Posts

Showing posts from April, 2022

Wagonjwa 20 wafanyiwa upasuaji mkubwa wa moyo katika kambi maalum ya matibabu iliyofanywa na madaktari wa JKCI na mwenzao kutoka Hospitali ya Max iliyopo nchini India

Image
Madaktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na mwenzao kutoka Hospitali ya Max ya nchini India Dkt. Subhash Sinha wakimbadilisha mshipa mkubwa wa moyo  (Aorta) mgonjwa ambaye mshipa wake uliokua umetanuka zaidi ya sentimita 5  wakati wa kambi maalum ya matibabu ya moyo ya siku saba iliyofanyika katika Taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam. Jumla ya wagonjwa 20 wamefanyiwa upasuaji mkubwa wa moyo Wataalam wa Afya kutoka Idara ya Upasuaji mkubwa wa Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiwa katika picha ya pamoja na Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu kutoka hospitali ya Max iliyopo nchini India Subhash Sinha baada ya kumalizika kwa kambi maalum ya matibabu ya moyo ya siku saba iliyofanyika katika Taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam. Na: JKCI ********************************************************************************************* Wagonjwa 20 wamefanyiwa upasuaji mkubwa wa moyo wa kufungua kif

Wafanyakazi bora wa robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2021/2022 wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wapongezwa kwa utendaji mzuri wa kazi

Image
Mfanyakazi bora wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Afisa Muuguzi Joshua Ogutu akipokea cheti cha mfanyakazi bora kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Dkt. Delilah Kimambo wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza wafanyakazi bora leo katika Ukumbi wa Taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam. Mfanyakazi bora wa robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2021/2022 aliyeshika nafasi ya kwanza Afisa Msaidi wa Afya Dominick Kanani katika picha ya pamoja na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delilah Kimambo na Mkurugenzi wa Idara ya Upasuaji Dkt. Angela Muhozya wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza wafanyakazi bora leo katika Ukumbi wa Taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam Mfanyakazi bora wa robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2021/2022 aliyeshika nafasi ya pili Mtunza Kumbukumbu (Afya) Vedastus Lazaro akipokea cheti cha mfanyakazi bora kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delilah Kimambo wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza wafanya

Watu 10 wafanyiwa upasuaji wa moyo kutumia tundu dogo (Minimum Invasive Surgery) katika kambi maalum ya matibabu iliyofanyika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete

Image
Wataalam wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na mwenzao kutoka Hospitali ya Max iliyopo nchini India Dkt. Viveka Kumar wakimfanyia mtoto upasuaji wa kumbadilishia betri ya moyo iliyoisha muda wake kwa kutumia tundu dogo (Minimum Invasive Surgery) katika kambi maalum ya siku nne iliyomalizika leo katika Taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam. Jumla ya wagonjwa 10 wenye matatizo ya hitilafu ya mfumo wa moyo na wale ambao mioyo yao imeshindwa kufanya kazi (Heart failure) wamefanyiwa upasuaji mdogo wa moyo katika kambi hiyo. Wataalam wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Kwa kushirikiana na mwenzao kutoka Hospitali ya Max iliyopo nchini India Dkt. Viveka Kumar wakiusoma mfumo wa umeme wa moyo wa mgonjwa ambaye ana hitilafu ya mfumo wa umeme wa moyo wakati wa upasuaji mdogo wa moyo kwa kutumia tundu dogo (Minimum Invasive Surgery) katika kambi maalum ya siku nne iliyomalizika leo katika Taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam. Na: JKCI ***************************************

Kwa mara ya kwanza wataalam wazawa wazibua mishipa pacha ya moyo iliyozi...

Image

Khakoo aizawadia JKCI ndoo nane za rangi zenye thamani ya Tshs. 1,500,000

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akipokea zawadi ya ndoo nane za rangi zenye thamani ya Tshs. 1,500,000 kutoka kwa mdau wa JKCI Akhter Khakoo kwa ajili ya matumizi ya Taasisi hiyo, zawadi hizo zimetolewa leo Jijini Dar es Salaam. Mhandisi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Haji Mbuta akipokea rola nne za kupakia rangi kutoka kwa mdau wa Taasisi hiyo Akhter Khakoo zilizotolewa leo Jijini Dar es Salaam pamoja na ndoo nane za rangi kwa ajili ya matumizi ya JKCI. Afisa Ugavi na Ununuzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Getrude Mnaye na Mhandisi wa JKCI Haji Mbuta wakikagua ndoo za rangi zenye thamani ya Tshs. 1,500,000 zilizotolewa na mdau wa Taasisi hiyo Akhter Khakoo kwa ajili ya matumizi ya JKCI leo Jijini Dar es Salaam Picha na: JKCI ****************************************************************************

Wataalamu wa Afya washiriki mafunzo ya kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (Echo-Cardiograph)

Image
  Mhadhiri mwandamizi na Dakatri bingwa wa magonjwa ya moyo kutoka Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Pilly Chillo akizungumza na washiriki wa mafunzo ya mwezi mmoja ya kufanya uchunguzi wa jinsi moyo unavyofanya kazi (Echo-Cardiograph) wakati wa uzinduzi wa mafunzo  hayo yaliyoandaliwa na (MUHAS) kwa kushirikiana na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa wataalam wa afya kutoka hospitali mbalimbali nchini. Mkugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akizungumza na washiriki wa mafunzo ya mwezi mmoja ya kufanya uchunguzi wa kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (Echo-Cardiograph) wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo yaliyoandaliwa na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) kwa kushirikiana na JKCI na Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa wataalam wa afya kutoka hospitali mbalimbali nchini. Wataalam wa afya kutoka hospitali mbalimbali nchini wanaoshiriki mafunzo

Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wafuturu pamoja

Image
Baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiwa katika foleni ya kuchukua futari iliyoandaliwa na Idara ya Tiba Shirikishi kwa ajili ya mfungo mtukufu wa Ramadhani na kufanyika hivi karibuni katika ukumbi wa Taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam. Futari hiyo imedhaminiwa na kampuni ya dawa za binadamu ya Ajanta Pharm Ltd Baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifuturu wakati wa futari iliyoandaliwa na Idara ya Tiba Shirikishi kwa ajili ya mfungo mtukufu wa Ramadhani na kufanyika hivi karibuni katika ukumbi wa Taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam. Futari hiyo imedhaminiwa na kampuni ya dawa za binadamu ya Ajanta Pharm Ltd Meneja wa Kanda wa kampuni ya dawa za binadamu ya Ajanta Pharm Ltd. Kumar Bangaru akiwasalimia wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete walioshiriki katika futari iliyodhaminiwa na kampuni hiyo na kufanyika hivi karibuni katika ukumbi wa Taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam  Picha na: JKCI

JKCI: Wanaotaka kusaidia matibabu waje kuwatambua wagonjwa

Image
Mwenyekiti wa Mfuko wa Hisani wa Kujitolea, Kuongoza na Kubadilisha Beatus Rwechungura akimkabidhi risiti ya malipo ya Tshs.2,655,000/= Edna Michael  leo jijini Dar es Salaam kwa ajili ya gharama za upasuaji wa moyo wa mtoto wake anayesubiri kufanyiwa upasuaji katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI). Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akiwaeleza wadau kutoka Mfuko wa Hisani wa Kujitolea, Kuongoza na Kubadilisha kuhusu magonjwa ya moyo kwa watoto walipotembelea Taasisi hiyo  leo kwa ajili ya kukabidhi risiti za malipo  ya Tshs.8,750,000/= ikiwa ni gharama za upasuaji wa moyo kwa watoto watatu. Kulia ni Ramadhani Iddi ambaye mtoto wake amelipiwa  Tshs.2,895,000/= kwa ajili ya upasuaji wa moyo. Mwenyekiti wa Mfuko wa Hisani wa Kujitolea, Kuongoza na Kubadilisha Beatus Rwechungura akimkabidhi risiti ya malipo ya Tshs.2,655,000/= Edna Michael   leo jijini Dar es Salaam kwa ajili ya gharama za upasuaji wa moyo wa mtoto wake anayesubiri kufa

Appreciation for successful surgeries

Image
 

Kwa mara ya kwanza wataalamu wazawa wazibua mishipa pacha ya moyo iliyoziba kwa asilimia 95

Image
  Wataalamu  wazawa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakimzibua mgonjwa   mishipa miwili iliyokuwa inapeleka damu kwa wakati mmoja kwenye moyo (mishipa pacha ya damu – bifurcation lesion) iliyokuwa imeziba kwa asilimia 95 na kupata shida ya kupitisha damu. Uzibuaji wa mishipa hiyo ulifanyika kwa njia ya upasuaji wa moyo kwa kutumia tundu dogo (Minimum Invasive Surgery) bila kufungua kifua kwa kutoboa mshipa kwenye paja (Percutaneous Coronary Angioplasty) kwa kutumia mtambo wa Cathlab (Catheterization Laboratory) ambayo ni maabara inayotumia mionzi maalum kwa ajili ya uchunguzi na tiba za magonjwa ya moyo. ************************************************************************************************************************************************************************************************************************************** Kwa mara ya kwanza wataalamu wazawa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wamezibua mishipa miwili il

Wagonjwa 19 wazibuliwa mishipa ya damu ya moyo iliyoziba kwa asilimia 100

Image

Wanafunzi wa shule ya Heaven of Peace Academy ya jijini Dar es Salaam watembelea JKCI kwa ajili ya kujifunza magonjwa ya moyo

Image
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mafunzo na Utafiti wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Pedro Pallangyo akiwaelezea huduma zinazotolewa na Taasisi hiyo wanafunzi kutoka shule ya Heaven of Peace Academy ya jijini Dar es salaam waliotembelea JKCI kwa ajili ya kujifunza magonjwa ya moyo ikiwa ni sehemu ya kupata mafunzo kwa vitendo. Wanafunzi hao wako katika Taasisi hiyo kwa muda wa siku tatu kwa ajili ya kujifunza magonjwa hayo pamoja na kuona huduma za matibabu zinavyotolewa. Mkuu wa Idara ya Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Salma Wibonela akiwafundisha taratibu za kuzuia na kujikinga na maambukizi wanafunzi kutoka shule ya Heaven of Peace Academy ya jijini Dar es Salaam wakati waliotembelea Taasisi hiyo kwa ajili ya kujifunza magonjwa ya moyo ikiwa ni sehemu ya kupata mafunzo kwa vitendo. Wanafunzi hao wako katika Taasisi hiyo kwa muda wa siku tatu kwa ajili ya kujifunza magonjwa hayo pamoja na kuona huduma za matibabu zinavyotolewa. Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mafu

Watoto 40 wafanyiwa uchunguzi, 21 kati yao watibiwa katika kambi maalum ya matibabu ya moyo iliyofanywa na JKCI kwa kushirikiana na Israel

Image
Wataalamu wa  usingizi na wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao kutoka Shirika la Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart – SACH) la nchini Israel wakimlaza  mtoto kabla ya kufanyiwa upasuaji wa kuzibua mshipa wa damu wa moyo kwa kutumia tundu dogo (Minimum Invasive Surgery)  katika kambi maalum ya siku tano ya matibabu ya moyo iliyomalizika leo jijini Dar es Salaam. Katika kambi hiyo watoto 40 wenye matatizo ya moyo ya kuzaliwa nayo walifanyiwa uchunguzi ambapo 21 kati yao walifanyiwa upasuaji wa kuziba matundu na kuzibuliwa mishipa ya damu ya moyo.  Wataalamu wa  Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao kutoka Shirika la Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart – SACH) la nchini Israel wakimfanyia mtoto upasuaji wa kuziba tundu kwenye moyo kwa kutumia tundu dogo (Minimum Invasive Surgery)   katika kambi maalum ya siku tano ya matibabu ya moyo iliyomalizika leo jijini Dar es Salaam. Katika kambi hiyo watoto 40