Posts

Showing posts from January, 2025

JKCI yapongezwa kwa kutoa huduma za kibingwa za matibabu ya moyo barani Afrika

Image
Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Nicole Kanyawa akimwelezea huduma zinazotolewa na taasisi hiyo Msanii wa Muziki nchini Mrisho Mpoto atembelea banda la Taasisi hiyo lililiokuwa katika mkutano wa nishati wa wakuu wa nchi za Afrika jijini Dar es Salaam. Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Alex Benjamini akimuelezea namna moyo unavyofanya kazi mshiriki wa mkutano wa nishati wa wakuu wa nchi za Afrika kutoka nchini Malawi alipotembelea banda la Taasisi hiyo jijini Dar es Salaam. Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Nicole Kanyawa akimuelezea namna taasisi hiyo inavyofanya utalii tiba mshiriki wa mkutano wa nishati wa wakuu wa nchi za Afrika kutoka nchini Djibouti alipotembelea banda la taasisi hiyo jijini Dar es Salaam. Daktari kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika Nelly Iteba akizungumza na wataalamu wa afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kuhusu masuala ya tiba utalii alipotembelea banda la JKCI...

Tanzania yapaa matibabu ya moyo kimataifa

Image
Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama akikata utepe wakati wa uzinduzi wa kliniki ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) tawi la Oysterbay lililopo Oyster plaza Haile Salassie barabara ya Ali Bin Said leo jijini Dar es Salaam. Afisa Lishe wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Husna Faraji akimuelezea Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama huduma inayotolewa na kitengo cha Lishe kwa wagonjwa wa moyo wakati wa uzinduzi wa kliniki mpya ya Taasisi hiyo iliyopo Oysterbay leo jijini Dar es Salaam. Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama akimsikiliza daktari bingwa wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Smita Bhalia wakati wa uzinduzi wa Kliniki ya Oysterba leo jijini Dar es Salaam. Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama akiwajulia hali wagonjwa waliofika kutibiwa katika kliniki ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) tawi la Kawe alipotembelea Kliniki hiyo leo jijini Dar es Salaam. Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama akimsikiliza mgonjwa aliyefika kutibiwa katika kliniki ya Taasisi ya Mo...

Wazibwa matundu ya moyo kwa kutumia mashine ya ECHO

Image
Wataalamu wa Afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao kutoka Hospitali ya Fuwai iliyopo Beijing nchini China wakimfanyia mtoto upasuaji wa kuziba tundu lililopo kwenye moyo bila kufungua kifua kwa kutumia mashine ya kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (Echocardiography – ECHO). Upasuaji huo umefanyika bila kutumia mashine za mionzi kwa watoto 5. Wataalamu wa Afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao kutoka Hospitali ya Fuwai iliyopo Beijing nchini China wakiangalia muonekano wa moyo wa mtoto katika  mashine ya kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (Echocardiography – ECHO) wakati wakiendelea na upasuaji wa kuziba tundu lililopo kwenye moyo bila kufungua kifua kwa kutumia mashine hiyo jana jijini Dar es Salaam. Upasuaji huo umefanyika bila kutumia mashine za mionzi kwa watoto 5. Wataalamu wa Afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao kutoka Hospitali ya Fuwai iliyopo Beijing nchini China wakiandaa vifaa kwaajili ya kumfanyia mtoto upasuaji...

JKCI wafundishwa teknolojia ya kisasa ya kuziba matundu ya moyo

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akiwa katika picha ya pamoja na Wataalamu wa afya kutoka Hospitali ya Fuwai iliyopo Beijing China na wengine wa JKCI mara baada ya mafunzo ya jinsi ya kuziba matundu na kuzibua mishipa ya damu ya moyo iliyoziba bila kutumia mashine ya mionzi leo katika taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na wataalamu wa afya kutoka Hospitali Fuwai iliyopo Beijing China leo wakati wataalamu hao walipofika JKCI kwaajili ya kubadilishana ujuzi na wenzao wa JKCI katika kutoa huduma za upasuaji mdogo wa moyo bila kutumia mashine ya mionzi kwa watoto wenye magonjwa ya moyo. Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Fuwai iliyopo Beijing China prof. Xiangbin Pan akielezea namna huduma za upasuaji mdogo wa moyo bila kutumia mionzi zinavyoweza kufanyika kirahisi kutokana na maendeleo ya teknolojia wakati wa mafunzo ya jinsi ya kuziba matundu na ...

JKCI kupunguza msongamano wa wagonjwa kupitia kliniki zake

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na wafanyakazi wa Taasisi hiyo jana wakati wa kikao cha wafanyakazi kujadili maendeleo ya Taasisi hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa JKCI uliopo jijini Dar es Salaam. Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakisikiliza wakati wa kikao cha wafanyakazi kilichofanyika jana katika ukumbi wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam Mkuu wa Kitengo cha Tehama wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Lazaro Swai akielezea namna mifumo ya Tehama inavyofanya kazi wakati wa kikao cha wafanyakazi kujadili maendeleo ya Taasisi hiyo kilichofanyika jana katika ukumbi wa JKCI uliopo jijini Dar es Salaam. Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Evarist Nyawawa akichangia mada wakati wa kikao cha wafanyakazi kujadili maendeleo ya Taasisi hiyo kilichofanyika jana katika ukumbi wa JKCI uliopo jijini Dar es Salaam. Daktari bingwa wa mfumo wa um...

Mhe. Balozi Mpoki apongezwa kwa kazi nzuri JKCI

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) Mhe. Balozi Ulisubisya Mpoki akizungumza na wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa hafla fupi ya kumuaga iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Dkt. Peter Kisenge. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimpa zawadi Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) Mhe. Balozi Ulisubisya Mpoki kumpongeza na kumshukuru kwa kazi nzuri aliyoifanya wakati akiwa JKCI wakati wa hafla fupi ya kumuaga iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam.  Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiwa wameshikana mikono na kuimba wimbo wa mshikamano baina ya wafanyakazi hao wakati wa hafla fupi ya kumuaga aliyekuwa Daktari bingwa wa usingizi JKCI ambaye sasa ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) Mhe. Balozi Ulisubisya Mpoki jana jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete ...

Wafamasia watakiwa kufanya kazi kwa kufuata mifumo na taratibu za Taasisi

Image
Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Dkt. Tatizo Waane akimkabidhi zawadi mfamasia aliyemaliza mafunzo ya miezi sita kwa vitendo (Internship) Moza Salimu wakati wa hafla fupi ya kuwaaga wafamasia waliomaliza muda wa mafunzo na kuwakaribisha wafamasia wanaoanza mafunzo kwa vitendo katika ukumbi wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Dkt. Tatizo Waane akimpatia cheti mfamasia aliyemaliza mafunzo ya miezi sita kwa vitendo (Internship) Farahani Nikuli wakati wa hafla fupi ya kuwaaga wafamasia waliomaliza muda wa mafunzo na kuwakaribisha wafamasia wanaoanza mafunzo kwa vitendo katika ukumbi wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Dkt. Tatizo Waane akimpatia cheti mfamasia aliyemaliza mafunzo ya miezi sita kwa vitendo (Internship) Edington Nkuba wakati wa hafla fupi ya kuwaaga wafamasia waliomaliza muda wa mafunzo ...

Mkutano wa kimataifa wa magonjwa ya moyo (CardioTan) 2025

Image

Watu wenye ulemavu 188 wapima moyo Dar

Image
Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mohamed Aloyce akizungumza na mtu mwenye ulemavu mara baada ya kupima vipimo vya moyo wakati wa hafla fupi ya chakula cha mchana na zawadi kwa watu hao iliyoandaliwa na Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao na kufanyika jana katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Fatma Suedy akimpima shinikizo la damu msanii wa muziki wa dansi Patcho Mwamba wakati wa hafla fupi ya chakula cha mchana na zawadi kwa watu wenye ulemavu iliyoandaliwa na Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao na kufanyika jana katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Happiness Shirima akimpima wingi wa sukari kwenye damu msanii wa muziki wa dansi kutoka bendi ya FM Academia Pablo Masai wakati wa hafla fupi ya chakula cha mchana na zawadi kwa watu wenye ulemavu iliyoandaliwa na Taasisi ya Mama...