Raia wa Ujerumani mbioni kutibiwa JKCI

Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Happy Malunde akimwonesha upasuaji mkubwa wa kubadilisha valvu ya moyo jinsi unavyofanyika Daktari kutoka ubalozi wa Ujerumani kanda ya Afrika Mashariki na Kati Jorg Siedenburg wakati alipotembelea Taasisi hiyo kwa ajili ya kuangalia huduma zinazotolewa. Lengo la kufanya ziara hiyo ni kuona namna ambavyo wafanyakazi wa balozi na watalii kutoka Ujerumani wanaotembelea nchi za Afrika Mashariki na kati pale watakapohitaji huduma za matibabu ya moyo watatibiwa JKCI.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akimuonesha moja ya chumba cha kulaza wagonjwa mashuhuri (VIP Room) Daktari kutoka ubalozi wa Ujerumani kanda ya Afrika Mashariki na Kati Jorg Siedenburg wakati alipotembelea Taasisi hiyo kwa ajili ya kuangalia huduma zinazotolewa na Taasisi hiyo. Lengo la kufanya ziara hiyo ni kuona namna ambavyo wafanyakazi wa balozi na watalii kutoka Ujerumani wanaotembelea nchi za Afrika Mashariki na kati pale watakapohitaji huduma za matibabu ya moyo watatibiwa JKCI.

Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Tatizo Waane akimwelezea huduma zinazotolewa kwa wagonjwa wa nje Daktari kutoka ubalozi wa Ujerumani kanda ya Afrika Mashariki na Kati Jorg Siedenburg alipotembelea Taasisi hiyo kwa ajili ya kuangalia huduma zinazotolewa na JKCI. Lengo la kufanya ziara hiyo ni kuona namna ambavyo wafanyakazi wa balozi na watalii kutoka Ujerumani wanaotembelea nchi za Afrika Mashariki na kati pale watakapohitaji huduma za matibabu ya moyo watatibiwa JKCI.

Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Tulizo Shemu akimuonesha  jinsi uzibuajia wa mishipa ya damu ya moyo unavyofanyika kwa kutumia mtambo wa Cathlab Daktari kutoka ubalozi wa Ujerumani kanda ya Afrika Mashariki na Kati Jorg Siedenburg wakati alipotembelea Taasisi hiyo kwa ajili ya kuangalia huduma zinazotolewa. Lengo la kufanya ziara hiyo ni kuona namna ambavyo wafanyakazi wa balozi na watalii kutoka Ujerumani wanaotembelea nchi za Afrika Mashariki na kati pale watakapohitaji huduma za matibabu ya moyo watatibiwa JKCI.

Daktari bingwa wa wagonjwa wa dharula na mahututi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Vivian Mlawi akimwelezea huduma wanazozitoa kwa watoto waliolazwa katika wodi ya wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum (ICU) daktari kutoka ubalozi wa Ujerumani kanda ya Afrika Mashariki na Kati Jorg Siedenburg wakati alipotembelea Taasisi hiyo kwa ajili ya kuangalia huduma mbalimbali zinazotolewa. Lengo la kufanya ziara hiyo ni kuona namna ambavyo wafanyakazi wa balozi na watalii kutoka Ujerumani wanaotembelea nchi za Afrika Mashariki na kati pale watakapohitaji huduma za matibabu ya moyo watatibiwa JKCI.


***********************************************

Picha na: JKCI


 

Comments

Popular posts from this blog

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yapata tuzo ya taasisi ambayo imetoa mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024

Maabara ya JKCI yapata ithibati ya kimataifa (ISO 15189:2012)