Posts

Showing posts from March, 2022

EAC, SADC wakaribishwa JKCI kutibiwa magonjwa ya moyo

Image
Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Stella Mongela akiwaonesha viongozi wa wizara zinazosimamia vituo vya umahiri (center of excellence) pamoja na viongozi wa vituo hivyo kutoka nchi wanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC) jinsi tundu lililoko kwenye  moyo linavyozibwa kwa kutumia mtambo wa Cathlab wakati viongozi hao walipotembelea JKCI kwa ajili ya kuangalia huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akielezea huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa na taasisi hiyo kwa viongozi wa wizara zinazosimamia vituo vya umahiri (center of excellence) pamoja na viongozi wa vituo hivyo kutoka nchi wanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC) na wataalamu wa afya  kutoka Hospitali ya Taifa ya Moyo ya nchini Zambia walipotembelea Taasisi hiyo leo jijini Dar es Salaam. Baadhi ya viongozi wa wizara zinazosimamia vituo vya umahiri (center of excellence) p...

Hospitali ya Taifa ya Moyo ya nchini Zambia yatembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kuangalia huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akielezea namna ambavyo JKCI inatoa huduma kwa wagonjwa wakati wa ziara ya viongozi kutoka Hospitali ya Taifa ya Moyo ya nchini Zambia walipotembelea JKCI kwa ajili ya kuangalia huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa na taasisi hiyo leo katika Taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam Baadhi ya viongozi kutoka Hospitali ya Taifa ya Moyo iliyopo nchini Zambia wakisikiliza taarifa iliyokuwa inatolewa na Prof. Janabi (hayupo pichani) wakati wa ziara ya viongozi hao kuangalia huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) leo katika ukumbi wa Taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam Makamu wa Chuo Kikuu cha Afya ya Sayansi Muhimbili Prof. Andrea Pembe akizungumza na uongozi kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ulioambatana na viongozi kutoka Hospitali ya Taifa ya Moyo ya nchini Zambia kwa ajili ya kuona namna ambavyo watashirikiana katika masuala ya taaluma baada ya viongozi hao ku...

Wagonjwa saba wenye tatizo la hitilafu ya mfumo wa umeme wa moyo watibiwa katika kambi maalum ya matibabu ya moyo

Image
Wataalamu mabingwa wa moyo na matibabu ya mfumo wa umeme wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Shifa iliyopo nchini Misri wakimwekea mgonjwa kifaa kinachousaidia moyo kufanya kazi kinachojulikana kwa jina la Cardiac resychronical Therapy – CRTD kinachotumia umeme mkubwa (High Power Device) wakati wa kambi maalum ya siku mbili ya matibabu hayo iliyomalizika hivi karibuni katika Taasisi hiyo. Jumla ya wagonjwa saba wenye tatizo la hitilafu ya mfumo wa umeme wa moyo walitibiwa katika   kambi hiyo. ****************************************************************************************************************************************************************************************************************************************** Wagonjwa saba wenye tatizo la hitilafu ya mfumo wa umeme wa moyo wamepatiwa matibabu katika kambi maalum ya matibabu iliyofanywa na wataalamu mabingwa wa mfumo wa umeme wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Ki...

Serikali ya awamu ya sita imedhamiria kuondoa uzembe na vitendo vya rushwa mahali pa kazi

Image
Mwenyekiti wa Baraza la wafanyakazi ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akizungumza na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la JKCI wakati wa kikao cha sita cha baraza hilo kilichafanyika hivi karibuni katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Daktari bingwa wa wagonjwa waliolazwa katika chumba cha uangalizi maalum (ICU) wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Vivian Mlawi akijibu swali kuhusu mafunzo ya kutoa huduma ya kwanza kwa watumishi wakati wa kikao cha sita cha baraza la wafanyakazi kilichafanyika hivi karibuni katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Tiba ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tatizo Waane akijibu swali kuhusu uimarishwaji wa miundombinu iliyopo katika chumba cha upasuaji mdogo wa moyo (Cathlab) wakati wa kikao cha sita cha baraza la wafanyakazi kilichafanyika hivi karibuni katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo ...

Raia wa Ujerumani mbioni kutibiwa JKCI

Image
Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Happy Malunde akimwonesha upasuaji mkubwa wa kubadilisha valvu ya moyo jinsi unavyofanyika Daktari kutoka ubalozi wa Ujerumani kanda ya Afrika Mashariki na Kati Jorg Siedenburg wakati alipotembelea Taasisi hiyo kwa ajili ya kuangalia huduma zinazotolewa. Lengo la kufanya ziara hiyo ni kuona namna ambavyo wafanyakazi wa balozi na watalii kutoka Ujerumani wanaotembelea nchi za Afrika Mashariki na kati pale watakapohitaji huduma za matibabu ya moyo watatibiwa JKCI. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akimuonesha moja ya chumba cha kulaza wagonjwa mashuhuri (VIP Room) Daktari kutoka ubalozi wa Ujerumani kanda ya Afrika Mashariki na Kati Jorg Siedenburg wakati alipotembelea Taasisi hiyo kwa ajili ya kuangalia huduma zinazotolewa na Taasisi hiyo. Lengo la kufanya ziara hiyo ni kuona namna ambavyo wafanyakazi wa balozi na watalii kutoka Ujerumani wanaotembelea nchi za Afrika Mashariki na kati ...

Watu 102 wafanyiwa uchunguzi wa magonjwa ya moyo wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani yaliyofanyika kimkoa katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam

Image
Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi ambaye pia ni Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Delilah Kimambo akimwelezea madhara ya magonjwa ya moyo mwananchi aliyefika katika banda la JKCI kwa ajili ya kupata huduma za upimaji na matibabu ya moyo bila malipo wakati wa maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika kimkoa jana katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam. Jumla ya watu 102 walifanyiwa uchunguzi wa   magonjwa ya moyo ambapo 41 walipewa dawa za kutumia. Wanawake wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakipita mbele ya mgeni rasmi wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani Katibu Tawala mkoa wa Dar es Salaam Hassan Rugwa wakati wa maadhimisho hayo yaliyofanyika kimkoa jana katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam.  Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Edna Mulenda akimpima urefu, uzito na uwiano wa urefu na uzito (BMI) mgeni rasmi wa maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani Katibu Tawala Mkoa wa Dar es S...