Maktaba ya watoto Hospitalini itawajenga kupenda kusoma kuliko kuogopa matibabu
Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi
akimwelezea namna taasisi hiyo inavyofanya kazi Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya
Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Jim Yonazi alipofanya ziara
katika taasisi hiyo jana kwa ajili ya kuangalia huduma zinazotolewa.
Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Jim
Yonazi akimjulia hali mtoto aliyelazwa katika wodi ya watoto wenye magonjwa ya
moyo wakati wa ziara yake ya kutembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) jana
kwa ajili ya kuangalia huduma zinazotolewa na Taasisi hiyo .
Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Jim
Yonazi akiangalia maktaba ya watoto wanaotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) wakati wa ziara yake ya kutembelea taasisi hiyo kwa ajili kuangalia
huduma zinavyotolewa.
Mkuu
wa Kitengo cha TEHAMA wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Raymond Machari
akimuonesha Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya
Habari Dkt. Jim Yonazi ujumbe ufupi wa simu kutoka kwa wananchi wanaopatiwa
huduma kupitia namba maalum ya kufikisha maoni ya wananchi wakati wa ziara yake
aliyoifanya katika taasisi hiyo kwa ajili ya kuangalia huduma zinazotolewa.
Afisa muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) anayefanya kazi katika mtambo wa Cathlab Rydiness Mulashani akimwelezea huduma za uchunguzi, upasuaji mdogo wa moyo pamoja na upandikizaji wa vifaa visaidizi vya moyo zinazotolewa katika chumba hicho Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Jim Yonazi alipofanya ziara katika taasisi hiyo kwa ajili ya kuangalia huduma zinazotolewa.
Mkuu wa Kitengo cha Ununuzi na Ugavi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Daniel Bunare akimwelezea Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Jim Yonazi namna ambavyo mfumo wa manunuzi unavyotumiwa na taasisi hiyo katika manunuzi mbalimbali wakati wa ziara yake ya kutembelea taasisi hiyo kwa ajili ya kuangalia huduma zinazotolewa.
Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Jim
Yonazi akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) na watendaji wa wizara hiyo mara baada ya kumaliza ziara yake ya
kuangalia huduma zinazotolewa na JKCI jana
Jijini Dar es Salaam kulia kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Prof. Mohamed
Janabi.
Kuwepo
kwa maktaba za watoto katika Hospitali kunawajenga kiakili siyo kwamba
wanakwenda kupata matibabu peke yake bali pia wanapata elimu ya darasani
kwa muda wanaopata au kusubiri tiba.
Hayo
yamesemwa jana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na
Teknolojia ya Habari Dkt. Jim Yonazi alipofanya ziara ya kutembelea Taasisi ya
Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kuangalia huduma zinazotolewa na
kuwakuta watoto wakiwa katika maktaba wanajisomea.
Dkt.
Yonazi alisema hakuwahi kufikiria kwamba hospitali inaweza kuwa na maktaba
ambayo itawawezesha wagonjwa wakiwemo watoto kusoma vitabu wakati wakisubiri
kupata matibabu au wakiendelea na matibabu yao.
“Ni
muhimu mtoto akapata elimu, Hospitali ikitoa kipaumbele kwa watoto wanaokaa
muda mrefu wakipata matibabu wakapata elimu kwa kuwajengea maktaba itawasaidia
kuwajenga kiakili pamoja na kuwa wanaumwa lakini pia wanapata haki yao ya
msingi ya kupata elimu sawa na watoto wengine”, alisema Dkt. Yonazi.
Dkt.
Yonazi alisema kuwepo kwa maktaba hiyo kumemshangaza na kupata jibu kuwa watoto
wanatakiwa kupata elimu wakiwa hospitali wakati wanaendelea kupata huduma za
matibabu.
Naibu
Katibu Mkuu huyo pia aliwapongeza wafanyakazi wa Taasisi hiyo kwa huduma ya
matibabu ya moyo wanayoitoa kwa wagonjwa na kusema kuwa kwa kufanya hivyo
wagonjwa wanafarijika kutokana na huduma wanayoipata.
“Kila
eneo nililopita nimeona wafanyakazi wanawahudumia wagonjwa kwa kujituma na
wanaonesha sura za kutabasamu hakika huduma hii mnayoitoa ni faraja kubwa kwa
wagonjwa na watu wengine wanaokuja katika Taasisi hii kupata huduma”,
alipongeza Dkt. Yonazi.
Kwa
upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof.
Mohamed Janabi alimshukuru Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano
na Teknolojia ya Habari kwa kutembelea Taasisi hiyo na kusema kuwa wamefarijika
kuona kiongozi wa Serikali amewatembelea na kuwaomba viongozi wengine
watembelee Taasisi hiyo ili waone huduma zinazotolewa kwa wananchi.
Prof.
Janabi alisema changamoto kubwa iliyopo ni hakuna data base ya kupata idadi sahihi ya wagonjwa wa moyo hapa nchini
jambo ambalo linawafanya washindwe kutunza kumbukumbu lakini kwa wagonjwa
wanaotibiwa katika Taasisi hiyo kumbukumbu zao wanazo na inawasaidia
kuwafuatilia wagonjwa hao.
Mkurugenzi
huyo Mtendaji ambaye pia ni daktari bingwa wa magonjwa ya moyo alisema takwimu
za Shirika la Afya Duniani (WHO) zinaonesha katika watoto 100 wanaozaliwa
wakiwa hai mmoja ana tatizo la moyo.
Kwa
Tanzania takwimu zinaonesha kila mwaka watoto wanaozaliwa wakiwa hai ni
milioni mbili na wenye matatizo ya moyo wanakadiriwa kuwa zaidi ya elfu
13 lakini haijulikani ni watoto wangapi wanazaliwa wakiwa na matatizo ya
moyo na wangapi watahitaji kutibiwa na kwa wakati gani.
“Katika
Taasisi yetu tuna kipimo cha kuangalia mtoto aliyepo tumboni kama ana matatizo
ya moyo au la (Fetal echocardiography). Kwa kufahamu tatizo tunamshauri mama
mjamzito ni hospitali gani aende kujifungua pia inatusaidia kumfuatilia mtoto
ili pindi atakapozaliwa aanze matibabu ya moyo mapema”,.
“Mama
mjamzito naye akiwa na tatizo la moyo ukimwambia ajifungue kwa njia ya kawaida
anaweza kupoteza maisha lakini kama mama huyu atagundulika kuwa na tatizo la
moyo atashauriwa ajifungue kwa njia ya upasuaji ili awe salama yeye na mtoto
wake aliyepo tumboni”, alisema Prof. Janabi.
Comments
Post a Comment