Posts

Showing posts from February, 2022

Serikali yaombwa kuyaingiza magonjwa yasiyoambukiza katika bima ya afya kwa watu wote

Image
Katibu wa Shirikisho la Vyama vya magonjwa yasiyoambukiza Tanzania (TANCDA) Prof. Kaushik Ramaiya akiwasilisha mada kuhusu ukubwa wa tatizo la magonjwa yasiyoambukiza wakati wa uzinduzi wa mkakati wa utetezi juu ya bima ya afya kwa watu wote inayojumuisha magonjwa yasiyoambukiza uliofanyika hivi karibuni katika Hoteli ya Protea jijini Dar es Salaam. Uzinduzi huo uliandaliwa na Shirikisho la Vyama vya magonjwa yasiyoambukiza Tanzania (TANCDA). Katibu wa Shirikisho la Vyama vya magonjwa yasiyoambukiza Tanzania (TANCDA) Prof. Kaushik Ramaiya akizungumza na wadau wa afya walioshiriki katika uzinduzi wa mkakati wa bima ya afya kwa wote inayojumuisha magonjwa yasiyoambukiza uliofanyika hivi karibuni katika Hoteli ya Protea jijini Dar es Salaam. Walioshiriki katika uzinduzi huo ni wadau mbalimbali  wakiwemo wizara ya Afya, wajumbe wa kamati ya kudumu ya bunge ya masuala ya UKIMWI, Kifua Kikuu, Dawa za kulevya na Magonjwa yasiyoambukiza, Kamati ya kudumu ya bunge ya huduma na maendeleo ya jami

Watu 26 kati ya 100 wana tatizo la ugonjwa wa shinikizo la juu la damu nchini

Image
Amina Mollel mkazi wa Arusha ambaye anaishi na ugonjwa wa saratani ya kizazi na Virusi vya UKIMWI akieleza jinsi anavyoishi na magonjwa hayo wakati wa  mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kuyafahamu magonjwa yasiyoambukiza yaliyoandaliwa kwa wajumbe wa kamati ya kudumu ya bunge ya masuala ya UKIMWI, Kifua kikuu, madawa ya kulevya na magonjwa yasiyoambukiza, watu wanaoishi na magonjwa hayo na wahariri wa vyombo vya habari. Washiriki 64 walihudhuria mafunzo hayo ya  siku mbili yaliandaliwa na  Wizara ya Afya kupitia  Shirikisho la Vyama vya Magonjwa yasiyoambukiza Tanzania  (TANCDA)  yaliyofanyika katika Hoteli ya Protea jijini Dar es Salaam.  Prof. Beatus Kundi akielezea  andiko la mkakati wa utetezi juu ya masuala ya lishe na kushughulisha mwili katika mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kuyafahamu magonjwa yasiyoambukiza yaliyoandaliwa kwa wajumbe wa kamati ya kudumu ya bunge ya masuala ya UKIMWI, Kifua kikuu, madawa ya kulevya na magonjwa yasiyoambukiza, watu wanaoishi na magonjwa hayo na waha

Wanawake watakiwa kuandaa mlo bora ili kuzikinga familia zao na magonjwa yasiyoambukiza

Image
Washiriki wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kuyafahamu magonjwa yasiyoambukiza ambao ni wajumbe wa kamati ya kudumu ya bunge ya masuala ya UKIMWI, Kifua kikuu, madawa za kulevya na magonjwa yasiyoambukiza, watu wanaoishi na magonjwa hayo na wahariri wa vyombo vya habari wakifuatilia mada ya umuhimu wa kufanya mazoezi iliyokuwa inatolewa kwenye mafunzo hayo yanayofanyika katika Ukumbi wa Protea jijini Dar es Salaam. Mfunzo hayo ya  siku mbili yameandaliwa na Wizara ya Afya kupitia  Shirikisho la Vyama vya Magonjwa yasiyoambukiza Tanzania  (TANCDA). Mkurugenzi Msaidizi huduma za lishe kutoka Wizara ya Afya Dkt. Grace Moshi akiwasilisha mada kuhusu lishe bora inavyoweza kuwakinga watu na magonjwa yasiyoambukiza kwa washiriki wa mafunzo ya kujenga uwezo wa kuyafahamu magonjwa hayo  ambao ni wajumbe wa kamati ya kudumu ya bunge ya masuala ya UKIMWI, Kifua kikuu, madawa za kulevya na magonjwa yasiyoambukiza, watu wanaoishi na magonjwa hayo na wahariri wa vyombo vya habari .  Mafunzo hayo ya

Afya ya akili inatupa uwezo wa kufurahia maisha kwenye viwango tofauti

Image

Umuhimu wa afya ya akili kwa watu wenye magonjwa yasiyo ya kuambukiza

Image

Wafanyakazi bora wa robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/2022 wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wapongezwa kwa utendaji mzuri wa kazi

Image
Mfanyakazi bora wa robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/2022 aliyeshika nafasi ya kwanza Dkt. Winnie Masakuya akipokea zawadi ya ngao kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Robert Mallya wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza wafanyakazi bora leo katika Ukumbi wa Taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam Mfanyakazi bora wa robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/2022 aliyeshika nafasi ya pili Radiographer Idris Juta akipokea cheti cha mfanyakazi bora kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Robert Mallya wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza wafanyakazi bora leo katika Ukumbi wa Taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam. Mfanyakazi bora wa robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/2022 aliyeshika nafasi ya tatu Edna Sanga akipokea cheti cha mfanyakazi bora kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Robert Mallya wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza wafanyakazi hao iliyofanyika leo katika Ukumbi wa Taasisi hiy

Jinsi ya kutoa huduma ya kwanza kwa mgonjwa mahututi ukaweza kuokoa mai...

Image

Wagonjwa 19 ambao mishipa yao ya damu ya moyo ilikuwa imeziba kwa asilimia 100 na kushindwa kupitisha damu na ambao valvu zao za moyo zilikuwa zimeziba wafanyiwa upasuaji mdogo

Image
  Madaktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa Shirika la Madaktari Afrika lililopo nchini Marekani wakimzibua mgonjwa mshipa wa damu wa moyo uliokuwa umeziba kwa asilimia 100 na kutokupitisha damu kabisa (Complex Percutaneous Coronary Intervention – PCI) wakati wa kambi maalum ya ya matibabu ya moyo ya siku tano inayoendelea katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Madaktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa Shirika la Madaktari Afrika lililopo nchini Marekani wakimzibua mgonjwa  Valvu ya moyo iliyokuwa imeziba na kushindwa kupitisha damu  (Balloon Mitral Valve -BMV) wakati wa kambi maalum ya matibabu ya moyo ya siku tano inayoendelea katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Mara nyingi matibabu ya aina hiyo yanafanyika JKCI kwa njia ya upasuaji mkubwa wa moyo wa  kufungua kifua. *************************************************************************************************

Serikali yaombwa kutoa elimu kinga ya magonjwa yasiyo ya kuambukiza ikiwemo umuhimu wa kudumisha afya ya akili kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari

Image
Watu wanaoishi na  magonjwa yasiyoambukiza wakiuliza maswali wakati wa mafunzo ya kutoa uelewa wa magonjwa hayo yaliyofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) uliopo jijini Dar es Salaam. Mafunzo hayo ya siku moja yaliandaliwa na Shirikisho la Vyama vya Magonjwa yasiyoambukiza Tanzania (TANCDA) ambapo washiriki walikuwa 30 kutoka mikoa mbalimbali. Watu wanaoishi na  magonjwa yasiyoambukiza wakiuliza maswali wakati wa mafunzo ya kutoa uelewa wa magonjwa hayo yaliyofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) uliopo jijini Dar es Salaam. Mafunzo hayo ya siku moja yaliandaliwa na Shirikisho la Vyama vya Magonjwa yasiyoambukiza Tanzania (TANCDA) ambapo washiriki walikuwa 30 kutoka mikoa mbalimbali.  Watu wanaoishi na  magonjwa yasiyoambukiza wakisikiza mada ya jinsi ya kutoa elimu kwa wagonjwa wenzao ilitokuwa inatolewa na Elizabeth Licoco wakati wa mafunzo

JKCI mbioni kushirikiana na Jamhuri ya watu wa Czech kutoa huduma za matibabu ya moyo

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akijadiliana na madaktari kutoka Hospitali ya Ostrava iliyopo Jamhuri ya Watu wa Czech namna ambayo watashirikiana katika kutoa huduma za matibabu ya moyo jana baada ya madaktri hao kutembelea JKCI Jijini Dar es Salaam Madaktari kutoka Hospitali ya Ostrava iliyopo nchini Czech na wenzao kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifuatilia majadiliano wakati madaktari hao walipotembelea JKCI kwa ajili ya kuona namna ya kushirikiana katika kutoa huduma za matibabu ya moyo jana katika ukumbi wa Taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam Afisa Muuguzi wa Chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum (ICU) wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prisca Kiyuka akiwaelezea namna ambavyo wagonjwa wanapatiwa huduma katika chumba hicho madaktari kutoka Hospitali ya Ostrava iliyopo Jamhuri ya Watu wa Czech walipotembelea Taasisi hiyo kwa ajili ya kuona namna ambavyo wanaweza kushirikiana katika kutoa huduma za matib