Khakoo aizawadia JKCI ndoo nane za rangi zenye thamani ya Tshs. 1,500,000

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akipokea zawadi ya ndoo nane za rangi zenye thamani ya Tshs. 1,500,000 kutoka kwa mdau wa JKCI Akhter Khakoo kwa ajili ya matumizi ya Taasisi hiyo, zawadi hizo zimetolewa leo Jijini Dar es Salaam.

Mhandisi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Haji Mbuta akipokea rola nne za kupakia rangi kutoka kwa mdau wa Taasisi hiyo Akhter Khakoo zilizotolewa leo Jijini Dar es Salaam pamoja na ndoo nane za rangi kwa ajili ya matumizi ya JKCI.

Afisa Ugavi na Ununuzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Getrude Mnaye na Mhandisi wa JKCI Haji Mbuta wakikagua ndoo za rangi zenye thamani ya Tshs. 1,500,000 zilizotolewa na mdau wa Taasisi hiyo Akhter Khakoo kwa ajili ya matumizi ya JKCI leo Jijini Dar es Salaam

Picha na: JKCI

****************************************************************************

Comments

Popular posts from this blog

JKCI na Burkina Faso zasaini makubaliano ya ushirikiano katika kutoa tiba ya magonjwa ya moyo

Wanawake waaswa kulinda mioyo yao, kuepuka sukari na chumvi kupita kiasi

Msumbiji kushirikiana na JKCI katika tiba ya moyo