TPDC Marathon 2026 kuokoa maisha ya watoto 100 wenye magonjwa ya moyo
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Derick Moshi wakati wa uzinduzi wa TPDC Marathon uliofanyika leo katika hoteli ya Johari Rotana iliyopo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa TPDC Marathon kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa JKCI leo katika hoteli ya Johari Rotana iliyopo jijini Dar es Salaam.
Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Derick Moshi
akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa TPDC Marathon
itakayofanyika tarehe 29 Novemba, 2026 katika viwanja vya Polisi Officers Mess
iliyopo Masaki kwaajili ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo
wanaotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI).
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge, Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Derick Moshi, baadhi ya wafanyakazi wa JKCI na Global Medicare wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa uzinduzi wa TPDC Marathon uliofanyika leo katika hoteli ya Johari Rotana iliyopo jijini Dar es Salaam.
Na JKCI
****************************************************************************************************
Watoto
100 wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
(JKCI) kuchangiwa gharama za matibabu kupitia marathon iliyoandaliwa na Shirika
la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) msimu wa tatu inayotarajiwa kufanyika
mwezi Novemba mwaka huu.
Marathon
hiyo yenye kauli mbiu “Hatua Yako Inaokoa Maisha” ni ishara ya
mshikamano wa jamii katika kulinda na kuokoa maisha ya watoto wanaotoka katika
familia zisizokuwa na uwezo wa kugharamia matibabu ya moyo.
Akizungumza
wakati wa uzinduzi wa marathon hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo
Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge alisema zaidi ya watoto 1,500 wenye
magonjwa ya moyo wako katika foleni ya kusubiria huduma za upasuaji wa moyo
huku wengi wao wakitoka katika familia zenye uwezo mdogo wa kumudu gharama za
matibabu.
Dkt.
Kisenge alisema hali hiyo imeifanya taasisi hiyo kuitegemea Serikali na wadau mbalimbali
ili kuhakikisha watoto wenye matatizo ya moyo wanapata matibabu kwa wakati na
kuokoa maisha yao.
“Tunapokea
watoto wengi wenye matatizo ya moyo. Takwimu zinaonesha kuwa kati ya watoto 100
wanaozaliwa, takribani wawili huzaliwa wakiwa na matatizo ya moyo”, alisema
Dkt. Kisenge.
Dkt
Kisenge alisema Serikali imeendelea kutoa msaada kwa watoto wenye magonjwa ya
moyo hasa kwa kuzingatia kuwa sehemu kubwa ya wagonjwa hao hutoka katika
familia zenye uwezo mdogo wa kifedha na hivyo kushindwa kumudu gharama za
matibabu.
“Tunaishukuru
TPDC kwa kuendelea kushiriki katika kusaidia gharama zamatibabu ya watoto wenye
magonjwa ya moyo kupitia mpango wake wa kuchangisha fedha, mwaka 2022 TPDC
ilichangia shilingi milioni 100 kwa ajili ya matibabu ya watoto wenye magonjwa
ya moyo, huku mwaka 2025 ikichangia shilingi milioni 50”,
“Tunawaomba
wananchi wajitokeze kwa wingi kushiriki mbio hizi. Zaidi ya kusaidia watoto
wenye magonjwa ya moyo, kushiriki mbio hizi ni sehemu ya kufanya mazoezi,
kujenga afya bora na hatimaye kuokoa maisha”, alisema Dkt. Kisenge.
Kwa
upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC)
Derick Moshi alisema afya ni miongoni mwa nguzo muhimu katika utekelezaji wa
majukumu ya kampuni hiyo, hivyo ushiriki wao katika kusaidia sekta ya afya ni
sehemu ya wajibu wao kwa jamii.
“Kaulimbiu
ya TPDC marathon msimu wa tatu inatukumbusha kuchukua hatua, kuunganisha nguvu
na kutumia nafasi tulizonazo kujali maisha ya wengine”, alisema Moshi.
Moshi
alisema mbio hizo zitakuwa jukwaa la kuunganisha nguvu ya michezo, dhamira ya
kijamii na ushiriki wa wadau mbalimbali katika kuchangisha fedha za kuboresha
huduma za matibabu kwa watoto wenye magonjwa ya moyo.
“Tunathamini
kuona watu wanakuwa na afya njema na wanaishi, jambo la afya linalowezekana
kufanyika leo lifanyike leo lisubiri kesho”, alisema Moshi.
Moshi
alisema ushiriki wa TPDC katika kusaidia watoto wenye matatizo ya moyo si jambo
jipya bali ni mwendelezo wa jitihada za kampuni hiyo za kuirudishia jamii
kupitia shughuli za uwajibikaji kwa jamii.
Naye
Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati Mussa Mussa aliwataka waandishi wa habari
kutumia nafasi yao kuelimisha na kuhamasisha jamii kuhusu TPDC Marathon 2026
ili kuongeza ushiriki wa wananchi na hatimaye kufanikisha lengo la kuwasaidia
watoto wenye magonjwa ya moyo.
Mussa
alisema kushiriki katika mbio hizo kuna faida mbili ikiwemo kuchangia katika
kuokoa maisha ya watoto wenye matatizo ya moyo na kuimarisha afya za washiriki
wenyewe.
“Naipongeza
TPDC kwa kuanzisha na kuendeleza mpango huo, Wizara ya Nishati inafurahia kuona
kampuni hii ikishiriki katika jambo lenye manufaa kwa jamii, tunatamani mpango
huu uwe uendelevu”, alisema Mussa.
.jpeg)

.jpeg)


Comments
Post a Comment