Mpango mkakati wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete kwa kipindi cha miaka mitano ijayo ni kutoa huduma bora zaidi kwa wananchi



Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akifunga kikao cha viongozi wa taasisi hiyo kwa ajili ya kutoa maoni juu ya rasimu ya mpango mkakati wa pili wa utendaji kazi wa Taasisi hiyo utakaotumika kwa kipindi cha miaka mitano ijayo kuanzia mwaka wa fedha 2022/23 Jana Jijini Dar es Salaam
Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambaye pia ni miongoni mwa wanakamati wa rasimu ya mpango mkakati Pedro Pallangyo akielezea baadhi ya vitu vilivyopo katika rasimu ya mpango mkakati wa pili wa utendaji kazi wa Taasisi hiyo wakati wa kikao cha kutoa maoni juu ya rasimu ya mpango mkakati huo utakaotumika kwa kipindi cha miaka mitano ijayo kuanzia mwaka wa fedha 2022/23 Jana Jijini Dar es Salaam

Mkurugenzi wa Fedha na Mipango wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) CPA Agnes Kuhenga akitoa ufafanuzi wakati wa kikao cha kutoa maoni juu ya rasimu ya mpango mkakati wa pili wa utendaji kazi wa Taasisi hiyo utakaotumika kwa kipindi cha miaka mitano ijayo kuanzia mwaka wa fedha 2022/23 Jana Jijini Dar es Salaam

Mkuu wa Kitengo cha Mipango wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambaye pia ni miongoni mwa wanakamati wa rasimu ya mpango mkakati Vida Mushi akielezea baadhi ya vitu vilivyopo katika rasimu ya mpango mkakati wa pili wa utendaji kazi wa Taasisi hiyo wakati wa kikao cha kutoa maoni juu ya rasimu ya mpango mkakati huo utakaotumika kwa kipindi cha miaka mitano ijayo kuanzia mwaka wa fedha 2022/23 Jana Jijini Dar es Salaam

Mkuu wa Kitengo cha Ununuzi na Ugavi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Daniel Bunare akichangia hoja wakati wa kikao cha kutoa maoni juu ya rasimu ya mpango mkakati wa pili wa utendaji kazi wa Taasisi hiyo utakaotumika kwa kipindi cha miaka mitano ijayo kuanzia mwaka wa fedha 2022/23 Jana Jijini Dar es Salaam

Mfamasia wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete ambaye pia ni miongoni mwa wanakamati wa rasimu ya mpango mkakati Nelson Njau akielezea baadhi ya vitu vilivyopo katika rasimu ya mpango mkakati wa pili wa utendaji kazi wa Taasisi hiyo wakati wa kikao cha kutoa maoni juu ya rasimu ya mpango mkakati huo utakaotumika kwa kipindi cha miaka mitano ijayo kuanzia mwaka wa fedha 2022/23 Jana Jijini Dar es Salaam

Baadhi ya viongozi wa Idara na Vitengo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifuatilia mawasilisho mbalimbali wakati wa kikao cha kutoa maoni juu ya rasimu ya mpango mkakati wa pili wa utendaji kazi wa Taasisi hiyo utakaotumika kwa kipindi cha miaka mitano ijayo kuanzia mwaka wa fedha 2022/23 Jana Jijini Dar es Salaam

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi katika picha ya pamoja na viongozi wa taasisi hiyo na wanakamati wa rasimu ya mpango mkakati wa pili wa utendaji kazi wa Taasisi hiyo baada ya kikao cha kutoa maoni juu ya rasimu ya mpango mkakati huo utakaotumika kwa kipindi cha miaka mitano ijayo kuanzia mwaka wa fedha 2022/23 Jana Jijini Dar es Salaam


XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX


 Wakurugenzi wa Idara na wakuu wa vitengo  wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wametakiwa kuwa mfano wa kuigwa na hospitali nyingine nchini pamoja na watumishi wanaowaongoza kwa kutekeleza majukumu yao kulingana na mpango mkakati wa utendaji kazi wa taasisi hiyo kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.

Kutekeleza kwao mpango mkakati huo kutasaidia kuboresha huduma za matibabu ya moyo na kuweza kutoa huduma zote za kibingwa za magonjwa hayo hapa nchini.

Rai hiyo imetolewa jana na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi wakati wa kikao cha viongozi hao kilichofanyika jijini Dar es Salaam kwa ajili ya  kutoa maoni juu ya  rasimu  ya mpango mkakati wa pili wa utendaji kazi wa Taasisi hiyo utakaotumika kwa kipindi cha miaka mitano ijayo kuanzia mwaka wa fedha ujao wa 2022/23.

Prof. Janabi alisema rasimu ya mpango mkakati huo wa kazi imeeleza kazi ambazo kila idara na kitengo zinatakiwa kufanya na imewashirikisha wafanyakazi wote kwa ajili ya kuweka maoni yao lakini pia rasimu hiyo imeandaliwa na baadhi ya wafanyakazi wa JKCI jambo ambalo litarahisisha utendaji kazi wa Taasisi hiyo.

“Nimefurahishwa na viongozi wote kwa pamoja jinsi mlivyoshirikiana kuweka mawazo yenu katika kuboresha rasimu hii ya kwanza ya mpango mkakati itakayoanza kutumika mwaka 2022/2023 hadi mwaka 2026/2027 tukiwa na lengo la kuendelea kuboresha huduma zetu lakini pia kutoka hapa tulipo na kuweza kutoa huduma zote za kibingwa za magonjwa ya moyo”,.

“Mpango mkakati huu ukianza kutumika ni vyema tukajiwekea malengo kwamba kila jukumu lililowekwa linafanyika kwa wakati husika na kumalizika kwa wakati kwa kufanya hivyo ninahakika baada ya miaka mitano ijayo tutakuwa tumefikia malengo yetu kwa asilimia mia moja”, alisema Prof. Janabi

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Fedha na Mipango CPA Agnes Kuhenga aliwashukuru wanakamati walioandaa rasimu hiyo ya mpango mkakati wa pili kwa mawazo na maoni yao ambayo yameweza kutoa rasimu inayokidhi vigezo vya kada zote zilizopo katika taasisi hiyo.

“Mpango mkakati huu utakapokamilika na kuanza kutumika bado utaendelea kupitiwa mara kwa mara ili yale yaliyoainishwa yaweze kufanyika kwa vitendo na hivyo kuboresha zaidi huduma tunazozitoa katika Taasisi yetu",.

“Leo katika kikao hiki cha kupitia rasimu ya kwanza ya mpango mkakati wa pili wa utendaji kazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete tumechukua tena mawazo ya viongozi walioshiriki kikao hiki ambayo tutaenda kuyafanyia kazi katika kuboresha rasimu hii na kutoa rasimu ya pili”, alisema CPA Agnes.

Naye Mkuu wa Kitengo cha Mipango wa Taasisi hiyo Vida Mushi alisema kushirikishwa kwa watendaji katika uandaaji wa mpango mkakati wa utendaji kazi za kila siku kunamsaidia mtumishi kutekeleza majukumu yake kirahisi kwani anakuwa na ufahamu wa nini anatakiwa kufanya.

“Kushirikishwa kwangu kuandaa mpango mkakati huu na kutoa maoni yangu kutaturahisishia mimi na wafanyakazi wenzangu kutekeleza majukumu yetu ya kila siku kwasababu kumenipa ufahamu mkubwa hivyo itakua rahisi pale ufuatiliaji na tathmini utakapofanyika”, alisema Vida.



Comments

Popular posts from this blog

Wataalamu wa JKCI kufanya upasuaji wa moyo nchini Zambia

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yamshukuru Rais Dkt.Samia kwa kuwapa magari