viwaja vya Chinangali park ambalo lilikwenda sambamba na zoezi l...

Profesa Janabi: Wahudumu wa afya wawe wa kwanza kuchanja chanjo ya UVIKO – 19

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi ambaye pia ni mhamasishaji wa kitaifa wa mpango wa jamii shirikishi na harakishi wa elimu na uhamasishaji wa  chanjo dhidi ya UVIKO – 19   akitoa elimu ya chanjo hiyo kwa watumishi wa afya wa hospitali ya taifa ya magonjwa ya akili Mirembe na wanafunzi wa chuo cha uuguzi Dodoma kilichopo chini ya hospitali hiyo. Watumishi  wa afya nchini wametakiwa kujitokeza kwa wingi kuchanja chanjo  dhidi ya UVIKO – 19   kwani wapo katika hatari kubwa ya kupata maam b ukizi ya ugonjwa huo kupita wagonjwa wanaowahudumia  ukilinganisha  na watu wengine. Rai hiyo imetolewa leo jijini Dodoma na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi   wakati akitoa elimu ya chanjo kwa watumishi wa afya wa hospitali ya taifa ya magonjwa ya akili Mirembe na wanafunzi wa chuo cha uuguzi Dodoma kilichopo chi n i ya hospitali hiyo. Prof. Janabi ambaye pia ni m...

Madaktari wazawa wa JKCI kwa mara ya kwanza wapandikiza mishipa miwili ya damu katika moyo bila ya kuusimamisha moyo (Off-Pump Coronary Artery Bypass Surgery)

Image
Madaktari wazawa wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa mara ya kwanza wakipandikiza mishipa miwili ya damu katika moyo bila ya kuusimamisha moyo (Off-Pump Coronary Artery Bypass Surgery) kwa mgonjwa ambaye mishipa yake mitatu ya damu ilikua imeziba na uwezo wa moyo kufanya kazi ukiwa umeshuka na kubaki asilimia 27 hivyo kumsababishia kuchoka na kushindwa kufanya kazi leo katika Taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam  

Wafanyakazi bora wa JKCI wapongezwa

Image
Mfanyakazi bora wa robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2021/2022 aliyeshika nafasi ya kwanza Joshua Ogutu  akiunganisha vifaa kwa ajili ya kuwasha mashine ya kumsaidia mgonjwa kupumua (Ventilator) ikiwa ni moja ya majukumu yake ya kazi za kila siku Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kiwete (JKCI) Hildergurd Karau akipokea cheti kwa niaba ya Mfanyakazi bora wa robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2021/2022 aliyeshika nafasi ya pili Afisa muuguzi Mohamed Wamara kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delilah Kimambo wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza wafanyakazi bora leo Jijini Dar es Salaam. Mfanyakazi bora wa robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2021/2022 aliyeshika nafasi ya tatu Kelvin Manyanga akipokea cheti cha mfanyakazi bora kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delilah Kimambo wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza wafanyakazi hao iliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.  

Wananchi waomba huduma za kibingwa za Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)

Image
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Dkt. Doroth Gwajima akiangalia dawa za moyo zinazotolewa bila malipo na  kampuni ya uagizaji na usambazaji wa dawa za binadamu ya Sun Pharmaceutical Industries Ltd. kwa wagonjwa wanaokutwa na matatizo ya moyo waliofika katika banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kupata huduma za upimaji na matibabu ya moyo zinazotolewa na wataalamu wa taasisi hiyo katika tamasha la Karibu Dodoma festival linalofanyika katika viwaja vya Chinangali park jijini Dodoma. ********************************************************************************************************************************************* Na Anna Nkinda Wananchi wa mkoa wa Dodoma wameiomba Serikali kutoa huduma za matibabu ya kibingwa za kuwafuata wananchi mahali walipo mara kwa mara kwa kufanya hivyo wananchi wengi zaidi hasa walioko vijijini watafikiwa na huduma hizo. Ombi hilo limetolewa leo jijini Dodoma na baadhi ya wananchi waliofika kat...

Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete yaibuka kinara matumizi ya Tehama sekta ya Afya

Image
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Zainab Chaula akimkabidhi   Mkuu wa Kitengo cha Tehama wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Raymond Machary  tuzo ya Taasisi ya mabadiliko Tehama bora katika utoaji wa huduma za afya  wakati wa kufunga  kongamano la tano la maafisa TEHAMA Tanzania lililomalizika Jana Jijini Arusha Na: Mwandishi Maalum - Arusha Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) imepewa tuzo ya Taasisi ya mabadiliko Tehama bora katika utoaji wa huduma za afya nchini. Tuzo hiyo imetolewa na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Zainab Chaula wakati wa kongamano la tano la siku tatu kwa maafisa TEHAMA Tanzania lililomalizika Jana Jijini Arusha. Akizungumza wakati wa kufunga kongamano hilo Bi. Chaula alisema kuwa JKCI ni miongoni mwa Taasisi za serikali ambayo inatoa huduma nzuri ya matibabu ya moyo kwa wagonjwa kupitia mifumo ya Tehama.   “Lengo la serikali ni pamoja na kuiwezesha nchi ya...

Maulid day

Image
 

Wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) waongezewa ujuzi wa jinsi ya kutumia mashine ya kuusaidia moyo kufanya kazi kwa kiwango cha juu (Intra-aortic balloon pump) na wakufunzi kutoka nchini Afrika ya Kusini

Image
Mkufunzi wa kutumia mashine ya kuusaidia moyo kufanya kazi kwa kiwango cha juu (Intra-aortic balloon pump) kutoka nchini Afrika Kusini Linda Veale akiwafundisha wataalam wa afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) (hawapo pichani) namna ambavyo mashine hiyo inavyoweza kufanya kazi wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika leo katika ukumbi wa Taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam. Baadhi ya wataalam wa afya kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifuatilia mafunzo ya namna ya kutumia mashine ya kuusaidia moyo kufanya kazi kwa kiwango cha juu (Intra-aortic balloon pump) wakati wa mafunzo hayo ya siku tano yaliyofanyika leo katika ukumbi wa Taasisi hiyo iliyopo Jijini Dar es Salaam. Wataalam wa afya kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakijifunza kwa vitendo namna ya kuunganisha vifaa vya kumuunganisha mgonjwa na mashine ya kuusaidia moyo kufanya kazi kwa kiwango cha juu (Intra-aortic balloon pump) wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika leo katika ukumbi wa Taasisi hiyo Jijini...

Kumbukizi ya kifo cha Baba wa Taifa

Image
 

Watu wengi waliojitokeza kupima magonjwa ya moyo wilayani Kigamboni wamebainika kuwa na shinikizo la juu la damu. Kati ya watu 173 waliopimwa 58 wamethibitika kuwa na tatizo hilo

Image
  Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Zitha Meela akimpima kiwango cha oxygen mwilini mtoto aliyefika katika viwanja vya Hospitali ya wilaya ya Kigamboni kwa ajili ya upimaji wa magonjwa ya Moyo uliofanywa na  wataalamu wa Taasisi hiyo kwa kushirikiana na wenzao wa Kigamboni ikiwa ni maadhimisho ya siku ya moyo Duniani Jumla ya watu 173 wamefanyiwa upimaji wa magonjwa ya moyo wakati wa maadhimisho ya siku ya moyo Duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Hospitali ya wilaya ya Kigamboni iliyopo Gezaulole. Upimaji huo uliofanywa na wataalamu wa magonjwa ya moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana   na wenzao wa Hospitali ya wilaya ya Kigamboni. Watu wote 173 walifanyiwa vipimo vya kuangalia uwiano wa urefu na uzito, wingi wa sukari kwenye damu na shinikizo la damu, waliokutwa na viashiria vya magonjwa ya moyo walifanyiwa vipimo zaidi ambapo   124 walifanyiwa vipimo vya kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (Echocardiogram...

Watu 160 wamefanyiwa upimaji wa magonjwa ya moyo bila malipo wakati wa Upimaji ulioandaliwa na Chama cha Madaktari Tanzania – MAT Mkoani Geita

Image
Baadhi ya wananchi wa Mkoa wa Geita wakiwa katika foleni ya kuingia katika banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete  (JKCI) kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi wa magonjwa ya moyo wakati wa kambi maalum ya matibabu iliyoandaliwa na Chama cha Madaktari Tanzania (MAT)  Watu 160 wamefanyiwa upimaji wa magonjwa ya moyo bila malipo wakati wa upimaji ulioandaliwa na chama cha Madaktari Tanzania (MAT) uliofanyika katika viwanja vya Hospitali ya Mkoa wa Geita na kumalizika jana.   Upimaji huo wa siku tatu ulifanywa na wataalam wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na kutoa rufaa kwa wagonjwa 14 Waliobainika kuwa na magonjwa mbalimbali ya moyo.  Akizungumza wakati wa upimaji huo Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Theophylly Mushi alisema upimaji uliofanyika ni wa kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi na mabadiliko ya ndani ya muundo wa kuta za moyo unaosababishwa na shinikizo la damu (Echocardioghraphy – ECHO), kuchunguza jinsi umeme wa moyo unavyofanya kazi...