EAC, SADC wakaribishwa JKCI kutibiwa magonjwa ya moyo

Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Stella Mongela akiwaonesha viongozi wa wizara zinazosimamia vituo vya umahiri (center of excellence) pamoja na viongozi wa vituo hivyo kutoka nchi wanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC) jinsi tundu lililoko kwenye  moyo linavyozibwa kwa kutumia mtambo wa Cathlab wakati viongozi hao walipotembelea JKCI kwa ajili ya kuangalia huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akielezea huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa na taasisi hiyo kwa viongozi wa wizara zinazosimamia vituo vya umahiri (center of excellence) pamoja na viongozi wa vituo hivyo kutoka nchi wanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC) na wataalamu wa afya  kutoka Hospitali ya Taifa ya Moyo ya nchini Zambia walipotembelea Taasisi hiyo leo jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya viongozi wa wizara zinazosimamia vituo vya umahiri (center of excellence) pamoja na viongozi wa vituo hivyo kutoka nchi wanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC) na wataalamu wa afya  kutoka Hospitali ya Taifa ya Moyo ya nchini Zambia wakifuatilia wasilisho la matibabu ya moyo  lililokuwa linatolewa na Prof. Janabi wakati wa ziara iliyofanywa na viongozi hao ya  kuangalia huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa na taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam.


Kiongozi wa wizara inayosimamia  kituo cha umahiri wa matibabu ya Saratani (center of excellence) kutoka nchini Uganda Richard Tumwesigye akichangia hoja wakati wa ziara iliyofanywa na viongozi wa wizara zinazosimamia vituo vya umahiri (center of excellence) pamoja na viongozi wa vituo hivyo kutoka nchi wanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC) ya kuangalia huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI).

Mkurugenzi wa Shirika la Save a Child Heart (SACH) la nchini Israel Simon Fishers akielezea ushirikiano uliopo kati ya Israel na Tanzania katika kutoa huduma za matibabu ya moyo kwa watoto wakati wa ziara iliyofanywa na viongozi wa wizara zinazosimamia vituo vya umahiri (center of excellence) pamoja na viongozi wa vituo hivyo kutoka nchi wanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC) waliyoifanya katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI).


Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delilah Kimambo akielezea miradi mbalimbali inayofanyika katika taasisi hiyo kwa viongozi wa wizara zinazosimamia vituo vya umahiri (center of excellence) pamoja na viongozi wa vituo hivyo kutoka nchi wanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC) walipotembelea Taasisi hiyo leo iliyopo jijini Dar es Salaam.

Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Tulizo Shem akiwaelezea huduma zinazotolewa katika wodi ya watoto wenye magonjwa ya moyo viongozi wa wizara zinazosimamia vituo vya umahiri (center of excellence) pamoja na viongozi wa vituo hivyo kutoka nchi wanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC) wakati wa ziara ya kuangalia huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa na Taasisi hiyo.


Mwenyekiti wa kamati ya viongozi wa wizara zinazosimamia vituo vya umahiri (center of excellence) pamoja na viongozi wa vituo hivyo kutoka nchi wanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC) Dkt. Nicholus Ndongi kutoka nchini Kenya akimjulia hali mtoto Jarden Maina kutoka nchini humo  aliyefanyiwa upasuaji wa moyo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa ziara yao ya  kuangalia huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa na Taasisi hiyo.


Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa wizara zinazosimamia vituo vya umahiri (center of excellence) pamoja na viongozi wa vituo hivyo kutoka nchi wanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC) na wataalam wa Hospitali ya Taifa ya Moyo ya nchini Zambia pamoja na madaktari wa Shirika la Save a Child Heart (SACH) la nchini Israel mara baada ya ziara fupi iliyofanywa na wataalamu hao ya kuangalia huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa JKCI.

Na: JKCI

****************************************************************************************************************************************************************

Nchi wanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC) na Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) wameombwa kupeleka wagonjwa wao kutibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwani matibabu yanayotolewa ni ya umahiri wa hali ya juu hayana tofauti na yanayotolewa nchi za Ulaya na India.

Hayo yamesemwa leo na Mwakilishi wa Katibu Mkuu wizara ya Afya ambaye ni Mkurugenzi wa Mafunzo kutoka wizara hiyo Dkt. Saitore Laizer wakati akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa ziara ya viongozi wa wizara zinazosimamia vituo vya umahiri (center of excellence) pamoja na viongozi wa vituo hivyo kutoka nchi wanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki waliotembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili yakuona huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa.

Dkt. Laizer alisema mashine zinazotumika kuchunguza na kutibu magonjwa ya moyo na mishipa ya damu zilizopo Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete ni zilezile zinazotumika Ulaya na nchini India ambazo katika nchi za Afrika ziko tatu  na Afrika Mashariki ziko mbili.

“Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete pako salama na gharama za matibabu wanaweza kuzimudu ukilinganisha na maeneo mengine ambayo  wangeenda kutibiwa nje ya Afrika pia mazingira ni  hayohayo ya kiafrika  ambayo wameyazoea na hata stress za kuwa nje ya nchi wanaweza kuziepuka”, anasema Dkt. Laizer.

Akizungumzia kuhusu ziara hiyo ya ugeni  kutoka nchi wanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki  Dkt. Laizer alisema katika Afrika Mashariki wametengeneza vituo vya umahiri wa matibabu tofauti kwa kila nchi kwa  upande wa  Tanzania ilichaguliwa  kuwa   kituo cha umahiri wa matibabu ya moyo na mishipa ya damu.

Alisema ujenzi wa kituo hicho unasimamiwa na wizara ya Elimu kupitia chuo Kikuu cha Sayansi na Tiba Muhimbili (MUHAS) kwani  taasisi hizi mbili zinafanya kazi kwa pamoja kwa sababu mwananchi anayelengwa ni  mmoja.

“Hatuwezi kuzungumzia  matibabu ya moyo na mishipa ya damu pasipo kujumuisha  Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Taasisi  ambayo imeleta mapinduzi makubwa katika matibabu ya moyo nchini na Afrika ya Mashariki na Kati. Ujumbe wa nchi za EAC  uko hapa wamepata maelezo na wengine wamekiri hawakuwa wanafahamu kama kuna huduma hizo hapa nchini ambazo hata kama mtu angeenda kutibiwa mbali na Afrika angezipata”,.

“Ujio wa ugeni huu ni kuona huduma zinazotolewa ambazo zitashahibiana  na kile ambacho wanachama wa nchi za Afrika Mashariki wamependekeza Tanzania iwe na kituo cha umahiri wa matibabu ya moyo na mishipa ya damu kwa hiyo wageni wamefurahi sana  na wakitoka hapa wataenda Mloganzila kuangalia maendeleo ya ujenzi wa kituo hicho umefikia wapi”, alisema Dkt. Laizer.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati ya viongozi wa wizara zinazosimamia vituo vya umahiri (center of excellence) pamoja na viongozi wa vituo hivyo Dkt. Nicholus Ndongi kutoka nchini Kenya alisema hii ni mara ya tatu wanakutana na leo hii wako nchini  Tanzania kwa ajili ya kuona hatua ya ujenzi wa kituo cha umahiri cha magonjwa ya moyo na mishipa ya damu umefikia katika hatua gani na kuangalia kama kuna matatizo yanayokwamisha ujenzi huo na kama yapo ni kwa ajili gani na angalia namna ya kuweza kutatua matatizo hayo.

Alizitaja sababu ya kuanzishwa kwa vituo hivyo vya umahiri ni mawaziri wa Afya wa Afrika Mashariki waliona watu wanapata shida wanapopata magonjwa ambayo hayawezi kutibiwa  katika nchi hizo na kwenda kutibiwa nje ya nchi. Mawaziri walikaa chini na kuona waanzishe vituo vya umahiri vya matibabu hayo ambavyo vitakuwa na vitendea kazi vyote ili wagonjwa wasiende nje kwenda  kutibiwa bali  watibiwe katika nchi  za Afrika Mashariki.

Kila nchi ilipewa kituo cha umahiri ambapo Tanzania ni kituo cha umahiri wa matibabu ya magonjwa ya moyo na mishipa ya damu, Uganda ugonjwa wa saratani, Rwanda chanjo na ufundi wa vifaa tiba (bio medical engineering) na Burundi lishe.

“Kabla ya kwenda kuona ujenzi wa kituo cha Mloganzila tumepita hapa Taasisi ya Moyo na kuona huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa, tumefurahi na hatukuwa tunajua kama JKCI inatoa huduma ya juu sana jambo la muhimu ni watangaze huduma wanazozitoa zijulikane Afrika Mashariki na Duniani ili watu wajue  kuna kituo ambacho wanaweza kutibiwa na wasiende mbali na Afrika”,.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi aliwashukuru wajumbe hao kwa kutembelea Taasisi hiyo na kusema idadi ya wagonjwa wanaowatibu  imekuwa ikiongezeka kila mwaka hiyo ni kutokana na kuwa na wataalamu wenye uzoefu wa hali ya juu  pamoja na vifaa tiba vya kisasa.

 “Katika Taasisi hii tunapokea wagonjwa kutoka nje ya nchi pia Kenya wameanza kuleta wagonjwa na wiki iliyopita tumewafanyia upasuaji mkubwa wa moyo watoto wawili kutoka nchini humo pia tunatarajia  kupata wagonjwa wengi zaidi. Burundi pia wanaleta wagonjwa kuja kutibiwa hapa  mwaka huu tumeshawatibu  wagonjwa sita kutoka nchini humo”, alisema Prof. Janabi.

Prof. Janabi alitoa ushauri wakati vituo hivyo vya umahiri vinajengwa pamoja na  kuwasomesha madaktari bingwa, technician na wauguzi waangalie namna ya kuwasomesha wataalamu wa vifaa tiba (bio medical engineering) kwani vifaa hivyo ni  vya gharama kubwa ni vizuri wawe na mafundi wao ambao wataijua mitambo na kufanya matengenezo madogo pale itakapoharibika kuliko kutegemea mafundi kutoka nje au kutoka kwa waliuwauzia mitambo ambao watawalipa fedha nyingi.

Wakati huohuo Lyidia Irima kutoka nchini Kenya ambaye mtoto wake amefanyiwa upasuaji wa moyo alishukuru kwa huduma aliyoipata na kusema kuwa mtoto wake alizaliwa na matatizo ya moyo na walimgondua akiwa na umri wa mwaka mmoja na miezi mitatu alizunguka katika Hospitali mbalimbali lakini hakuweza kupona hadi alipofika JKCI.

“Mtoto wangu alikuwa na matunu kwenye moyo na mishipa inayopeleka damu kwenye moyo ilikuwa na shida hakuwa anaweza kuhema vizuri lakini baada ya kufanyiwa upasuaji anapumua vizuri ile sauti aliyokuwa anatoa haiku tena”,. 

“Ninawaambia wamama wa Afrika Mashariki ambao watoto wao wanamatatizo kama ya mwanangu wasife moyo kwani kuna Hospitali zinazoweza kuwasaidia watoto wao  ikiwemo Taasisi ya  Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wanaweza kuja hapa wakatibiwa”, alisema Lyidia .

Wakiwa katika Taasisi hiyo viongozi hao walitembelea maeneo mbalimbali ya Taasisi hiyo ikiwemo mitambo ya Cathlab, wodi za wagonjwa walioko katika uangalizi maalum (ICU) na  wodi ya watoto.  

Comments

Popular posts from this blog

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yapata tuzo ya taasisi ambayo imetoa mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024

Maabara ya JKCI yapata ithibati ya kimataifa (ISO 15189:2012)