Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wafuturu pamoja
Baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
(JKCI) wakiwa katika foleni ya kuchukua futari iliyoandaliwa na Idara ya Tiba
Shirikishi kwa ajili ya mfungo mtukufu wa Ramadhani na kufanyika hivi karibuni
katika ukumbi wa Taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam. Futari hiyo imedhaminiwa na
kampuni ya dawa za binadamu ya Ajanta Pharm Ltd
Baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
(JKCI) wakifuturu wakati wa futari iliyoandaliwa na Idara ya Tiba Shirikishi
kwa ajili ya mfungo mtukufu wa Ramadhani na kufanyika hivi karibuni katika
ukumbi wa Taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam. Futari hiyo imedhaminiwa na
kampuni ya dawa za binadamu ya Ajanta Pharm Ltd
Meneja wa Kanda wa kampuni ya dawa za binadamu ya Ajanta
Pharm Ltd. Kumar Bangaru akiwasalimia wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete walioshiriki katika futari iliyodhaminiwa na kampuni hiyo na kufanyika
hivi karibuni katika ukumbi wa Taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam
Picha na: JKCI
Comments
Post a Comment