Wachezaji wawili wa klabu ya Yanga wafanyiwa vipimo vya moyo kabla ya kupatiwa leseni ya kujiunga na timu hiyo


Fundi sanifu wa moyo (Cardiovascular technologist) wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Paschal Kondi akimpima kipimo cha kuangalia jinsi mfumo wa umeme wa moyo unavyofanya kazi (Electrocardiography – ECG) mchezaji wa timu ya mpira wa miguu ya Yanga Aboutwaleeb Mshery wakati wachezaji wawili wa timu hiyo walipofika katika Taasisi hiyo kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa afya ya moyo kabla ya kupata leseni ya kujiunga na timu hiyo


Radiografa wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Indrisa Juma akimpima X-ray ya kifua ili kuchunguza moyo na mapafu mchezaji wa timu ya mpira wa miguu ya Yanga Salum Salum (Sureboy) wakati wachezaji wawili wa timu hiyo walipofika katika Taasisi hiyo jana kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa afya ya moyo kabla ya kupata leseni ya kujiunga na timu hiyo 


Mtaalam wa maabara wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Jordan Megabe akimtoa damu mchezaji wa timu ya mpira wa miguu ya Yanga Aboutwaleeb Mshery wakati wachezaji wawili wa timu hiyo walipofika katika Taasisi hiyo kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa afya ya moyo kabla ya kupata leseni ya kujiunga na timu hiyo



Daktari wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dickson Minja akimpima kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (Echocardiograph - ECHO) mchezaji wa timu ya mpira wa miguu ya Yanga Salum Salum (Sureboy) wakati wachezaji wawili wa timu hiyo walipofika katika Taasisi hiyo kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa afya ya moyo kabla ya kupata leseni ya kujiunga na timu hiyo 

Picha na: JKCI


 

Comments

Popular posts from this blog

Wataalamu wa JKCI kufanya upasuaji wa moyo nchini Zambia

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yamshukuru Rais Dkt.Samia kwa kuwapa magari