Hospitali ya Taifa ya Moyo ya nchini Zambia yatembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kuangalia huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akielezea namna ambavyo JKCI inatoa huduma kwa wagonjwa wakati wa ziara ya viongozi kutoka Hospitali ya Taifa ya Moyo ya nchini Zambia walipotembelea JKCI kwa ajili ya kuangalia huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa na taasisi hiyo leo katika Taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam

Baadhi ya viongozi kutoka Hospitali ya Taifa ya Moyo iliyopo nchini Zambia wakisikiliza taarifa iliyokuwa inatolewa na Prof. Janabi (hayupo pichani) wakati wa ziara ya viongozi hao kuangalia huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) leo katika ukumbi wa Taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam

Makamu wa Chuo Kikuu cha Afya ya Sayansi Muhimbili Prof. Andrea Pembe akizungumza na uongozi kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ulioambatana na viongozi kutoka Hospitali ya Taifa ya Moyo ya nchini Zambia kwa ajili ya kuona namna ambavyo watashirikiana katika masuala ya taaluma baada ya viongozi hao kutembelea JKCI kuangalia huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa na Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam  


Mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa ya Moyo ya nchini Zambia Chabwela Shumba akielezea mafanikio ya ziara iliyoifanywa na viongozi kutoka hospitali hiyo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na Chuo Kikuu cha Afya ya Sayansi Muhimbili wakati wa kikao mara baada ya kutembelea na kuangalia huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa katika Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam

Msimamizi wa wodi ya watoto wenye magonjwa ya moyo ambaye pia ni Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Tedy Tarimo akielezea majukumu ya wodi hiyo kwa viongozi kutoka Hospitali ya Taifa ya Moyo ya Nchini Zambia walipotembelea wodi hiyo kuangalia huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa leo katika Taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam

Msimamizi wa chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum (ICU) wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Abela Venance akimuonesha namna ambavyo taarifa za mgonjwa huandikwa Mkurugenzi wa Idara ya Uuguzi kutoka Hospitali ya Taifa ya Moyo ya Nchini Zambia Josephine Chimpinde wakati wa ziara ya viongozi kutoka hospitali hiyo walipotembelea JKCI kwa ajili kuangalia huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa na taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam


Mkuu wa Kitengo cha huduma bora wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Naiz Majani akiwaelezea namna ambavyo kliniki ya watoto wenye magonjwa ya moyo inavyofanya kazi viongozi kutoka Hospitali ya Taifa ya Moyo ya Nchini Zambia walipotembelea JKCI kwa ajili ya kuangalia huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa na taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam


Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Moyo kwa Watoto ambaye pia ni daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Sulende Kubhoja akiwaelezea uchunguzi anaofanyiwa mtoto anapofika katika kliniki za moyo viongozi kutoka Hospitali ya Taifa ya Moyo ya Nchini Zambia walipotembelea JKCI kwa ajili ya kuangalia huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa na taasisi hiyo  leo Jijini Dar es Salaam 


Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Stella Mongela akielezea huduma anayopatiwa mtoto katika chumba cha upasuaji mdogo wa moyo kwa viongozi kutoka Hospitali ya Taifa ya Moyo ya Nchini Zambia walipotembelea JKCI kwa ajili ya kuangalia huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa na taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akiwa katika picha ya pamoja na viongozi kutoka Hospitali ya Taifa ya Moyo ya Nchini Zambia walipotembelea JKCI kwa ajili ya kuangalia huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa na taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam

Picha na: JKCI

 

Comments

Popular posts from this blog

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yapata tuzo ya taasisi ambayo imetoa mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024

Maabara ya JKCI yapata ithibati ya kimataifa (ISO 15189:2012)