Khakoo aizawadia JKCI ndoo nane za rangi zenye thamani ya Tshs. 1,500,000
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
Prof. Mohamed Janabi akipokea zawadi ya ndoo nane za rangi zenye thamani ya
Tshs. 1,500,000 kutoka kwa mdau wa JKCI Akhter Khakoo kwa ajili ya matumizi ya
Taasisi hiyo, zawadi hizo zimetolewa leo Jijini Dar es Salaam.
Mhandisi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Haji Mbuta akipokea rola nne za kupakia rangi kutoka kwa mdau wa Taasisi hiyo Akhter Khakoo zilizotolewa leo Jijini Dar es Salaam pamoja na ndoo nane za rangi kwa ajili ya matumizi ya JKCI.
Afisa Ugavi na Ununuzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
(JKCI) Getrude Mnaye na Mhandisi wa JKCI Haji Mbuta wakikagua ndoo za rangi zenye
thamani ya Tshs. 1,500,000 zilizotolewa na mdau wa Taasisi hiyo Akhter Khakoo
kwa ajili ya matumizi ya JKCI leo Jijini Dar es Salaam
Picha na: JKCI
****************************************************************************
Comments
Post a Comment